Mwitongo
JF-Expert Member
- Jan 30, 2009
- 312
- 360
chanzo: gazeti la MTANZANIA
Mfanyabiashara awanasa wabunge
*Awaandalia semina, awapa posho ya kujikimu
*Awandaa wapinge ugawaji vitalu vya uwindaji
*Matokeo ya kazi kuanza kusikika bungeni leo
Na Mwandishi Wetu
Mfanyabiashara ambaye pia ni mwanasheria maarufuku kutoka Arusha anayejihusisha na biashara ya uwindaji wa kitalii, ameandaa semina nono kwa wabunge wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira.
Matokeo ya semina hiyo yanatarajiwa kuanza kusikika bungeni leo kwani kuna kundi la wabunge walioandaliwa kuhakikisha wanatetea ugawaji upya wa vitalu vya uwindaji wa kitalii. Kama ilivyo mijadala mingine, wananchi watakuwa na fursa ya kuwasikia wabunge hao wakitetea wazungu wapewe vitalu zaidi.
Mfanyabiashara huyo mwenye ukwasi kutoka kaskazini mwa nchi, aliandaa semina hiyo Jumatatu wiki hii katika Hoteli ya St. Gasper mjini Dodoma, akilenga kuwandaa wabunge hao ili wafanikishe mpango wake ambao mara zote umelemea kuwabeba wazungu kwenye tasnia ya uwindaji wa kitalii.
Taarifa za kufanyika kwa semina hiyo zilitawaliwa na usiri wa hali ya juu. Zilisambazwa kwa wajumbe na mmoja wa wajumbe kwa njia ya mdomo na ujumbe mfupi wa maandishi wa simu, tofauti na semina zote zenye nia njema ambazo hutangazwa hadharani.
Semina ilianza saa saba mchana katika ukumbi huo na kumalizika saa 10 jioni. Baada ya hapo, wajumbe hao walipewa posho ambayo mmoja wa wabunge ameeleza bayana kuwa ilikuwa "nono mno".
Katika kuthibitisha usiri wa semina hiyo, mwandaaji wa mada hakuweka jina lake wala la taasisi anayoiwakilisha kwenye mada aliyoiandaa kwa maandishi. MTANZANIA ina nakala hiyo na nyingine ya Ripoti ya Uwindaji alizowapa wabunge hao.
Wabunge hao waliitwa kwa ajili ya kuwekwa sawa na mfanyabiashara huyo ambaye ni miongoni mwa wanasheria wanaojihusisha sana na masuala ya uwindaji wa kitalii, akiwa amejiegemeza zaidi kwa raia wa kigeni.
Mmoja wa wajumbe wa Kamati hiyo amesema kwamba semina hiyo iliandaliwa kama sehemu ya kuwaandaa wabunge ili wahakikishe kuwa wanatumia ushawishi wao wa kuzungumza bungeni ili kulishawishi Bunge liiamuru Serikali irejee ugawaji vitalu vya uwindaji.
Habari za uhakika zinaonyesha kuwa Kamati Ndogo ya Bunge iliyoundwa kuchunguza usafirishaji wanyamapori leo inatarajiwa kuwasilisha ripoti yake bungeni.
Kuna habari kwamba kwenye uchunguzi huo haikubaini moja kwa moja kama kweli twiga wawili, na wanyama wengine walisafirishwa kinyemela.
Hata hivyo, kwenye suala la ugawaji vitalu kunaonekanakuwa ndiko Kamati hiyo imeegemea zaidi kwa kutoa mapendekezo yanayohamasisha ugawaji vitalu ufanywe upya, huku ikielezwa kuwa kuna idadi ya kampuni za kizalendo zilizopewa vitalu bila kuwa na uwezo.
Tangu mwaka jana, MTANZANIA imekuwa ikieleza kuwa baadhi ya mawakala wa wazungu waliokosa vitalu, wanawatumia Watanzania kuhakikisha wanawatubuni wabunge ili wakubaliane na mpango wa kugawa upya vitalu vya uwindaji wa kitalii.
