JK: Sina mpango kuvunja Baraza

Ukisoma mahojiano na JK kwenye The Citizen, :

Bonyeza hapa: http://www.thecitizen.co.tz/newz.php?id=1964


Ngoja nijaribu kuingia katika akili za Mkuu wetu wa Nchi kutokana na kuyatafakari mahojiano hayo:

Mosi; Rais anampango wa kuvunja baraza la mawaziri lakini asingependa iwe ni kwa msukumo toka nje-ndio maana kwa sasa ameuita uvumi

Pili; Rais ana mpango wa kupunguza ukubwa wa baraza la Mawaziri- lakini hataki ionekane ni mwa msukumo kutoka nje, anataka iwe bayana kuwa ni kwa kuwa wameshatimiza malengo

Tatu; Rais aliunda kamati ya Bomani kuridhisha tu upinzani(wale wakina Tomaso wasioamini) lakini ukweli ni kuwa ana imani na ripoti ambayo wakina Masha tayari walishampelekea.

Nne; Rais anafahamu kuhusu mikataba yote ambayo imesainiwa na pengine ina baraka zake kwa ukamilifu wake na pia anaamini hakuna mazingira ya rushwa hata kidogo katika uingiwaji wa mikataba hiyo.

Tano; Rais hataki kabisa kuwatafuta wachawi- hivyo chini ya Rais huyu tusahau kabisa suala la kurekebisha makosa ya zamani

Sita; Rais anaridhishwa kabisa na hali ya Taifa- kisiasa, kiuchumi na kijamii; anaona mambo yote ni safi kabisa! Katika hii miaka miwili, Rais anaona tumekwenda kwa Ari, Nguvu na Kasi Mpya kwenye Tanzania yenye neema kama alivyopanga na kwamba Misingi ya Maisha bora kwa kila Mtanzania imeshajengwa. Kuanzia mwaka ujao na kuendelea ni wakati wa Ndege kupaa…..abiria fungeni mikanda.

JJ
 
Tano; Rais hataki kabisa kuwatafuta wachawi- hivyo chini ya Rais huyu tusahau kabisa suala la kurekebisha makosa ya zamani


JJ

Soma: "Tusahau kabisa suala la kuwachukulia hatua waliofanya makosa ya zamani". Kwa hiyo, watanzania wenye tuhuma kama Mkapa wataachwa tu waendelee kupumzika.

Hii si mara ya kwanza kwa Kikwete kusema haya, aliyasema haya pindi alipotoka Chimwaga baada ya kupitishwa. Nilisika live clouds FM wakati huo baada ya kufika Mikocheni, aliulizwa: Utarudisha nyumba za serikali? Katika majibu yake, msimamo huu wa kutokutafutana uchawi aliuweka bayana. Na wapiga kura walimchagua ili hali wakijua msimamo huo; kwa hiyo sitashangaa kama akisema hii ni utekelezaji wa ahadi zake na ilani ya uchaguzi ya CCM ambayo msingi wake ni kuendeleza yaleyale kwa ari, nguvu na kasi mpya

JJ
 
Tano; Rais hataki kabisa kuwatafuta wachawi- hivyo chini ya Rais huyu tusahau kabisa suala la kurekebisha makosa ya zamani


JJ

Soma: "Tusahau kabisa suala la kuwachukulia hatua waliofanya makosa ya zamani". Kwa hiyo, watanzania wenye tuhuma kama Mkapa wataachwa tu waendelee kupumzika.

Hii si mara ya kwanza kwa Kikwete kusema haya, aliyasema haya pindi alipotoka Chimwaga baada ya kupitishwa. Nilisika live clouds FM wakati huo baada ya kufika Mikocheni, aliulizwa: Utarudisha nyumba za serikali? Katika majibu yake, msimamo huu wa kutokutafutana uchawi aliuweka bayana. Na wapiga kura walimchagua ili hali wakijua msimamo huo; kwa hiyo sitashangaa kama akisema hii ni utekelezaji wa ahadi zake na ilani ya uchaguzi ya CCM ambayo msingi wake ni kuendeleza yaleyale ya Mkapa kwa ari, nguvu na kasi mpya

JJ
 
I guess the guy is even weaker than Mzee Ruksa. The bad news are: We are still to leave with these for another 8 years. Watanzania inabidi kujadili jinsi ya kumuondoa 2010 na sio yeye kurekebisha kitu.


Yeah, but we as a people are we stronger than him? Come to think of these issues now and then, I am almost close to agreeing with FMES thesis that our leaders (JK et al.) are a good reflection of ourselves. I think we need to take 50% of our population to Kenya to take some civic education lessons, maybe it could help to awaken us.
 
Yeah, but we as a people are we stronger than him? Come to think of these issues now and then, I am almost close to agreeing with FMES thesis that our leaders (JK et al.) are a good reflection of ourselves. I think we need to take 50% of our population to Kenya to take some civic education lessons, maybe it could help to awaken us.

Bado naamini bado kuna haja ya kurejesha uzalendo (Country before self)na ninakubaliana na Kitila kuhusiana na suala la uraia (civics). Watanzania tulio wengi bado hatujali, kwa kuwa cha wote si cha yoyote.
JK aliwahi kugusia kuhusu masuala ya kurejesha uzalendo katika hotuba yake kule Bungeni, but then it has just fizzled out.
 
Mnyika,

Nadhani upo sawa kwa mengi uliyosema na indeed its good analysis. Mimi pia nimekuwa na mawazo kama hayo kuwa madadiliko ya baraza na upunguzwaji wake ni vitu ambavyo vinakuja.. lini hilo ni gumu na the more we speculate the more the guy gonna make us wait...
 
