JK kufanya mabadiliko

Mkuu jiulize,
Kwa nini JK achukiwe why? kwa nini? Kuna watu wana ajira zinazolingana na uwezo/elimu yao na wengine wanafanya kazi kwa ufanisi sana, sio wezi na si wafuasi wa mtandao wa mafisadi na wanamchukia JK why? kwa nini?
Mkuu Said jiulize na tuambie hapa!!

...sasa hivi wanamkakati wa kikwete wanakuja na hoja dhaifu kuwa kikwete hajashindwa ila wasaidizi wake ndio wanamuangusha....kama mnavyojuwa kikwete amekuwa mwepesi sana kupokea sifa hata pale "TAIFA stars inaposhinda 1-0"....hapo hapo kutaka kujiweka kando na ,mambo yote mabaya yanayofanyika.....simply yeye aonekane mzuri ..wabaya waonekane wengine..."

watanzania tunaweza kuamua moja HILI SUALA LA EPA NA MENGINE ..hata kama yangekuwa hayapo...je still jk analo lipi alilolifikia kimaendeleo ndani ya hii miaka 3....zaidi ya kila wakati kuleta mazingaombwe ya kuteka akili za watu???

natoa changamoto kwa wahariri wa magazeti waanze kumuhumu kikwete kwa ahadi zake..zinazobebwa ba kauli mbiu za "KASI MPYA,NGUVU MPYA NA ARI MPYA"..," MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA "..,: " TANZANIA YENYE NEEMA INAWEZEKANA'"....hizi ni kauli mbinu ambazo ghafla zimekuwa mwiba ..na kuzitamka mbele ya kikwete sembuse yeye mwenyewe kuzitamka ..imejeuka kama uhaini..au kumkebehi..mkuu...

sasa turudi kwenye ilani ya uchaguzi.....ambayo aliisoma na kuielewa kabla ya kugombea ..aliiamini kuwa anao uwezo wa kuitekeleza...tulipohoji alipofikisha mwaka mmoja ikulu..watu walimrushia taulo jeupe wakisema tunamuonea tumpe muda....wakasahau nyota njema huonekana asubuhi...........sasa tuanze kuangalia ameshatekeleza ahadi ngapi na kwa asilimia ngapi..akiwa tayari ana miaka mitatu ikulu????.......hasa ukizingatia kama yeye mwenyewe anavyosema ..kuwa he was president in waiting for ten years.....
 
Fanya mabadiliko hata kila siku, kinachoangaliwa ni tija iliyopatikana baada ya kufanya mabadiliko hayo.
 
"sasa turudi kwenye ilani ya uchaguzi....ambayo aliisoma na kuielewa kabla ya kugombea"

Hii mbona alishaikana siku nyingi.... alishasema yeye hakuhusika katika kuiandaa wala kuweka ajenda.... kwa kifupi kainawa kitambo!
 
Imetolewa mara ya mwisho: 22.11.2008 0010 EAT

Hata katika ziara za Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Bw. Edward Lowassa, matukio ya wakuu hao wengi kuonekana wanafanyakazi kwa kukurupuaka yalionekana huku malalamiko ya wananchi katika vyombo vya habari wakati fulani yakiwahusisha wakuu hao katika tuhuma kama vile kukumbatia wawekezaji wanaonyanyasa wananchi, kushindwa kwao kuwasikiliza wananchi na kutatua shida zao na wengi pia kukosa mbinu madhubuti za kiutawala.

Wakuu hawa wa wilaya wanafanya kama anachofanya yeye mwenyewe JK. Wanawakumbatia matajiri....kama yeye alivyo na anavyoendelea kuwakumbatia..........Hayo mabadiliko sijui yataleta nini kipya.
 
"sasa turudi kwenye ilani ya uchaguzi....ambayo aliisoma na kuielewa kabla ya kugombea"

Hii mbona alishaikana siku nyingi.... alishasema yeye hakuhusika katika kuiandaa wala kuweka ajenda.... kwa kifupi kainawa kitambo!