Taarifa ya kuwatisha Watanzania
Kwenye mada iliyowasilishwa katika hoteli ya St. Gasper, mtoa mada ambaye ni mwanasheria wa kampuni zaidi ya nne za uwindaji, mmiliki wa kampuni moja na mmoja wa wanahisa katika kampuni nyingine mbili, anawaeleza wabunge hao kuwa ugawaji vitalu uliofanywa unahatarisha rasilimali ya wanyamapori.
Licha ya kukiri kwenye mada yake kuwa Tanzania ndiyo nchi pekee duniani yenye wanyamapori wasiokuwa na mfano, anasema ugawaji uliofanywa utawafanya wawindaji matajiri kutokuja nchini.
Anapinga ugawaji vitalu kwa namna ulivyofanywa kwa kusema, "Ugawaji vitalu kwa ajili ya uwindaji wa kitalii kwa makampuni mbalimbali kwa kipindi cha mwaka 2013-2018 umeongeza tishio la wanyama wetu na viumbe mbalimbali kuongeza kasi ya kumalizika."
Anatoa sababu kadhaa za kuwapo kwa hatari hiyo kuwa ni kuongezeka kwa idadi ya vitalu vya uwindaji, na ugawaji vitalu kutozingatia sheria ya uhifadhi wa wanyamapori na ikolojia ya eneo husika.
Anatoa mfano wa ugawaji vitalu vilivyopo Ziwa Natron kuwa umeenda kinyume cha kifungu 16 (4 na 5) ambacho kinasema Waziri hatagawa eneo kabla ya kushirikisha Serikali za Vijiji na kutangaza maeneo hayo kwenye Gazeti la Serikali. Eneo jingine analolalamikia ni la Pori la Akiba la Ugala.
Hata hivyo, imebainika kuwa juhudi za mfanyabiashara huyo ni kuhakikisha kuwa baadhi ya maeneo aliyowahakikishia wadau wake (Wazungu) kuwa wangeyapata, yametolewa kwa kampuni nyingine. Miongoni mwa maeneo aliyoapa kuyarejesha kwa udi na uvumba, ni ya Maswa ambayo kuna ahadi ya kutoa kiasi chochote cha fedha ili kuyapata kutokana na kuwa na wanyama wengi, kwa muda mrefu na wanaopenda na wawindaji wengi.
Mara zote Wizara ya Maliasili na Utalii imesema kwamba ugawaji vitalu katika maeneo hayo ulilenga kuongeza mapato ya Serikali na pia kuzifanya kampuni nyingine ziweze kupata wanyamapori ambao hawapatikani maeneo mengine.
Safari ya kufanikisha matakwa ya wazungu
Katika kuweka mambo sawa, mmoja wa wajumbe wenye ushawishi mkubwa kwenye Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, alisafiri kwenda Afrika Kusini ambako pamoja na mambo mengine yaliyompeleka, aliweza kuonana na baadhi ya mawakala wa Wazungu wanaotaka ugawaji vitalu ufanywe upya.
"Alikwenda Novemba 26 hadi Desemba 7, 2010. Aliwekwa sawa na wanaotaka ugawaji urejewe upya, akawaahidi kuwasaidia kadri atakavyoweza. Akawahakikishia kuwa Spika ni ‘mwelewa', hivyo wasiwe na wasiwasi," kimesema chanzo chetu.
Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira ni Mbunge wa Kahama, James Lembeli (CCM).
Ingawa suala la vitalu liliingizwa kwenye Kamati Ndogo inayoongozwa na Mbunge wa Mafia, Abdulkarim Shah (CCM), habari za uhakika zinaonyesha kuwa hakuna malalamiko rasmi yaliyowasilishwa kwenye Kamati ‘mama' kama alivyonukuliwa na Lembeli.
"Kwenye vitalu, Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira itueleze imekutana na wanachama au chombo gani cha wawindaji?
"Kinachofanywa na Kamati ya Bunge ni kuingilia utendaji kazi wa Wizara ya Maliasili na Utalii. Sheria imeainisha wazi kuwa suala la ugawaji vitalu linafanywa na Kamati ya Ushauri wa Ugawaji Vitalu, Waziri mwenye dhamana na Mahakama.