JK amesema kazi ya kujenga msingi wameshaimaliza sasa tusubiri waanze kuweka matofali!!!What a JOKE! Kweli tumeliwa. Anyway 80% tulimpa wenyewe akasema BWM ameshamjegea msingi yeye ataendeleza yale aliyoyakuta bila hata kusema atafanya vipi lakini tukamuamini. Sasa leo anasema alikuwa anajenga msingi, can't believe what I 'am hearing. Hivi barabara zipi amejenga toka aanze?? Je Mwanza - Dodoma imefikia wapi???
 
Kuna maneno nimeruka kidogo hapo-nilitaka kumaanisha interview ya Rais imejikita katika kufanya PR Gimmick on ministerial issues instead of responding to lingering national questions! Nadhani ya wizara angeziachia wizara. Angejikita katika masuala machache yenye kutoa Dira na Uongozi wa Vitendo kuelekea Tanzania tunayoitaka katika miaka michache ya utawala wake iliyobaki na pengine kujenga misingi ya miaka mingi ya baadaye ya Taifa letu hata kama yeye hatakuwa Rais tena wakati huo

JJ
MNYIKA
Nimesoma comment zako kwa kina na nimeweza kuelewa jambo mmoja kubwa sana kama mwananchi wa kawaida(mkulima.
Jambo la kwanza nimejifunza kua una jenga hoja kwa HISIA zaidi kuliko uhalisia wa mambo na hisia zako zimekua more personalised kwa watu flani nitajibu hoja zako kwa kuchukua vipengele vinne ulivotamka ktk ushauri wako kwa MH RAIS.
(1) MAISHA BORA
Umejenga hoja kua maisha bora serekali imeshindwa kuwaletea watanzania nadhani hapa kuna tatizo au nyie mlioko mijini hamjaelewa alicho kisema Ahadi ya CCM kuleta maisha bora haikua jambo la usiku mmoja ni jambo endelevu na hasa ktk sekta ambazo zina gusa watu wengi,na haya maisha hayaji ukiwa kijiweni serekali inawatengenezea mazingira ni jukumu lako kutumia firsa hizo kutafuta hayo maisha bora e.g Mikopo kwa wajasiria mali wadogo wadgo serekali imepeleka 1bn kila mkoa na watu wamekopesha kuna awamu ya pili itatoka na sasa zitatumika Saccos zaidi kuliko kutumia Ma BANK,eg Wakulima tumepewa mikopo ya matreka madogo na makubwa kupitia mpango wa kuboresha sekta ya kilimo na kuna mradi mkubwa uliowekwa na serekali kutupatia pembejeo na mbolea, leo mbolea ruzuku imeongezeka na yote haya hamyaoni ww ulipo mjini baada ya kumaliza elimu ya chuo kikuu urudi kwenu (kijijini) maeneo ni mengi uendeshe kilimo cha kisasa through ur education background na pia uwasaidie wanakiji na wakulima wenzio ili watumie firsa hizo.
Leo Barabara ya Kati ina kamilika just only 100km si lami ambazo ni btn BAHI to Manyoni 40km na Manyoni to Singida 60km pia Dar to Mtwara only 170km si lami ambazo ni rufiji kilwa part kilwa Lindi,(NAJUA HAPA WENYE MAWAZO FINYU WATASEMA SI SEREKALI YA JK NATAKA NIWAKUMBUSHE SEREKALI ZINAFANYA KAZI KWA KUPOKEZANA NA PIA NI UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM.

(2)OPINION POLLS
Hapa ndg mnyika umetumia zaidi study za REDET kua wenye elimu ndogo wanaimani na Rais wakati wenye elimu kubwa wana less confidence,Nataka niseme hivi hayo ni mawazo yao na haki yao but ikumbukwe kua serekali hii ni ya watu zaidi na experience imeonyesha kua sisi wakulima ndo sehemu kubwa wenye elimu ndogo ya DARASANI lakini tuna elimu kubwa ya MTAANI kuliko nyie wa hapo mlimani,sasa nini nasema programe nyingi za awamu ya NNE ni kunipatia elimu vijijini,Zahanati,Barabara,Mbolea,Masoko ya kata na wilaya ili niuze mahindi,mpunga,uwele etc,kunipatia elimu ya bure kwa watoto na wadogo zangu,thats why tuna imani na Rais,nyie Graduets mnaotaka ajira za ofisi ukiwa kiyoyzi mnaona hajafanya kitu,pia kwenu nyie mantumia zaidi THEORIES kuliko uhalisia eg.WB watatuambia pato langu mtanzania ni dola 200 walicho hesabu is only market price vitu vilivyo letwa sokoni naonekana mtanzania ni maskini while pato langu si hivo what abt mahindi ninayo chuma shambani na kusaga na kula ugali,what abt maboga,etc vyote hivi kwa sababu haviendi sokini havionekani ktk pato langu.sasa nyie wasomi kwasababu mnatumia zaidi theories kuliko uhalisia na mnataka serekali iendeshwe kwa mawazo hayo bado mtakua hamna imani.
(3)KUVUNJWA BARAZA
Mnyika hapa umenishangaza sana na wote wenye mawazo yako unajenga hoja LOWASA aondolewe na baraza livinjwe umeshindwa kutaja mapungufu ya LOWASA na Baraza kwa ujumla toa Annalysis yako kwa kila waziri taja mapungufu ya KIUTENDAJI na si BINAFSI ili tuweze kuchangia usiseme baraza livunjwe na LOWASA aondolewe bila kujenga hoja na kutuonyesha mapungufu yao ya na kutoa njia mbadala atoke nani aingie nani na kwa sababu zipi kiutendaji,sisi TUNAONA ZAHANATI ZINA JENGWA,SHULE ZINAJENGWA,BARABARA ZINA JENGWA najua mtajenga hoja yenu kua HAMNA WAALIMU,napenda mfahamu kua huwezi kununu furniture kabla hujawa na makazi or huwezi kulima kabla hujaandaa shamba.
Ktk ushauri wako kwa Rais umedai kua serekali imeshindwa kuleta huduma bora kwa wananchi jambo ambalo napingana na ww bcs umeshindwa kuonyesha measurement yako kutaka kupima hizo huduma na ukumbuke kua ILANI ambayo imeahidi kua itatoa maisha bora kwa kila mtazania ni ya miaka 10 longterm indication za hayo maisha tunaziona sisi wakulima huku vijijini nyie mlioko Dar es saalam inakua ngumu kuona bcs wote mnataka change za over nite,ifike mahali Upinzani ufanye kazi kwa maslahi ya Watanzania kuliko mnavofanya kazi sasa mnejenga hoja nyingi kwa ubinafsi zaidi kuliko uhalisia Chama chako kupitia Slaa mmetangaza kwa watanzania Mafisadi which u cant proove.its full of FALACIES kuliko uhalisia wa jambo,JIULIZE WEWE KAMA MTANZANIA UNAFANYA NINI KUTUSAIDIA WATANZANIA SI UNAFANYA NINI KUJISAIDIA BINAFSI,napo ona issue imeongelewa na ZITO,WEWE mnanikumbusha machungu ya pale mlimani mlivokua mnatumanupulate kutuingiza ktk migogoro kumbe mna maslahi binafsi nacho waomba msiwapotoshe watanzania nilisikia kauli ya ZITO NA MBOWE walipokuja mikoani kutueleza mabo ya ufisadi na budget btn jully na august nilisikitika sana walipokua wakinadi agenda kua wamekuja kututia HASIRA WANANCHI nikakumbuka siasa za Daruso nataka niwashauri this is not Daruso politics ni issue ya Taifa.

