John Jambele "Mjesani" na Uongozi wa Yanga

yusufummaka

Member
Apr 7, 2012
30
20
Hongera "Mjesani" kwa kuipenda club yetu ya Yanga hadi kutamani kuiongoza katika ngazi yake ya juu. Ninakufahamu sana John tangu ulipokuwa Tanga kwenye mashamba ya Mjesani na Mwinduro, shuleni, chuoni na Maramba JKT. Tulikuwa marafiki wa hapa na pale, nakujua ulivyokuwa mbishi wa kila kitu kinavyojadiliwa mbele yako. Lakini hili la yanga waachie wenye pesa waindeshe klabu. Mpira wa leo duniani kote unahitaji fedha nyingi tofauti na zama zile za akina Daud Salum, Kampila na Mahadhi. Wachezaji wa zamani walikuwa wanatoka kwenye kambi za mashamba ya mkonge, tumbaku, mpira na kakao. Hivi leo wachezaji wanatoka Nigeria, Ghana, Kongo, East Africa, Zambia, etc. Hawa wahataka pesa nyingi pamoja na kocha wao. Lazima kiongozi pamoja na mapenzi ya klub pia sharti awe na fweza. Angalia club za Ulaya zote zinavyokabidhiwa kwa matajiri kutoka kwa viongozi wazawa na mashabiki. Acha, acha, acha kabisa habari yako hiyo, wewe huna fweza, utategemea kutembeza bakuri na kupiga magoti kwa matajiri. Wanachama na mashabiki wa Yanga tupo wengi kweli, lakini hatuna kitu, tunashindwa hata kumudu milo 3 kamili kwa siku itakuwa kuchangia club? Najua unaipenda Yanga lakini............
 
Umenena vema sana Mkuu,wakati huu tunahitaji mabadiriko...kwa mtazamo wangu pamoja na kutaka kuitumia haki yake ya uanachama wa Yanga ya kuchagua na kuchaguliwa lkn ningependa kuongezea kumshauri huyu Bwana John Jambele kukaa pembeni na kuwaacha wenye fedha wajaribu kuivusha Club yetu kwenda level nyingine,Yanga imeongozwa sana na Viongozi sampuli yake na ya kina Rage,sasa ni kipindi cha kujaribu Viongozi wa sampuli ya kina Moize Katumbi ili kuona itachukua muda gani kwa Club yetu kufikia level iliyofikiwa na TP Mazembe.
 
rage msanii,mpaka sasa hajafanya lolote...tunataka wenye pesa sasa!
 
Umenena vema sana Mkuu,wakati huu tunahitaji mabadiriko...kwa mtazamo wangu pamoja na kutaka kuitumia haki yake ya uanachama wa Yanga ya kuchagua na kuchaguliwa lkn ningependa kuongezea kumshauri huyu Bwana John Jambele kukaa pembeni na kuwaacha wenye fedha wajaribu kuivusha Club yetu kwenda level nyingine,Yanga imeongozwa sana na Viongozi sampuli yake na ya kina Rage,sasa ni kipindi cha kujaribu Viongozi wa sampuli ya kina Moize Katumbi ili kuona itachukua muda gani kwa Club yetu kufikia level iliyofikiwa na TP Mazembe.

WELL SAID MKUU!!! Tena wangejitoa tu hawana jipya tumewachoka :israel:
 
Na hao mambumbumbu akina kitenge wanakupigia debe Jambili ili tu wamtumikie bwana wao Mengi, Eti mwanahabari anataka atafutwe na Mgombea? utawapata hao hao wenye njaa kama wewe. Lakini usichoke kitenge na radio one yako endelea kupigia debe wanao kutafuta. siku zote habari hutafutwa bwana vipi wewe au umevuta !
 
pesa fweza hela ... haya bana!
tunataka viongozi waliokuliwa vyoovya kuvuta na sio waliokulia vyoo vya kuchimba. Usimpe kiongozi fukara uongozi maana ataanza kwanza kujenga choo cha kuvuta wakati timu ipo mashindanoni! hata jali kama timu inashindwa mpaka amlize kujenga choo cha kuvuta!
 