..atakuwa kiongozi wa kwanza kuikana ilani iliyomuweka madarakani ....maana chama chochote duniani kabla ya uchaguzin huandaa ilani ambayo hutumia kwenye uteuzi kwa kutafuta miongoni mwa wanachama wake wenye uwezo wa kuitekeleza huisoma na kuamua kugombea au la....

sasa akikataa ilani atataka tumpime kwa kipimio kipi.............
 
mmmhh kweli nam-miss sana Mkuu FM ES


...jamani huyu mkulu ni mdau muhimu sana hapa forum...what is the problem..

..kamanda sisi wapiganaji tunakuangalia wewe..ukirudi nyuma tutaishiwa morali.....tafadhali kamata ramani ,chapa mguu tusonge mbele!.....yote haya ni kwa faida ya watoto na wajukuu zetu ndani ya mama yetu TANZANIA.

,..popote ulipo pokea salamu zangu!
 
Kwa maoni yangu naona suala si kufanya mabadiliko ya wakuu wa wilaya ama wakuu wa mikoa ama mawaziri, suala kubwa ni yeye mwenyewe JK. Yeye kama mkuu wa nchi akiwa makini katika kazi zake akaacha kuchanganya urafiki, ushikaji na kujuana katika kazi kila kitu kitakuwa makini. Lakini kwa sasa kila mkuu wa wilaya ama mkuu wa mkoa ama waziri ama balozi ni rafiki ya JK, kuna kitu cha maana kweli kitafanyika hapa?

Uteuzi ama uchaguzi wa viongozi katika kipindi hiki haufuati maadili ila umeegemea urafiki na ushikaji na wala haufuati uwezo na uwajibikaji wa mtu.
 

..atakuwa kiongozi wa kwanza kuikana ilani iliyomuweka madarakani ....maana chama chochote duniani kabla ya uchaguzin huandaa ilani ambayo hutumia kwenye uteuzi kwa kutafuta miongoni mwa wanachama wake wenye uwezo wa kuitekeleza huisoma na kuamua kugombea au la....

sasa akikataa ilani atataka tumpime kwa kipimio kipi.............
Hata Mkapa aliikana ilani yake akisema kuwa haitekelezeki.
Naona ni tabi ya CCM hiyo. Kila mtu akiingia mamlakani anafanya vyakevyake kwa sababu ilani yao haitekelezeki.
 

...sasa hivi wanamkakati wa kikwete wanakuja na hoja dhaifu kuwa kikwete hajashindwa ila wasaidizi wake ndio wanamuangusha....kama mnavyojuwa kikwete amekuwa mwepesi sana kupokea sifa hata pale "TAIFA stars inaposhinda 1-0"....hapo hapo kutaka kujiweka kando na ,mambo yote mabaya yanayofanyika.....simply yeye aonekane mzuri ..wabaya waonekane wengine..."

watanzania tunaweza kuamua moja HILI SUALA LA EPA NA MENGINE ..hata kama yangekuwa hayapo...je still jk analo lipi alilolifikia kimaendeleo ndani ya hii miaka 3....zaidi ya kila wakati kuleta mazingaombwe ya kuteka akili za watu???

natoa changamoto kwa wahariri wa magazeti waanze kumuhumu kikwete kwa ahadi zake..zinazobebwa ba kauli mbiu za "KASI MPYA,NGUVU MPYA NA ARI MPYA"..," MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA "..,: " TANZANIA YENYE NEEMA INAWEZEKANA'"....hizi ni kauli mbinu ambazo ghafla zimekuwa mwiba ..na kuzitamka mbele ya kikwete sembuse yeye mwenyewe kuzitamka ..imejeuka kama uhaini..au kumkebehi..mkuu...

sasa turudi kwenye ilani ya uchaguzi.....ambayo aliisoma na kuielewa kabla ya kugombea ..aliiamini kuwa anao uwezo wa kuitekeleza...tulipohoji alipofikisha mwaka mmoja ikulu..watu walimrushia taulo jeupe wakisema tunamuonea tumpe muda....wakasahau nyota njema huonekana asubuhi...........sasa tuanze kuangalia ameshatekeleza ahadi ngapi na kwa asilimia ngapi..akiwa tayari ana miaka mitatu ikulu????.......hasa ukizingatia kama yeye mwenyewe anavyosema ..kuwa he was president in waiting for ten years.....