"Mtiririko uko hivi… Kamati ya Ushauri inapitia maombi yote, inatoa alama kwa kila kampuni na kushauri kampuni gani ipate kitalu gani kati ya vile ilivyoomba. Baada ya hapo inawasilisha kwa Waziri mwenye dhamana ambaye naye anatoa uamuzi. Kama yupo asiyeridhishwa anamwandikia Waziri, na Waziri anaiandikia Kamati ya Ushauri ili kujibu hoja za mlalamikaji. Ushauri wa Kamati unarejeshwa kwa Waziri anayepaswa kutoa uamuzi wa mwisho. Kama mlalamikaji hakuridhika anaruhusiwa kisheria kwenda Mahakama Kuu.
"Utaona kuwa kama kulikuwa na malalamiko, bado mchakato upo kwenye Kamati ya Ushauri wa Ugawaji Vitalu na kwa Waziri. Sasa kwa mazingira hayo unaweza kujiuliza, imekuwaje Kamati ya Lembeli iingilie suala ambalo bado lipo kwenye mpangilio wa kupata utatuzi kwa mujibu wa sheria zilizopitishwa na Bunge?
"Kama kweli wapo waliolalamika, wameshindwa nini kwenda kwa Waziri au mahakamani? Hapo mwenye akili hawezi kushindwa kutambua kuwa Kamati ya Bunge inatumiwa na waliokosa vitalu.
"Ndiyo maana kwenye mpango wao wanasema ile asilimia 15 kwa kampuni za kigeni iongezwe hadi kufikia asilimia 30. Hiyo maana yake ni kwamba ikitekelezwa wageni wengi watapata vitalu," kimesema chanzo chetu.
Kampuni zilizopata vitalu 2013-2018
Kampuni kadhaa zilipeleka maombi ya kupatiwa vitalu. Kati ya kampuni hizo ni 60 pekee zilizokidhi viwango kwa mujibu wa Sheria Namba 5 ya Wanyamapori ya mwaka 2009 na Kanuni zake za Mwaka 2010.
Hapa chini kuna orodha ya kampuni hizo. Kampuni tisa kati yake ni za kigeni. Zinamilikiwa kwa asilimia 100 na raia wa kigeni. Kampuni zilizobaki ama zinamilikiwa na Watanzania kwa asilimia 100 au kwa ubia na wageni. Nyingi zina ubia na wageni. Kampuni hizo ni:
1. Marera Lodges and Tours Ltd
(Tanzania)
2. Bunda Safaris Ltd (Tanzania)
3. Siafu Safaris Ltd (Tanzania)
4. Snfnf Hunting Safaris Ltd (Tanzania)
5. Traditional African Safaris Ltd (Tanzania)
6. Fereck Safaris Limited (Tanzania)
7. Miombo Safaris Ltd (Tanzania)
8. Tanzania Bundu Safaris (Tanzania)
9. Royal Frontiers Ltd (Tanzania)
10. Game Frontiers Ltd (Tanzania)
11. Northern Hunting Ent. Ltd (Tanzania)
12. Western Frontiers Ltd (Tanzania)
13. Mkwawa Hunting Safaris Ltd (Tanzania)
14. Ebn Hunting Safaris Ltd (Tanzania)
15. Tanza Guides Ltd (Tanzania)
16. African Buffalo Safari Trackers Ltd (Tanzania)
17. Tanzania Wildlife Co Ltd (Tanzania)
18. Old Nyika Safaris Ltd (Tanzania)
19. Muhesi Safaris Ltd (Tanzania)
20. Z. H. Poppe Ltd (Tanzania)
21. Kilimanjaro Game Trail (Tanzania)
22. Michael Matheankis Safaris (Tanzania)
23. Safari Royal Holding (Tanzania)
24. Tandala Hunting Safaris (Tanzania)
25. Go Wildhunting (Tanzania)
26. Bushman Hunting Safaris (Tanzania)
27. Melami Hunting Safaris (Tanzania)
28. Mwatisi Safaris (Tanzania)
29. Tanganyika Game Fishing (Tanzania)
30. Maasailand Hunting Co (Tanzania)
31. Safari Club Ltd (Tanzania)