Nimefuatilia michango ya wote hapa jamvini pamoja na huko nje. Lakini nimegundua kuna tatizo kwenye kufikiri na kulinganisha kwa watu wengi.

Nakubaliana na wote kwamba Yanga inahitaji watu wenye pesa ili iweze kupiga hatua katika soka si Tanzania tu bali hata Afrika na Duniani kote. Ili Yanga ipate pesa si lazima iwe na mwenyekiti mwenye pesa asiye kuwa na mtu wa kuwajibisha kama anavyotaka kufanya Manji.

Yanga inahitaji matajiri kweli lakini kwa aina ya matajiri wenye agenda zilizojificha kama za Manji na chelea kusema ni hatari na hatari kabisa.

Kwa research yangu ndogo na ya uhakika nimegundua kwamba Manji ndiye aliyeifanya Yanga isifanye vizuri kwa miaka ya hivi karibuni. Yeye kama mfadhili mkuu na anayetegemewa angekuwa thabiti leo Yanga isingekuwa hivi huku akidai ameshatumia mabilioni kuisaidia. Mmambo yako mengi sana.

1. Aligoma kabisa kutaja kiasi anachojitolea ku sponsor Yanga, iwe kama grant au mkopo. Kwa hali hiyo hakuna anayejua Manji anategemea kutoa kiasi gani kwa mwaka kwa Yanga. Hii imesababisha wenyeviti wengi kuonekana wajinga maana wanakuwa hawajui wategemee kiasi gani ili waweze kuplan uendeshaji. Nani anaweza kuishi maisha bora kama ana matarajio ya nini atapata kesho. Kuna watu wanafanya biashara wanaingiza hata milion kwa mwezi. Lakini maisha yao yanazidiwa na mfanyakazi anayepata laki 5 kwa mwezi, simply kwa vile ana uhakika wa kupata kila mwezi wakati mfanyabiashara huyu hana.

2. Manji amekuwa akitumia pesa bila mpangilio. Mfano wakati Yanga ilikuwa inahitaji pesa ya kusajili wachezaji wazuri yeye alijitolea kuwalipia wanachama ada yao ya mwezi kiasi cha sh 90m bila sababu, huku akikataa kulipia usajili wa wachezaji. Aliwahi kutoa sh 50m eti Madega na wazee watumia kuifunga Simba huku wachezaji wa Yanga wakilia njaa. Amekuwa akitoa pesa kusajili wachezaji kama akina Jama Mba, Mwape na makapi mengi mengi. Kweli tujiulize kama yeye ni kilaza wa mpira kiasi hicho kiasi cha kutojua wachezaji wazuri wakoje ndio ataongoza Yanga ambayo ni timu ya mpira? Si hayo tu watu kibao wana ishi kwa kutumia pesa yake. Cha kujiuliza ili iweje???

3. Kama Mfadhili alikuwa na uwezo wa kulazimisha Policy za kusaidia Yanga ili kuendelea. Mfano kama usajili wa wachezaji ungekuwa na policy kuwa mchezaji wa kigeni lazima awe kwenye timu ya taifa lake, umri wake usizidi miaka kadhaa, na taifa lake liwe juu kisoka kuliko Tanzania, tungeshindwa kuivusha Yanga na kuifanya timu kubwa? Tulikuwa na wafadhili ambao hawakuwa na pesa labda kama za Manji lakini mbona Yanga ilikuwa vizuri ukilinganisha na huyu Manji.

4. Manji amekuwa akiwalazimisha wenyeviti wa sign mikataba ya kumnufaisha Manji, mfano kuwa kutumia nembo ya Yanga n.k. Pindi wanapokataa Manji amekuwa akitumia watu wake ku-wasabbotage na kuwafukuza kwenye uongozi. Mfano ili la Nchunga. Katumia watu kuivuruga timu kufanya vibaya, akatumia wazee kujitapa eti wana pesa na kuinyima pesa timu akama alivyo ahidi na ikashindwa kulipa mishahara ya wachezaji n.k. Mwana Yanga gani yuko tayari kuiona Yanga ikifungwa 5 na Simba simply uongozi uonekane haufai?

