TinyMonster
JF-Expert Member
- Jun 15, 2009
- 248
- 154
Askari wa jeshi la wananchi JWTZ wilayani Ngara wanadaiwa kuwanyanyasa wananchi wa wilaya hiyo. Inadaiwa wanajeshi hao wamekuwa wakiwanyanyasa wananchi hao kwa kigezo cha kuwaita wanyarwanda. Mwezi uliopita Waziri wa Mambo ya ndani Mh Shamsi Vuai Nahodha baada ya kutembelea wilaya hiyo na kujionea mgogoro uliokuwepo kati ya wakulima wa wilayani humo na wafugaji waliovamia vijiji vilivyo mpakani wakitokea nchini Rwanda na kusababisha vifo vya wakulima kadhaa liamuru jeshi la wananchi kufanya safisha safisha katika mapori ya wilaya hiyo ambako kunadaiwa wafugaji hao wamekimbilia, lakini matokeo yake wanajeshi hao wamekuwa wakienda vijijini na kuwakamata wananchi wasiokuwa na vitambulisho vya mpiga kura na kuwaita wakimbi na ili kuwaachia inabidi watoe kitu kidogo. Pia wamekuwa wakikamata ngombe wa wafugaji wa wilayani humo na kulazimisha wananchi hao kutoa shilingi 50,000 kwa kila ngombe na wanaposhindwa inadaiwa wanawashikilia na kuwauza.
Sasa wanajamvi ninachojiuliza, Hawa ndugu zetu waliopewa kazi ya kulinda mipaka yetu kama wanaanza kufanya madudu tuliyozoea kuyaona kwa jeshi la Polisi.. hivi tutakuwa wageni wa nani nchi hii?
Sasa wanajamvi ninachojiuliza, Hawa ndugu zetu waliopewa kazi ya kulinda mipaka yetu kama wanaanza kufanya madudu tuliyozoea kuyaona kwa jeshi la Polisi.. hivi tutakuwa wageni wa nani nchi hii?