32. Kiboko Hunting Safaris (Tanzania)
33. Pori Tracker Safaris of Africa (Tanzania
34. Green Miles Ltd (Tanzania)
35. Rungwa Game Safaris (Tanzania)
36. East Africa Trophy Hunters (Tanzania)
37. Kilombero North Safaris (Tanzania)
38. Wembere Hunting Safaris (Tanzania)
39 Coastal Sable Safaris (Tanzania)
40. Eshkesh Safaris (Tanzania)
41. Palahala Safaris & Horizon (Tanzania)
42. Maully Tours & Safaris (Tanzania)
43. Giant Hunting Club Ltd (Tanzania)
44. Mwanauta Co Ltd (Tanzania)
45. Wild Foot Prints Ltd (Tanzania)
46. Malagarasi Hunting Safaris Ltd (Tanzania)
47. African Trophy Hunting Ltd (Tanzania)
48. Hsksk Safaris Co Ltd (Tanzania)
49. Green Leaf Ltd (Tanzania)
50. Out of Africa Safaris (Tanzania)
51. Said Kawawa Hunting Safaris (Tanzania)
52. Tanganyika Wildlife Safaris Co Ltd (kigeni)
53. Barlette Safaris Corp Ltd (kigeni)
54. Gerald Pasanisi Safaris Corp (kigeni)
55. Game Tracker Safaris (kigeni)
56. Wengert Windrose (kigeni)
57. Grumeti Reserves (kigeni)
58. Robin Hurt Safaris (kigeni)
59. Otterlo Business Corp (kigeni)
60. Luke Samara Safaris (kigeni)
Kuna habari kwamba mkubwa umesukwa na kundi la wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi kuhakikisha kuwa mchakato mzima wa ugawaji vitalu vya uwindaji wa kitalii unaanza upya.
Baada ya kuona mbinu zote za kuwalegeza viongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii zimeshindikana, sasa mpango huo umepenyezwa kwa wabunge.
..tamati…..
Mfanyabiashara awanasa wabunge
*Awaandalia semina, awapa posho ya kujikimu
*Awandaa wapinge ugawaji vitalu vya uwindaji
*Matokeo ya kazi kuanza kusikika bungeni leo
Na Mwandishi Wetu
Mfanyabiashara ambaye pia ni mwanasheria maarufuku kutoka Arusha anayejihusisha na biashara ya uwindaji wa kitalii, ameandaa semina nono kwa wabunge wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira.
Matokeo ya semina hiyo yanatarajiwa kuanza kusikika bungeni leo kwani kuna kundi la wabunge walioandaliwa kuhakikisha wanatetea ugawaji upya wa vitalu vya uwindaji wa kitalii. Kama ilivyo mijadala mingine, wananchi watakuwa na fursa ya kuwasikia wabunge hao wakitetea wazungu wapewe vitalu zaidi.
Mfanyabiashara huyo mwenye ukwasi kutoka kaskazini mwa nchi, aliandaa semina hiyo Jumatatu wiki hii katika Hoteli ya St. Gasper mjini Dodoma, akilenga kuwandaa wabunge hao ili wafanikishe mpango wake ambao mara zote umelemea kuwabeba wazungu kwenye tasnia ya uwindaji wa kitalii.
Taarifa za kufanyika kwa semina hiyo zilitawaliwa na usiri wa hali ya juu. Zilisambazwa kwa wajumbe na mmoja wa wajumbe kwa njia ya mdomo na ujumbe mfupi wa maandishi wa simu, tofauti na semina zote zenye nia njema ambazo hutangazwa hadharani.
Semina ilianza saa saba mchana katika ukumbi huo na kumalizika saa 10 jioni. Baada ya hapo, wajumbe hao walipewa posho ambayo mmoja wa wabunge ameeleza bayana kuwa ilikuwa "nono mno".