Nakubaliana na wote kwamba Yanga inahitaji wenye fedha. Lakini kama wenye fedha ni kama Manji sioni kama wanaifaa Yanga. Nashauri badala ya kumshauri Jambele ajitoe, tumshauri Manji ajitoe na abakie mfadhili mwenye nia thabiti ya kuifanikisha Yanga. Watu wanatoa mifano ya timu za ulaya, bila kuelewa wenzetu matajiri wao ni watu wa aina gani. Matajiri wanatoa pesa kulingana na mipango fulani, sio kutoa pesa ili kujulikana wana pesa. Mfano toa pesa Yanga iwe bingwa wa Africa, na kwa hali hoyo utalazimika kununua wachezaji wa hadhi ya TP MAZEMBE. Tajiri wa TP Mazembe anatoa pesa mwanzo wa msimu say USD 10m na kuipa timu ili itimize lengo fulani.

Manji ni binadamu anaweza kufa, kufilisika au kufungwa japo simuombei mabaya. Mwenye mipango ya kuifanya Yanga ijitegemee ndiye tunayemtaka. Timu kumilikiwa na matajiri hata ulaya wameanza kuistukia ndio maana wanakuja na policy za kudhibiti kama "Financial Fair Play".

Najua mtamchagua lakini mimi nitamnyima kura yangu maana ana "hidden agenda"

YANGA DAIMA MBELE NYUMA MWIKO
 
hizo fikra zenu FINYU ndizo zinazowafanya mmewaweka wabunge kama akin DEWJI, MURJI na masingasinga mwngne pale bungeni ambao hawana mchango wowote pale bungeni zaidi kugonga meza eti tu kwasababu ya utajiri wao.. Yanga kama yanga inatakiwa ijiendeshe kwa mapato yake na resources zake ilizonazo na sio kwa utajiri wa mwenyekiti au viongozi. Labda awe ni mmiliki
 
Kama mna ugonvi na akina Manji basi mumshawishi tajiri mwingine kama Mengi, Kifukwe, n.k wajitokeze waziwazi waiongoze timu moja kwa moja, lakini sio kumtumia mtu sampuli ya akina Jambele na wenzake wagombee ili waanze kutembeza bakuli la kulipa wachezaji mishahara. Hatutaki ubabaishaji wa hivyo.
 
Duniani kote sasa hivi hakuja timu ya mpira inayojiendesha kwa mapato yake. Timu za ulaya kaibu zote zimeuzwa kwa matajiri wa kirusi, kiarabu na kimarekani. Arsernal ilijaribu kujiendesha kwa mapato yake, lakini wapi unaona wachezaji wanavyokimbia club. Mpira ni pesa sio maneno na porojo kama za John Jambele na wengine "pangu pakavu". Tunajua tukimchagua ashike Club atampa ukocha mtu wa design kama Juma Mgunda, Mkwasa ama Julio wasio na gharama. HATUTAKI, hata ulaya makocha wao huwa wanatoka nje ya nchi yao kama Wenger, Mancini, Morinho, Erickson, n.k. makocha wa aina hii hawawezi kulipwa kwa shilingi 1000 za mashabiki, we acha wee!
 
Umenena vema sana Mkuu,wakati huu tunahitaji mabadiriko...kwa mtazamo wangu pamoja na kutaka kuitumia haki yake ya uanachama wa Yanga ya kuchagua na kuchaguliwa lkn ningependa kuongezea kumshauri huyu Bwana John Jambele kukaa pembeni na kuwaacha wenye fedha wajaribu kuivusha Club yetu kwenda level nyingine,Yanga imeongozwa sana na Viongozi sampuli yake na ya kina Rage,sasa ni kipindi cha kujaribu Viongozi wa sampuli ya kina Moize Katumbi ili kuona itachukua muda gani kwa Club yetu kufikia level iliyofikiwa na TP Mazembe.
Moize Katumbi ga ni mmiliki wa timu sio kiongozi kama kwenye vilabu vyetu vya simba au yanga
 
Back
Top Bottom