nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
[h=2][/h]JUMATANO, AGOSTI 15, 2012 06:08 NA AZIZA HASSAN, DAR ES SALAAM
MJUMBE wa Mkutano Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Godfrey Chikandamwali, amejivua gamba. Wakati wa kukabidhi barua yake katika Ofisi za Tawi la la CCM lililopo Sinza E, Kata ya Sinza, ulizuka mtafaruku baina ya Katibu wa tawi hilo, Muhidini Mavufa na Chikandamwali.
Katibu wa huyo alikuwa anashangaa ujio wa waandishi wa habari na kusema yeye si msemaji wa tawi.
Sielewi barua hiyo ina nini na mimi si kwamba sitaki kupokea barua kwa kuwa barua ni kitu cha kawaida na unaweza kuleta muda wowote na God hajakosea kuleta barua hapa, ila alichokosea ni kuja na waandishi wa habari na mimi si msemaji.
Pia God ni mwanachama wetu na sina taarifa kama kuna mgogoro wa aina yoyote katika tawi letu na wana CCM, lakini nashangaa kaniletea barua, waziache hapa nitazisoma kwa muda wangu nini kilichopo hapa ndani ya barua.
Kwanza unajitoa kwa sababu ulikosa kura wakati uliomba uongozi, ungepata usingejitoa, umeishiwa ndio maana umeamua kujitoa CCM, alisikika mwanachama mmoja aliyekuwamo katika ofisi hizo.
Kwa upande wake, Chikandamwali, alisema amefika katika ofisi hiyo ya tawi lengo likiwa ni kujitoa uwanachama ili aishi kwa amani.
Nashangaa nafika hapa kukabidhi barua Katibu anataka akatae na kuniambia nipeleke Makao Makuu ya Kata, lakini Katiba ya CCM inasema ulipojiunga uanachama ndio utakapojitoa, kama mimi na mke wangu ulivyofanya, alisema Chikandamwali.
Alisema amekuwa alihujumiwa katika uchaguzi wa mwaka 2009 alipogombea uenyekiti wa mtaa akashinda katika kura za maoni na baada ya hapo jina lake likakatwa na kupewa mtu aliyeshika nafasi ya pili.
Niligombea na kupata kura za uenyekiti na udiwani mwaka 2010, lakini wana CCM wakanihujumu, wakanizushia kesi nikaambiwa mimi jambazi namiliki silaha, mara nimebaka pia nimekuwa nikifanyiwa hujuma katika biashara zangu, alisema Chikandamwali.
MJUMBE wa Mkutano Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Godfrey Chikandamwali, amejivua gamba. Wakati wa kukabidhi barua yake katika Ofisi za Tawi la la CCM lililopo Sinza E, Kata ya Sinza, ulizuka mtafaruku baina ya Katibu wa tawi hilo, Muhidini Mavufa na Chikandamwali.
Katibu wa huyo alikuwa anashangaa ujio wa waandishi wa habari na kusema yeye si msemaji wa tawi.
Sielewi barua hiyo ina nini na mimi si kwamba sitaki kupokea barua kwa kuwa barua ni kitu cha kawaida na unaweza kuleta muda wowote na God hajakosea kuleta barua hapa, ila alichokosea ni kuja na waandishi wa habari na mimi si msemaji.
Pia God ni mwanachama wetu na sina taarifa kama kuna mgogoro wa aina yoyote katika tawi letu na wana CCM, lakini nashangaa kaniletea barua, waziache hapa nitazisoma kwa muda wangu nini kilichopo hapa ndani ya barua.
Kwanza unajitoa kwa sababu ulikosa kura wakati uliomba uongozi, ungepata usingejitoa, umeishiwa ndio maana umeamua kujitoa CCM, alisikika mwanachama mmoja aliyekuwamo katika ofisi hizo.
Kwa upande wake, Chikandamwali, alisema amefika katika ofisi hiyo ya tawi lengo likiwa ni kujitoa uwanachama ili aishi kwa amani.
Nashangaa nafika hapa kukabidhi barua Katibu anataka akatae na kuniambia nipeleke Makao Makuu ya Kata, lakini Katiba ya CCM inasema ulipojiunga uanachama ndio utakapojitoa, kama mimi na mke wangu ulivyofanya, alisema Chikandamwali.
Alisema amekuwa alihujumiwa katika uchaguzi wa mwaka 2009 alipogombea uenyekiti wa mtaa akashinda katika kura za maoni na baada ya hapo jina lake likakatwa na kupewa mtu aliyeshika nafasi ya pili.
Niligombea na kupata kura za uenyekiti na udiwani mwaka 2010, lakini wana CCM wakanihujumu, wakanizushia kesi nikaambiwa mimi jambazi namiliki silaha, mara nimebaka pia nimekuwa nikifanyiwa hujuma katika biashara zangu, alisema Chikandamwali.