Katika kuthibitisha usiri wa semina hiyo, mwandaaji wa mada hakuweka jina lake wala la taasisi anayoiwakilisha kwenye mada aliyoiandaa kwa maandishi. MTANZANIA ina nakala hiyo na nyingine ya Ripoti ya Uwindaji alizowapa wabunge hao.
Wabunge hao waliitwa kwa ajili ya kuwekwa sawa na mfanyabiashara huyo ambaye ni miongoni mwa wanasheria wanaojihusisha sana na masuala ya uwindaji wa kitalii, akiwa amejiegemeza zaidi kwa raia wa kigeni.
Mmoja wa wajumbe wa Kamati hiyo amesema kwamba semina hiyo iliandaliwa kama sehemu ya kuwaandaa wabunge ili wahakikishe kuwa wanatumia ushawishi wao wa kuzungumza bungeni ili kulishawishi Bunge liiamuru Serikali irejee ugawaji vitalu vya uwindaji.
Habari za uhakika zinaonyesha kuwa Kamati Ndogo ya Bunge iliyoundwa kuchunguza usafirishaji wanyamapori leo inatarajiwa kuwasilisha ripoti yake bungeni.
Kuna habari kwamba kwenye uchunguzi huo haikubaini moja kwa moja kama kweli twiga wawili, na wanyama wengine walisafirishwa kinyemela.
Hata hivyo, kwenye suala la ugawaji vitalu kunaonekanakuwa ndiko Kamati hiyo imeegemea zaidi kwa kutoa mapendekezo yanayohamasisha ugawaji vitalu ufanywe upya, huku ikielezwa kuwa kuna idadi ya kampuni za kizalendo zilizopewa vitalu bila kuwa na uwezo.
Tangu mwaka jana, MTANZANIA imekuwa ikieleza kuwa baadhi ya mawakala wa wazungu waliokosa vitalu, wanawatumia Watanzania kuhakikisha wanawatubuni wabunge ili wakubaliane na mpango wa kugawa upya vitalu vya uwindaji wa kitalii.
Taarifa ya kuwatisha Watanzania
Kwenye mada iliyowasilishwa katika hoteli ya St. Gasper, mtoa mada ambaye ni mwanasheria wa kampuni zaidi ya nne za uwindaji, mmiliki wa kampuni moja na mmoja wa wanahisa katika kampuni nyingine mbili, anawaeleza wabunge hao kuwa ugawaji vitalu uliofanywa unahatarisha rasilimali ya wanyamapori.
Licha ya kukiri kwenye mada yake kuwa Tanzania ndiyo nchi pekee duniani yenye wanyamapori wasiokuwa na mfano, anasema ugawaji uliofanywa utawafanya wawindaji matajiri kutokuja nchini.
Anapinga ugawaji vitalu kwa namna ulivyofanywa kwa kusema, "Ugawaji vitalu kwa ajili ya uwindaji wa kitalii kwa makampuni mbalimbali kwa kipindi cha mwaka 2013-2018 umeongeza tishio la wanyama wetu na viumbe mbalimbali kuongeza kasi ya kumalizika."
Anatoa sababu kadhaa za kuwapo kwa hatari hiyo kuwa ni kuongezeka kwa idadi ya vitalu vya uwindaji, na ugawaji vitalu kutozingatia sheria ya uhifadhi wa wanyamapori na ikolojia ya eneo husika.
Anatoa mfano wa ugawaji vitalu vilivyopo Ziwa Natron kuwa umeenda kinyume cha kifungu 16 (4 na 5) ambacho kinasema Waziri hatagawa eneo kabla ya kushirikisha Serikali za Vijiji na kutangaza maeneo hayo kwenye Gazeti la Serikali. Eneo jingine analolalamikia ni la Pori la Akiba la Ugala.
Hata hivyo, imebainika kuwa juhudi za mfanyabiashara huyo ni kuhakikisha kuwa baadhi ya maeneo aliyowahakikishia wadau wake (Wazungu) kuwa wangeyapata, yametolewa kwa kampuni nyingine. Miongoni mwa maeneo aliyoapa kuyarejesha kwa udi na uvumba, ni ya Maswa ambayo kuna ahadi ya kutoa kiasi chochote cha fedha ili kuyapata kutokana na kuwa na wanyama wengi, kwa muda mrefu na wanaopenda na wawindaji wengi.