Sipingi wajibu wenu wa kukosoa na pinga kazi mnayofanya ya kupotosha acheni serekali hii imefanya na inafanya mengi kwetu wananchi Vyombo vya habari through nyie manafanya kazi kubwa ya kupotosha uhalisia.Nahapa namkumbuka FIDEL CASTROL aliwahi kusema sababu kubwa ya kuminya vyombo vya habari kwa nchi changa kama yake ni kusaidia maendeleo bcs ukiacha freedom kubwa unasababisha vurugu kwani kila oppurtnist atatumia vyombo kujijenga.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
0713375955
NB;Administrator anatabia ya kuondoa baadhi ya koment na omba asifanye hivo kama this forum is open for every one basi huo mchezo aache.nimekoment issues 2 or 3 next day imeondolewa sidhani kama tuna jenga bali tuna bomoa.
Mnyika nimeweka namba yangu ili ikifika one day wilaya Njombe unipigie nikupeleke kwenye mashamba muone kazi inayofanywa na serekali ya awamu ya nne.
 
This is JK bwana kwake anaona kuwa serikali yake inafanya miujiza ya kutisha kwenye kujenga taifa .

kwa kweli hapa watanzania tuna kazi ya ziada kwenye kuelekea safari hii ngumu ya kujikomboa , jambo la kwanza ni kujitambua kwanza then tukajikomboe.
 
Ninapenda kuwahakikishia kwamba JK atafanya mabadiliko ya baraza lake very soon.Ila kujibu maswali kajibu kisanii na naungana na Jasusi kwamba wale alio waita ndiyo Ikulu inakubaliana naye katika kumjenga.Akisema Baraza lake liko kamili na habadilishi basi ana waangusha wale redet anbao ni kitengo chake cha kumwekea mambo sawa.Redet ni mali ya CCM na baada ya kuona bwana mkubwa anaadhirika wakaja na nayo ya kusema anakubalika na mawaziri hawakubaliki . Now akikataa hata kuchukua maoni ya Redet hapo atakuwa anawadhihirishia watanzania kwamba Urais wake una Ubia na ndiyo maana anasema tuta ikibidi .
 
MNYIKA
Nimesoma comment zako kwa kina na nimeweza kuelewa jambo mmoja kubwa sana kama mwananchi wa kawaida(mkulima.
Jambo la kwanza nimejifunza kua una jenga hoja kwa HISIA zaidi kuliko uhalisia wa mambo na hisia zako zimekua more personalised kwa watu flani nitajibu hoja zako kwa kuchukua vipengele vinne ulivotamka ktk ushauri wako kwa MH RAIS.
(1) MAISHA BORA
Umejenga hoja kua maisha bora serekali imeshindwa kuwaletea watanzania nadhani hapa kuna tatizo au nyie mlioko mijini hamjaelewa alicho kisema Ahadi ya CCM kuleta maisha bora haikua jambo la usiku mmoja ni jambo endelevu na hasa ktk sekta ambazo zina gusa watu wengi,na haya maisha hayaji ukiwa kijiweni serekali inawatengenezea mazingira ni jukumu lako kutumia firsa hizo kutafuta hayo maisha bora e.g Mikopo kwa wajasiria mali wadogo wadgo serekali imepeleka 1bn kila mkoa na watu wamekopesha kuna awamu ya pili itatoka na sasa zitatumika Saccos zaidi kuliko kutumia Ma BANK,eg Wakulima tumepewa mikopo ya matreka madogo na makubwa kupitia mpango wa kuboresha sekta ya kilimo na kuna mradi mkubwa uliowekwa na serekali kutupatia pembejeo na mbolea, leo mbolea ruzuku imeongezeka na yote haya hamyaoni ww ulipo mjini baada ya kumaliza elimu ya chuo kikuu urudi kwenu (kijijini) maeneo ni mengi uendeshe kilimo cha kisasa through ur education background na pia uwasaidie wanakiji na wakulima wenzio ili watumie firsa hizo.
Leo Barabara ya Kati ina kamilika just only 100km si lami ambazo ni btn BAHI to Manyoni 40km na Manyoni to Singida 60km pia Dar to Mtwara only 170km si lami ambazo ni rufiji kilwa part kilwa Lindi,(NAJUA HAPA WENYE MAWAZO FINYU WATASEMA SI SEREKALI YA JK NATAKA NIWAKUMBUSHE SEREKALI ZINAFANYA KAZI KWA KUPOKEZANA NA PIA NI UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM.