Yapo ya ILANI anayotaka kuyatekeleza lkn wengine HAWATAKI...na WANAMTISHIA KUWA NCHI HAITAKALIKA!!!!
 
kwa hili la wakuu wa wilaya jamani wacheni afanye mabadiliko,huko wilayani kusema za ukweli kumeoza,wilaya nyingi zimeshikiliwa na kina mama,wachache wao wanajitahidi angalau angalau lakini wilaya zilizo nyingi zina watendaji dhaifu sana. singependa kuzitaja lakini wanachi wa wilaya hizo ndio mashaidi wa jinsi wilaya zao zinavyoendeshwa i.e korogwe,lushoto ,hai wapate watu wa shemu hizo utapata muziki wake.

kwa hapo JK nakupongeza!
 
Kwa suala la wakuu wa wilaya nafikiri mtu wa kwanza kulaumiwa atakuwa ni rais mwenyewe kwani wengi kati yao aliwachagua kwa kigezo cha kufahamiana/urafiki zaidi bila kuangalia uwezo wa mtu katika utendaji wa kazi. Nafikiri wilayani ni sehemu muhimu sana kwani huko ndiko kiongozi anafanyakazi na raia wa kawaida kabisa na huko ndiko matatizo yote ya kijamii yalikojikita zaidi.
 
Hata barazani mwake anapaswa kuwaacha waliodhihirika kuwa ni mzigo kwake na awape fursa wataalamu wenye kuthubutu ktk utendaji, awe tayari kupokea mawazo tofauti toka kwa hao wanaomsaidia kazi vinginevyo ni kuruhusu wasaidizi incompetent kila kukicha wanachojua ni kujipendekeza na kupikiana majungu kwa rais ili kukomoana wakati mambo hayaendi.

Jk ana watu wengi safi kitaaluma na kiutendaji lakini amewaacha wakinangwa wa wale anaowaamini yeye kuwa ni watu bora kumbe vilaza na si wakweli kwake.

All in all anastahili kuwapumzisha wakuu wengi wa wilaya, mikoa, maktibu wakuu, na mawaziri kadhaa, imetosha muungwana,sisi tumeona na wewe unaona kwa dhati, tupangie safu ya wachapa kazi wa kweli, usihofu kuitwa mdini, mkabila au la..........

Twende kazini mkuu
 
kwa hili la wakuu wa wilaya jamani wacheni afanye mabadiliko,huko wilayani kusema za ukweli kumeoza,wilaya nyingi zimeshikiliwa na kina mama,wachache wao wanajitahidi angalau angalau lakini wilaya zilizo nyingi zina watendaji dhaifu sana. Singependa kuzitaja lakini wanachi wa wilaya hizo ndio mashaidi wa jinsi wilaya zao zinavyoendeshwa i.e korogwe,lushoto ,hai wapate watu wa shemu hizo utapata muziki wake.

Kwa hapo jk nakupongeza!

tena akinmama hao hawajaacha umbea wa mitaani
 
Tatizo lenu mnataka kumungunya maneno.

Kuweni wakweli, JK hafai kuongoza nchi, aende akaongoze familia yake.

Vile vile mnaniudhi mnapotumia initials za JK mkimaanisha Jakaya Kikwete. Hizi initials ni Julius Kambarage (mtu ambaye kama angelikuwapo leo angeshakemea na kusikilizwa kuhusu urafiki wa Kikwete na Mafisadi).

Nashauri huyu bwana mkubwa tumuite JMK (Jakaya Mrisho Kikwete) ili tumtofautishe na Marehemu Baba wa Taifa kwa jina na kwa matendo yake.
 
Asilimia kubwa ya watendaji wa serikali inayoongozwa na JK ni watu wa karibu nae kwa maana ya marafiki wa kuanzia vyuoni, jeshini, TANU na hata wale wenye ukaribu na mamaa.