Mara zote Wizara ya Maliasili na Utalii imesema kwamba ugawaji vitalu katika maeneo hayo ulilenga kuongeza mapato ya Serikali na pia kuzifanya kampuni nyingine ziweze kupata wanyamapori ambao hawapatikani maeneo mengine.
Safari ya kufanikisha matakwa ya wazungu
Katika kuweka mambo sawa, mmoja wa wajumbe wenye ushawishi mkubwa kwenye Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, alisafiri kwenda Afrika Kusini ambako pamoja na mambo mengine yaliyompeleka, aliweza kuonana na baadhi ya mawakala wa Wazungu wanaotaka ugawaji vitalu ufanywe upya.
"Alikwenda Novemba 26 hadi Desemba 7, 2010. Aliwekwa sawa na wanaotaka ugawaji urejewe upya, akawaahidi kuwasaidia kadri atakavyoweza. Akawahakikishia kuwa Spika ni ‘mwelewa', hivyo wasiwe na wasiwasi," kimesema chanzo chetu.
Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira ni Mbunge wa Kahama, James Lembeli (CCM).
Ingawa suala la vitalu liliingizwa kwenye Kamati Ndogo inayoongozwa na Mbunge wa Mafia, Abdulkarim Shah (CCM), habari za uhakika zinaonyesha kuwa hakuna malalamiko rasmi yaliyowasilishwa kwenye Kamati ‘mama' kama alivyonukuliwa na Lembeli.
"Kwenye vitalu, Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira itueleze imekutana na wanachama au chombo gani cha wawindaji?
"Kinachofanywa na Kamati ya Bunge ni kuingilia utendaji kazi wa Wizara ya Maliasili na Utalii. Sheria imeainisha wazi kuwa suala la ugawaji vitalu linafanywa na Kamati ya Ushauri wa Ugawaji Vitalu, Waziri mwenye dhamana na Mahakama.
"Mtiririko uko hivi… Kamati ya Ushauri inapitia maombi yote, inatoa alama kwa kila kampuni na kushauri kampuni gani ipate kitalu gani kati ya vile ilivyoomba. Baada ya hapo inawasilisha kwa Waziri mwenye dhamana ambaye naye anatoa uamuzi. Kama yupo asiyeridhishwa anamwandikia Waziri, na Waziri anaiandikia Kamati ya Ushauri ili kujibu hoja za mlalamikaji. Ushauri wa Kamati unarejeshwa kwa Waziri anayepaswa kutoa uamuzi wa mwisho. Kama mlalamikaji hakuridhika anaruhusiwa kisheria kwenda Mahakama Kuu.
"Utaona kuwa kama kulikuwa na malalamiko, bado mchakato upo kwenye Kamati ya Ushauri wa Ugawaji Vitalu na kwa Waziri. Sasa kwa mazingira hayo unaweza kujiuliza, imekuwaje Kamati ya Lembeli iingilie suala ambalo bado lipo kwenye mpangilio wa kupata utatuzi kwa mujibu wa sheria zilizopitishwa na Bunge?
"Kama kweli wapo waliolalamika, wameshindwa nini kwenda kwa Waziri au mahakamani? Hapo mwenye akili hawezi kushindwa kutambua kuwa Kamati ya Bunge inatumiwa na waliokosa vitalu.
"Ndiyo maana kwenye mpango wao wanasema ile asilimia 15 kwa kampuni za kigeni iongezwe hadi kufikia asilimia 30. Hiyo maana yake ni kwamba ikitekelezwa wageni wengi watapata vitalu," kimesema chanzo chetu.
Kampuni zilizopata vitalu 2013-2018
Kampuni kadhaa zilipeleka maombi ya kupatiwa vitalu. Kati ya kampuni hizo ni 60 pekee zilizokidhi viwango kwa mujibu wa Sheria Namba 5 ya Wanyamapori ya mwaka 2009 na Kanuni zake za Mwaka 2010.