(2)OPINION POLLS
Hapa ndg mnyika umetumia zaidi study za REDET kua wenye elimu ndogo wanaimani na Rais wakati wenye elimu kubwa wana less confidence,Nataka niseme hivi hayo ni mawazo yao na haki yao but ikumbukwe kua serekali hii ni ya watu zaidi na experience imeonyesha kua sisi wakulima ndo sehemu kubwa wenye elimu ndogo ya DARASANI lakini tuna elimu kubwa ya MTAANI kuliko nyie wa hapo mlimani,sasa nini nasema programe nyingi za awamu ya NNE ni kunipatia elimu vijijini,Zahanati,Barabara,Mbolea,Masoko ya kata na wilaya ili niuze mahindi,mpunga,uwele etc,kunipatia elimu ya bure kwa watoto na wadogo zangu,thats why tuna imani na Rais,nyie Graduets mnaotaka ajira za ofisi ukiwa kiyoyzi mnaona hajafanya kitu,pia kwenu nyie mantumia zaidi THEORIES kuliko uhalisia eg.WB watatuambia pato langu mtanzania ni dola 200 walicho hesabu is only market price vitu vilivyo letwa sokoni naonekana mtanzania ni maskini while pato langu si hivo what abt mahindi ninayo chuma shambani na kusaga na kula ugali,what abt maboga,etc vyote hivi kwa sababu haviendi sokini havionekani ktk pato langu.sasa nyie wasomi kwasababu mnatumia zaidi theories kuliko uhalisia na mnataka serekali iendeshwe kwa mawazo hayo bado mtakua hamna imani.
(3)KUVUNJWA BARAZA
Mnyika hapa umenishangaza sana na wote wenye mawazo yako unajenga hoja LOWASA aondolewe na baraza livinjwe umeshindwa kutaja mapungufu ya LOWASA na Baraza kwa ujumla toa Annalysis yako kwa kila waziri taja mapungufu ya KIUTENDAJI na si BINAFSI ili tuweze kuchangia usiseme baraza livunjwe na LOWASA aondolewe bila kujenga hoja na kutuonyesha mapungufu yao ya na kutoa njia mbadala atoke nani aingie nani na kwa sababu zipi kiutendaji,sisi TUNAONA ZAHANATI ZINA JENGWA,SHULE ZINAJENGWA,BARABARA ZINA JENGWA najua mtajenga hoja yenu kua HAMNA WAALIMU,napenda mfahamu kua huwezi kununu furniture kabla hujawa na makazi or huwezi kulima kabla hujaandaa shamba.
Ktk ushauri wako kwa Rais umedai kua serekali imeshindwa kuleta huduma bora kwa wananchi jambo ambalo napingana na ww bcs umeshindwa kuonyesha measurement yako kutaka kupima hizo huduma na ukumbuke kua ILANI ambayo imeahidi kua itatoa maisha bora kwa kila mtazania ni ya miaka 10 longterm indication za hayo maisha tunaziona sisi wakulima huku vijijini nyie mlioko Dar es saalam inakua ngumu kuona bcs wote mnataka change za over nite,ifike mahali Upinzani ufanye kazi kwa maslahi ya Watanzania kuliko mnavofanya kazi sasa mnejenga hoja nyingi kwa ubinafsi zaidi kuliko uhalisia Chama chako kupitia Slaa mmetangaza kwa watanzania Mafisadi which u cant proove.its full of FALACIES kuliko uhalisia wa jambo,JIULIZE WEWE KAMA MTANZANIA UNAFANYA NINI KUTUSAIDIA WATANZANIA SI UNAFANYA NINI KUJISAIDIA BINAFSI,napo ona issue imeongelewa na ZITO,WEWE mnanikumbusha machungu ya pale mlimani mlivokua mnatumanupulate kutuingiza ktk migogoro kumbe mna maslahi binafsi nacho waomba msiwapotoshe watanzania nilisikia kauli ya ZITO NA MBOWE walipokuja mikoani kutueleza mabo ya ufisadi na budget btn jully na august nilisikitika sana walipokua wakinadi agenda kua wamekuja kututia HASIRA WANANCHI nikakumbuka siasa za Daruso nataka niwashauri this is not Daruso politics ni issue ya Taifa.

Sipingi wajibu wenu wa kukosoa na pinga kazi mnayofanya ya kupotosha acheni serekali hii imefanya na inafanya mengi kwetu wananchi Vyombo vya habari through nyie manafanya kazi kubwa ya kupotosha uhalisia.Nahapa namkumbuka FIDEL CASTROL aliwahi kusema sababu kubwa ya kuminya vyombo vya habari kwa nchi changa kama yake ni kusaidia maendeleo bcs ukiacha freedom kubwa unasababisha vurugu kwani kila oppurtnist atatumia vyombo kujijenga.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
0713375955
NB;Administrator anatabia ya kuondoa baadhi ya koment na omba asifanye hivo kama this forum is open for every one basi huo mchezo aache.nimekoment issues 2 or 3 next day imeondolewa sidhani kama tuna jenga bali tuna bomoa.
Mnyika nimeweka namba yangu ili ikifika one day wilaya Njombe unipigie nikupeleke kwenye mashamba muone kazi inayofanywa na serekali ya awamu ya nne.


