RAIS Jakaya Kikwete, ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa, amesema mtu yeyote atakayebainika kujihusisha na ufisadi hata kama ni mwanachama wa chama hicho, atashughulikiwa.
Alisema orodha ya majina ya watu wanaotuhumiwa imekuwa ikipokewa na wamekuwa wakichunguzwa, kwa kuzingatia utaratibu uliopo wa kuchunguza na kamwe Serikali haiwezi kukurupuka na kuwakamata na kuwaweka ndani.
Alisema hata mtu anayetajwa katika orodha hiyo ni lazima atendewe haki kwa kuwa zipo sheria na taratibu zinazomlinda.
"Mafisadi ni lazima washughulikiwe ili nchi ipate heshima naomba wale wote wanaowafahamu wasaidie kuwataja," alisema.
source: Nifaamishe
Alisema orodha ya majina ya watu wanaotuhumiwa imekuwa ikipokewa na wamekuwa wakichunguzwa, kwa kuzingatia utaratibu uliopo wa kuchunguza na kamwe Serikali haiwezi kukurupuka na kuwakamata na kuwaweka ndani.
Alisema hata mtu anayetajwa katika orodha hiyo ni lazima atendewe haki kwa kuwa zipo sheria na taratibu zinazomlinda.
"Mafisadi ni lazima washughulikiwe ili nchi ipate heshima naomba wale wote wanaowafahamu wasaidie kuwataja," alisema.
source: Nifaamishe