Hapa chini kuna orodha ya kampuni hizo. Kampuni tisa kati yake ni za kigeni. Zinamilikiwa kwa asilimia 100 na raia wa kigeni. Kampuni zilizobaki ama zinamilikiwa na Watanzania kwa asilimia 100 au kwa ubia na wageni. Nyingi zina ubia na wageni. Kampuni hizo ni:
1. Marera Lodges and Tours Ltd
(Tanzania)
2. Bunda Safaris Ltd (Tanzania)
3. Siafu Safaris Ltd (Tanzania)
4. Snfnf Hunting Safaris Ltd (Tanzania)
5. Traditional African Safaris Ltd (Tanzania)
6. Fereck Safaris Limited (Tanzania)
7. Miombo Safaris Ltd (Tanzania)
8. Tanzania Bundu Safaris (Tanzania)
9. Royal Frontiers Ltd (Tanzania)
10. Game Frontiers Ltd (Tanzania)
11. Northern Hunting Ent. Ltd (Tanzania)
12. Western Frontiers Ltd (Tanzania)
13. Mkwawa Hunting Safaris Ltd (Tanzania)
14. Ebn Hunting Safaris Ltd (Tanzania)
15. Tanza Guides Ltd (Tanzania)
16. African Buffalo Safari Trackers Ltd (Tanzania)
17. Tanzania Wildlife Co Ltd (Tanzania)
18. Old Nyika Safaris Ltd (Tanzania)
19. Muhesi Safaris Ltd (Tanzania)
20. Z. H. Poppe Ltd (Tanzania)
21. Kilimanjaro Game Trail (Tanzania)
22. Michael Matheankis Safaris (Tanzania)
23. Safari Royal Holding (Tanzania)
24. Tandala Hunting Safaris (Tanzania)
25. Go Wildhunting (Tanzania)
26. Bushman Hunting Safaris (Tanzania)
27. Melami Hunting Safaris (Tanzania)
28. Mwatisi Safaris (Tanzania)
29. Tanganyika Game Fishing (Tanzania)
30. Maasailand Hunting Co (Tanzania)
31. Safari Club Ltd (Tanzania)
32. Kiboko Hunting Safaris (Tanzania)
33. Pori Tracker Safaris of Africa (Tanzania
34. Green Miles Ltd (Tanzania)
35. Rungwa Game Safaris (Tanzania)
36. East Africa Trophy Hunters (Tanzania)
37. Kilombero North Safaris (Tanzania)
38. Wembere Hunting Safaris (Tanzania)
39 Coastal Sable Safaris (Tanzania)
40. Eshkesh Safaris (Tanzania)
41. Palahala Safaris & Horizon (Tanzania)
42. Maully Tours & Safaris (Tanzania)
43. Giant Hunting Club Ltd (Tanzania)
44. Mwanauta Co Ltd (Tanzania)
45. Wild Foot Prints Ltd (Tanzania)
46. Malagarasi Hunting Safaris Ltd (Tanzania)
47. African Trophy Hunting Ltd (Tanzania)
48. Hsksk Safaris Co Ltd (Tanzania)
49. Green Leaf Ltd (Tanzania)
50. Out of Africa Safaris (Tanzania)
51. Said Kawawa Hunting Safaris (Tanzania)
52. Tanganyika Wildlife Safaris Co Ltd (kigeni)
53. Barlette Safaris Corp Ltd (kigeni)
54. Gerald Pasanisi Safaris Corp (kigeni)
55. Game Tracker Safaris (kigeni)
56. Wengert Windrose (kigeni)
57. Grumeti Reserves (kigeni)
58. Robin Hurt Safaris (kigeni)
59. Otterlo Business Corp (kigeni)
60. Luke Samara Safaris (kigeni)
Kuna habari kwamba mkubwa umesukwa na kundi la wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi kuhakikisha kuwa mchakato mzima wa ugawaji vitalu vya uwindaji wa kitalii unaanza upya.
Baada ya kuona mbinu zote za kuwalegeza viongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii zimeshindikana, sasa mpango huo umepenyezwa kwa wabunge.
..tamati…..