1. Kuhusu Opinion Polls

Kama unataka kujua maoni yangu kuhusu hizo Poll za REDET tazama TVT leo, lakini kwa ujumla mimi nakubaliana nazo kwa kiasi tu! Ila, nimejenga hoja zangu kwa kutumia ripoti yao kwa kuwa Rais Kikwete, serikali yake na CCM wote wameyakubali matokeo ya maoni hayo kuwa yanawasilisha HALI HALISI(soma uhalisia) na sauti ya wananchi. Kama hivyo ndivyo, katika muktadha huo basi niliyoyasema si HISIA zangu, ndio HALI HALISI. Labda kama umeamua kupingana na msimamo wa CCM chama chako ulichosema kidumu

2. Kuhusu Maisha Bora kwa kila Mtanzania

Si maoni yangu kwamba imani juu ya Kikwete imepungua kutokana na kushindwa kuleta maisha bora. Ni sauti ya wananchi katika kura hizo za maoni. Hivyo hayo maelezo unayoyatoa kuhusu SACCOS, mabilioni ya JK, ruzuku kwa wakulima nk inayonyesha vitu hivyo havijawafikia watanzania walio wengi. Unaweza kutueleza ni watanzania wangapi wamefikiwa na hayo? Kuhusu barabara naona umejitilia shaka mwenyewe. Ukitaka kujua hali ya umasikini ilivyo na jinsi ambayo bado suala la maisha bora ni ndoto tazama ripoti ya MKUKUTA ya mwaka huu ambayo ilitolewa kama nyaraka ya awali katika wiki ya umasikini nchini. Niliwahi kuandika siku chache baada ya Kikwete kuingia ikulu kwamba watanzania wamelishwa matumaini hewa kwa ahadi lukuki na nikasema kwamba Serikali ya Kikwete ijitahidi ku-manage public expectation badala ya kuongeza tena ahadi lukuki, laiti kama huu ungekuwa ni msingi wa kazi wa mwaka mzima wa kwanza wa Kikwete- wananchi(labda) wangekuwa wanaielewa lugha yako hiyo. Watanzania wanampima Kikwete kwa maneno na ahadi zake, wanalinganisha na vitendo! Huwezi kusema unaboresha maisha halafu unaongeza gharama za maisha kwa bajeti wakati vipato viko pale pale. Huwezi kusema wananchi wafunge mkanda halafu kuna mjadala wa viongozi kuongeza matobo ya mikanda kwa ufisadi na matumizi ya anasa. Nakubaliana na wewe kwamba maoni ya watanzania wa kawaida ni tofauti kidogo na ya wasomi, ndio maana wakati wasomi wengi wanaguswa na masuala ya rushwa na ufisadi, wananchi wa kawaida shida yao kuu ni huduma za kijamii. Je, Dira na vitendo vya serikali vinakabiliana na hali hizo kwa ukamilifu? Ripoti ya MKUKUTA na Hata kura za maoni za REDET zinaonyesha bado safari ni ndefu.

3. Kuvunjwa kwa Baraza

Mosi, ndio nasikia toka kwako kuwa Ilani ya CCM ni ya miaka 10? Nijuavyo ni miaka mitano na sasa tuko miwili- karibu ya nusu, kipande kilichofanywa na kipande kilichobaki, Je-kinakuthibitishia kwamba yote yatatekelezwa ifikapo 2010? Kama sio, kwanini miaka miwili iliyopita serikali ya CCM imeshindwa kwenda kwa Ari, Nguvu na Kasi mpya kama ilivyoimba? Je, mawaziri waliopo wameweza kuongoza hizo mbio? Kura za maoni zinaonyesha wakati JK wanaoridhika na utendaji wake ni 44% ni asilimia 56% ndio wana imani naye kama kiongozi.(Mimi naamini ni chini kidogo ya hapo, ndio maana nimetoa mwito taasisi nyingine nazo ziendeshe kura ya maoni) lakini ni takribani asilimia 20 tu wanaridhika na baraza lililopo, na kumbuka hapa ni baada ya JK kufanya mabadiliko huko nyuma. Kinara wa Mawaziri hao ni Waziri Mkuu. Na Lowassa kuzidiwa umaarufu(wa imani) na Zitto Kabwe, hapa inabidi kutafuta waziri mkuu mwingine. Sasa usichanganye mambo haya na masuala ya DARUSO, najua unafahamu kabisa kuwa sijawahi kujihusisha na siasa za DARUSO, sijawahi kuwa kiongozi wa DARUSO. Lakini kubwa zaidi ni kuwa Lowasa amekuwa akikabiliwa na tuhuma kadhaa na amekuwa kinara wa kuzuia kashfa hizo zisijadiliwe bungeni- Kamati ya Bunge sasa inachunguza kuhusu Richmond, lakini kwa matokeo yoyote yatakayokuja hayawezi kuacha kuondoa ukweli kuwa aliingilia mchakato wa Zabuni iliyopelekea kupata Richmond iliyopelekea kukosa umeme wa dharura iliyopelekea uchumi kuathirika kwa namna mbalimbali wakati wa uhaba wa umeme. Kwa matumizi haya mabaya tu ya madaraka hata kama ikionekana hakuna Rushwa bado anastahili kuwajibika! Karamagi na suala la Buzwagi limeshushia hadhi katika jamii, Kikwete kuongozana na Waziri wa namna hiyo katika miaka inayofuata ni kuathiri taswira ya Taasisi ya Urais. Binafsi sijawahi kukutana na Lowassa wala Karamagi, hivyo sina suala lolote personal nao- lakini kwa manufaa ya Rais wetu na Taifa letu wanapaswa wapumzishwe pamoja na wenzao wengine kadhaa. Kwani Taifa letu limeishiwa na viongozi mpaka tuendelee kuwang’ang’ania? Hii nimetoa ni mifano michache tu, najua wengine wataendeleza hapa.

Nashukuru, nami ukija DSM nitafute kupitia 0754694553.

JJ

BTW: Uko Njombe, unaweza kunieleza ni kwanini katika kura za maoni za REDET watu wa wilaya ya Mbarali wanaoridhika na Kikwete wamekuwa asilimia 0%(sifuri) pamoja na hizo jitihada za Kilimo ulizotaja? Au ni kwa sababu ya kuwahamisha wananchi kule Ihefu?
 