Alipowaamini kuwa wanaweza kumsaidia aliwapatia nafasi za kuwatumikia wananchi lakini wengi wao wamemwangusha kwa kushindwa kukidhi mahitaji ya wananchi na kwa kiwangi kikubwa watendaji hawaendi na mdundo wa ngoma ya ARI MPYA KASI MPYA NA NGUVU MPYA.

katika siasa kuwaweka watu uliowazoea na unaowaamini karibu nawe kiutendaji ni jambo zuri kama kweli wana malengo ya kukusaidia.Kwa upande wa JK, watu wake wa karibu wanamwangusha kwa sababu mbili kubwa:mosi waliingia katika serikali wakitamani kutumia ukaribu wao na JK kujineemesha kwanza.Miaka mitatu kwao wameitumia kujichotea na kutengenrza mazingira ya kupata zaidi.Pili wapo wanaomwangusha kwa lengo la kiumweka mahali pagumu 2010.Kwa lugha nyepesi hawa wanatumiwa au wenyewe kwa matakwa yao wanamwona JK kuwa ni msaliti.Mpasuko ulioanza ndani ya sisiemu unaakisi hili.

Mabadiliko atakayoyafanya JK ni hatua ya kusafisha serikali yake na kujenga taswira nzuri kwa umma wakati amebakiza miaka miwili tu kabla ya uchaguzi.Hata hivyo suluhisho siyo kubadili watendaji, kinachotakiwa kwenda sanjari na hilo ni usimamizi wa watendaji kule waliko pamoja na kuendesha mambo kwa uwazi.Mfano mzuri ni sakata la EPA amabalo hata sasa likiwa mahakamani bado mambo mengi na mazito yanafichwa.Usiri huu ndio unaoondoa imani ya wananchi na kuharibu taswira ya JK mbele ya watanzania waliompa kura za kishindo mwaka 2005.

Mabadiliko yaanzie ngazi ya juu ya utawala kwa kuweka kila ovu lililofichwa wazi na kuwaacha watanzania watafute mbaya ni nani.Hata kama wewe ni sisiemu damu lakini sharti nchi yako TANZANIA iwe muhimu kuliko chama chako.Hapo ndipo pa kuanza kufanyia mabadiliko kabla ya kuwabadilisha ma- DC na ma-RC
 
Kwa kweli Watanzania tunataka kuzugwa. Kifupi hii habari nzima imejaa usanii wa hali ya juu kutaka kuwazuga Watanzania. Mabadiliko yanayotaka kufanywa ni remote control ya mtu aliye nje ya utawala anayetaka kujaribu kuonyesha kwamba bado ana nguvu katika utawala wa sasa na hilo ni hatari sana kwa wananchi wa Tanzania.
 
Kwa kweli Watanzania tunataka kuzugwa. Kifupi hii habari nzima imejaa usanii wa hali ya juu kutaka kuwazuga Watanzania. Mabadiliko yanayotaka kufanywa ni remote control ya mtu aliye nje ya utawala anayetaka kujaribu kuonyesha kwamba bado ana nguvu katika utawala wa sasa na hilo ni hatari sana kwa wananchi wa Tanzania.

Ameyataka mwenyewe!!! Ukitaka kufanikiwa kiutendaji wa dhamana kubwa kama ya JMK kuliongoza taifa hupaswi kuwachagua wasaidizi wako kutoka kwenye kapu la 1. maswahiba 2. mwenzetu 3. mashoga/marafiki/maswahiba wa mkeo. Katika maswahiba au wenzetu hao ndo utakuta wanajeshi, waalimu, waandishi wa habari walioweza kupeperusha habari zako vizuri, vimada wa maswahiba, yaani you name all. Sasa niambie hapo utafanikiwa vipi katika utekelezaji??? Ufahamu kuwa huwezi kumkemea hata kama atafanya vibaya!!!

On the other hand, wakuu wengine wa Wilaya walichaguliwa ili kuweka mazingira mazuri ya uchaguzi mwaka 2010 (majina kapuni) kwa baadhi ya wakuu fulani na ilikuwa ni mtandao haswa!!!!!!!!!!! Na kwa sasa wanaweza kuonekana ni hatari kwa uongozi so to hell with them!!!!! Kama unaweza kufanya ka analysis kadogo jaribu kupata jina la kila mkuu wa Wilaya then fanya upembuzi utajua aliwekwa kwa upande upi (mtandao au si mtandao).

Any way, tuyasubiri mabadiliko hayo japo tetesi zimekuwako muda sasa na hakuna kilichafanyika.
 
Back
Top Bottom