1. Kuhusu Opinion Polls

Kama unataka kujua maoni yangu kuhusu hizo Poll za REDET tazama TVT leo, lakini kwa ujumla mimi nakubaliana nazo kwa kiasi tu! Ila, nimejenga hoja zangu kwa kutumia ripoti yao kwa kuwa Rais Kikwete, serikali yake na CCM wote wameyakubali matokeo ya maoni hayo kuwa yanawasilisha HALI HALISI(soma uhalisia) na sauti ya wananchi. Kama hivyo ndivyo, katika muktadha huo basi niliyoyasema si HISIA zangu, ndio HALI HALISI. Labda kama umeamua kupingana na msimamo wa CCM chama chako ulichosema kidumu

2. Kuhusu Maisha Bora kwa kila Mtanzania

Si maoni yangu kwamba imani juu ya Kikwete imepungua kutokana na kushindwa kuleta maisha bora. Ni sauti ya wananchi katika kura hizo za maoni. Hivyo hayo maelezo unayoyatoa kuhusu SACCOS, mabilioni ya JK, ruzuku kwa wakulima nk inayonyesha vitu hivyo havijawafikia watanzania walio wengi. Unaweza kutueleza ni watanzania wangapi wamefikiwa na hayo? Kuhusu barabara naona umejitilia shaka mwenyewe. Ukitaka kujua hali ya umasikini ilivyo na jinsi ambayo bado suala la maisha bora ni ndoto tazama ripoti ya MKUKUTA ya mwaka huu ambayo ilitolewa kama nyaraka ya awali katika wiki ya umasikini nchini. Niliwahi kuandika siku chache baada ya Kikwete kuingia ikulu kwamba watanzania wamelishwa matumaini hewa kwa ahadi lukuki na nikasema kwamba Serikali ya Kikwete ijitahidi ku-manage public expectation badala ya kuongeza tena ahadi lukuki, laiti kama huu ungekuwa ni msingi wa kazi wa mwaka mzima wa kwanza wa Kikwete- wananchi(labda) wangekuwa wanaielewa lugha yako hiyo. Watanzania wanampima Kikwete kwa maneno na ahadi zake, wanalinganisha na vitendo! Huwezi kusema unaboresha maisha halafu unaongeza gharama za maisha kwa bajeti wakati vipato viko pale pale. Huwezi kusema wananchi wafunge mkanda halafu kuna mjadala wa viongozi kuongeza matobo ya mikanda kwa ufisadi na matumizi ya anasa. Nakubaliana na wewe kwamba maoni ya watanzania wa kawaida ni tofauti kidogo na ya wasomi, ndio maana wakati wasomi wengi wanaguswa na masuala ya rushwa na ufisadi, wananchi wa kawaida shida yao kuu ni huduma za kijamii. Je, Dira na vitendo vya serikali vinakabiliana na hali hizo kwa ukamilifu? Ripoti ya MKUKUTA na Hata kura za maoni za REDET zinaonyesha bado safari ni ndefu.

3. Kuvunjwa kwa Baraza

Mosi, ndio nasikia toka kwako kuwa Ilani ya CCM ni ya miaka 10? Nijuavyo ni miaka mitano na sasa tuko miwili- karibu ya nusu, kipande kilichofanywa na kipande kilichobaki, Je-kinakuthibitishia kwamba yote yatatekelezwa ifikapo 2010? Kama sio, kwanini miaka miwili iliyopita serikali ya CCM imeshindwa kwenda kwa Ari, Nguvu na Kasi mpya kama ilivyoimba? Je, mawaziri waliopo wameweza kuongoza hizo mbio? Kura za maoni zinaonyesha wakati JK wanaoridhika na utendaji wake ni 44% ni asilimia 56% ndio wana imani naye kama kiongozi.(Mimi naamini ni chini kidogo ya hapo, ndio maana nimetoa mwito taasisi nyingine nazo ziendeshe kura ya maoni) lakini ni takribani asilimia 20 tu wanaridhika na baraza lililopo, na kumbuka hapa ni baada ya JK kufanya mabadiliko huko nyuma. Kinara wa Mawaziri hao ni Waziri Mkuu. Na Lowassa kuzidiwa umaarufu(wa imani) na Zitto Kabwe, hapa inabidi kutafuta waziri mkuu mwingine. Sasa usichanganye mambo haya na masuala ya DARUSO, najua unafahamu kabisa kuwa sijawahi kujihusisha na siasa za DARUSO, sijawahi kuwa kiongozi wa DARUSO. Lakini kubwa zaidi ni kuwa Lowasa amekuwa akikabiliwa na tuhuma kadhaa na amekuwa kinara wa kuzuia kashfa hizo zisijadiliwe bungeni- Kamati ya Bunge sasa inachunguza kuhusu Richmond, lakini kwa matokeo yoyote yatakayokuja hayawezi kuacha kuondoa ukweli kuwa aliingilia mchakato wa Zabuni iliyopelekea kupata Richmond iliyopelekea kukosa umeme wa dharura iliyopelekea uchumi kuathirika kwa namna mbalimbali wakati wa uhaba wa umeme. Kwa matumizi haya mabaya tu ya madaraka hata kama ikionekana hakuna Rushwa bado anastahili kuwajibika! Karamagi na suala la Buzwagi limeshushia hadhi katika jamii, Kikwete kuongozana na Waziri wa namna hiyo katika miaka inayofuata ni kuathiri taswira ya Taasisi ya Urais. Binafsi sijawahi kukutana na Lowassa wala Karamagi, hivyo sina suala lolote personal nao- lakini kwa manufaa ya Rais wetu na Taifa letu wanapaswa wapumzishwe pamoja na wenzao wengine kadhaa. Kwani Taifa letu limeishiwa na viongozi mpaka tuendelee kuwang’ang’ania? Hii nimetoa ni mifano michache tu, najua wengine wataendeleza hapa.

Nashukuru, nami ukija DSM nitafute kupitia 0754694553.

JJ

BTW: Uko Njombe, unaweza kunieleza ni kwanini katika kura za maoni za REDET watu wa wilaya ya Mbarali wanaoridhika na Kikwete wamekuwa asilimia 0%(sifuri) pamoja na hizo jitihada za Kilimo ulizotaja? Au ni kwa sababu ya kuwahamisha wananchi kule Ihefu?
MNYIKA

Comment zangu ni ndogo to hapa

(1)Si lazima nikubaliane na Report ya Redet eti kwa sababu RAIS amesema ni nzuri au ccm wameikubali i have my opinion na mtazamo wangu ktk hilo bcs hatujui wanatumia sampling techniques zipi wala hatujui walitumia sample space ya kiasi gani ili iwe true representation ya watanzania.
(2) About Ilani jua kwamba Serekali yetu ni mpaka 2010 other things remain constant, that why nasema ilani yetu ni DIRA yetu kwa miaka mitano then 10,abt kipindi kilichobaki kua 2010 yote yatakua yametekelezwa hiyo no DOUBT bcs indication inaonekana.
(3)Abt budget nilitegemea ungelikua ni mmoja watakao tupongeza kwa kupunguza utegemezi by increasing internal revenue though inawezekana machungu ni makubwa kwetu but mutiplier effect yake in long run hasa upande wa utegemezi ni kubwa.

(4)Abt PM na ZITTO kama kigezo ni umaarufu i dont have tatizo na hilo bcs redet hawajasema walipima umaarufu wa kitu gani(imani)ktk lipi bcs that item its wide kwahiyo hilo nalo sitalisemea na kama sample iliyochukuliwa nayo inaweza kuathiri matokeo ya research.

Mwisho niliwahi kumsikia Katibu mkuu wa chadema ikihojiwa ktk Kituo cha redio one alitakiwa kutamka kama kuna jema ambalo serekali imefanya alikataa ana kusema hawezi kutamka atakua anaharibu mantiki nzima ya upinzani. Kwahiyo nachojaribu kusema hapa ni kua CCM na serekali yake imetuonyesha na imedhamiria kutekeleza ilani ya uchaguzi na yapo yaliyofanyika mengi.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
 
MNYIKA

Comment zangu ni ndogo to hapa

(1)Si lazima nikubaliane na Report ya Redet eti kwa sababu RAIS amesema ni nzuri au ccm wameikubali i have my opinion na mtazamo wangu ktk hilo bcs hatujui wanatumia sampling techniques zipi wala hatujui walitumia sample space ya kiasi gani ili iwe true representation ya watanzania.
(2) About Ilani jua kwamba Serekali yetu ni mpaka 2010 other things remain constant, that why nasema ilani yetu ni DIRA yetu kwa miaka mitano then 10,abt kipindi kilichobaki kua 2010 yote yatakua yametekelezwa hiyo no DOUBT bcs indication inaonekana.
(3)Abt budget nilitegemea ungelikua ni mmoja watakao tupongeza kwa kupunguza utegemezi by increasing internal revenue though inawezekana machungu ni makubwa kwetu but mutiplier effect yake in long run hasa upande wa utegemezi ni kubwa.

(4)Abt PM na ZITTO kama kigezo ni umaarufu i dont have tatizo na hilo bcs redet hawajasema walipima umaarufu wa kitu gani(imani)ktk lipi bcs that item its wide kwahiyo hilo nalo sitalisemea na kama sample iliyochukuliwa nayo inaweza kuathiri matokeo ya research.

Mwisho niliwahi kumsikia Katibu mkuu wa chadema ikihojiwa ktk Kituo cha redio one alitakiwa kutamka kama kuna jema ambalo serekali imefanya alikataa ana kusema hawezi kutamka atakua anaharibu mantiki nzima ya upinzani. Kwahiyo nachojaribu kusema hapa ni kua CCM na serekali yake imetuonyesha na imedhamiria kutekeleza ilani ya uchaguzi na yapo yaliyofanyika mengi.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI


Kaka

Nashauri ukasome kwanza ripoti ya REDET ndio tutaweza kujadiliana vizuri zaidi.

1. Ripoti imeeleza methodolojia waliyotumia na idadi ya watu waliohusika na mchakato gani wamepitia kupata sampuli nasibu.

2. Miaka miwili imepita kati ya mitano(ndio maisha ya Ilani ya CCM sio miaka 10) hebu niambie ni yapi yametekelezwa kiasi cha kutia moyo kwamba ilani nzima itakuwa imetimizwa ifikapo 2010?

3. Siwezi kupongeza kupunguza utegemezi wa serikali kwa kuwakamua wananchi kupitia ongezeko la kodi huku wawekezaji wakubwa wakipewa msamaha wa kodi, vyanzo mbadala vya mapato vikipuuzwa na fedha nyingi zikipotea katika ufisadi na matumizi ya anasa ya serikali. Wapinzani tuliwaeleza katika bajeti mbadala jinsi ya kupunguza utegemezi kuliko hata ilivyo sasa bila kuwaumiza wananchi kwa kupandisha gharama za maisha. Wabunge wa CCM kwa uwingi wao, wakapuuza. Sikushangaa kwamba kura za maoni inaonyesha imani kwa wabunge nayo imeshuka sana.

4. Kuhusu Zitto; Swali lilikuwa ni kiongozi gani unamuamini zaidi? Hii ni zaidi ya umashuhuri. Lowassa akazidiwa na Zitto. Sasa kama watanzania wana imani na Zitto kuliko Lowassa; waziri mkuu huyu anaendeleaje kuwa kiongozi wa shughuli za serikali bungeni? Kama yeye ndio mzungukaji mikoani kuhamasisha maendeleo na watu hawamuamini unategemea nini? Kama mfuatuliaji wa maagizo ya Rais haaminifiki Kikwete ategemee nini? Hakuna jinsi zaidi ya ndugu Lowassa kupumzika na wenzake wakina Karamagi na Kingunge Ngombare Mwiru.

Nieleze basi hayo unayoona wewe ni mafanikio ya serikali yanayohitaji kupigiwa upatu na kila mtanzania kila mahali.

KIGUMU CHAMA CHA MAPINDUZI!, SWALI YA KUJIULIZA, NI MAPINDUZI YA KUPINDUA NINI? LABDA KAMA NI KIGUMU KUKUBALI MABADILIKO

JJ
 
Hi Mtoto wa mkulima!

Mimi nna mchango kidogo kuhusu hoja zako. Kwanza kabisa naomba ufahamu maana ya neno performance naanza na hili kwa sababu inaonyesha wewe unaridhika kabisa na perfomance/utendaji wa serikali ya awamu ya nne.

Perfomance kwa kifupi kabisa ni kwamba chini ya asilimia 100% ni non perfomer, asilimia 100% ni compliance (huhitaji hata kusifiwa kwa hilo maana umefanya ulichotarajiwa kufanya), zaidi ya asilimia 100% hapo ndio unakuwa unaanza kuperform.

Je unazikumbuka vizuri ahadi za JK 2005? alitaja barabara nyingi tu kwamba zitajengwa kwa kiwango cha lami na nyingi zilikuwa mpya kabisa tofauti na zile za mkapa je ni ngapi zimekamilika???? Hizo kilomita anazotaja mbona hataji ni barabara zipi?

Mbona hasemi amejenga uwanja wa kisasa pale neshno stadium maana nao haujakamilika, na kazi imeendelea na inaendelea ndani ya awamu yake?

Wewe unazungumzia njombe, hivi umewahi kufika shinyanga vijini, nkasi, lindi vijijini na kwingineko au huko si Tanzania?

Hizo shule ambazo ansema wamejenga anaweza kupeleka toto wake akasome au wa EL katika shule kata iliyoko say Mpanda vijini?

Kwa kuhitimisha mimi kwa nnavyoifahamu REDET na mwenendo wake toka JK anwania uRAHISI walionekana wazi kujikomba kwa huyu mkuu an wameendelea kufanya hivyo, hivyo basi kuna uwezekano mkubwa kabisa kwamba takwimu halisi ni mbaya zaidi hata ya zilizotolewa.

Nahitimisha kwa kusema serikali hii ni non performers na wao wanalijua hilo nakushangaa sana wewe unayesifu mambo ambayo hata unaowasifia hawayaamini.

Jioni njema
 
...mwenyewe unajiona insider kumbe mpiga ngoma tuu,they dont even know you

Huwezi kujua,pengine ni mjumbe wa CCM wa kujitegemea.Kwani bila ya kuwepo wao mambo yangu mengi yasingekamilika hivyo napaswa kuwatetea ,kuwaunga mkono ,kuwapongeza na kutilia nguvu msimamo wa kutotetereka kwa makelele ya washangiliaji , sometimes mechi zinakuwa na mashabiki ambao hatujapata kuwaona wanazuka na kuzua kila kona ,kama mjumbe wa kujitegemea nina husika moja kwa moja kutetea maslahi ya Chama na kuhakikisha Interest za chama na zinabaki na hazipo hatarini kwetu.
 
Wewe kweli ni Mtoto wa Mkulima ama mojawapo wa mitoto wa wale Mafisadi 10 unatuchora hapa ? Mbona una hoja tenge ?Mtoto wa Mkulima ni kama mimi hapa bwana nalonga bila kuegemea maana najitegemea mimi hata faida ya CCM siijui.
 
Yeah, but we as a people are we stronger than him? Come to think of these issues now and then, I am almost close to agreeing with FMES thesis that our leaders (JK et al.) are a good reflection of ourselves. I think we need to take 50% of our population to Kenya to take some civic education lessons, maybe it could help to awaken us.

Mr someone not almost to agreeing but huo ndio ukweli.
Ukirejea ktk vitabu vitakatifu kwangu ngoja tuchukulie Biblia samani kwa wale nitakaowakwaza ni kuwa -
Kiongozi yeyote anawekwa na Mungu na kwa misingi kwamba ndiye mwafaka kwa watu wale
yani ni kwamba ukimshutumu kiongonzi ni kilaza that implies wanaoongozwa wengi wao ni vilaza.

kwa kutia msisitizo ktk hilo bible says usitupe lulu zako ktk nguruwe maana watazikanyaga na kugeuka wakufutilie mbali

Kiongozi mwenye hekima hawezi kuongoza GOZIGOZi ama kiongozi GOZIGOZI hawezi kuongoza wenye Hekima

Hivyo kila kiongozi ni mwafaka kwa watu muafaka.

Ukitaka kupata kiongozi mwenye HEKIMA vivyo hivyo lazima watawaliwa wawe wenye Hekima
OTHERWISE
BOILING UNEMPTY POT EXPECTING SOUP
 
Mr someone not almost to agreeing but huo ndio ukweli.
Ukirejea ktk vitabu vitakatifu kwangu ngoja tuchukulie Biblia samani kwa wale nitakaowakwaza ni kuwa -
Kiongozi yeyote anawekwa na Mungu na kwa misingi kwamba ndiye mwafaka kwa watu wale
yani ni kwamba ukimshutumu kiongonzi ni kilaza that implies wanaoongozwa wengi wao ni vilaza.

kwa kutia msisitizo ktk hilo bible says usitupe lulu zako ktk nguruwe maana watazikanyaga na kugeuka wakufutilie mbali

Kiongozi mwenye hekima hawezi kuongoza GOZIGOZi ama kiongozi GOZIGOZI hawezi kuongoza wenye Hekima

Hivyo kila kiongozi ni mwafaka kwa watu muafaka.

Ukitaka kupata kiongozi mwenye HEKIMA vivyo hivyo lazima watawaliwa wawe wenye Hekima
OTHERWISE
BOILING UNEMPTY POT EXPECTING SOUP


Makamap,
Tatizo ni kwamba wengine wameingia kwa nguvu za vibuyu!! kwahiyo hayao maandiko matakatifu is not applicable
soma hapa!
http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=8263
 
Back
Top Bottom