Jicho la mwewe: ATCL saga

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Feb 4, 2009
74,891
155,905
Wengi wameanza kudai kuwa Serikali imekosea sana kununua ndege maana ni vitu vya hovyo na vyenye kuleta hasara tu kwenye nchi.

Kabla sijaenda mbali, ngoja niulize vijiswali..

1. Hivi pesa zote Serikali inazozitoa kwenye mikopo ya elimu ya juu na kuchelewa kupata return, Je ni hasara au faida? Mbona wapinzani hamjazisemea?

2. Hivi pesa zote Serikali inazozitoa kama ruzuku ya vyama vya siasa, ni hasara au faida kwa nchi?

3. Hivi fedha zote Serikali inazozotoa kuchapisha vitambulisho vya taifa na vipalata vya mpiga kura na kuvigawa bure bila malipo, ni hasara au faida kwa nchi?

4. Hivi mnajua kuwa treni ya abiria, Huduma za umeme, maji, tiba ( hospital) huendeshwa bila ya Serikali kupata faida yoyote? Je ni hasara au faida kwa Nchi?

Ndugu zanguni watanzania wapenzi, siku zote Serikali huwa haifanyi biashara Bali inatoa Huduma. Hela kidogo tunazozitoa kama malipo ni kama kusaidia uendeshaji na ujenzi wa nchi yetu kwa mikono yetu wenyewe.

Serikali ina mipango ya aina 3:

1. Mipango ya muda mfupi

2. Mipango ya muda wa kati.

3. Mipango ya muda mrefu.

Pia kwa sisi tuliyopitia elimu kidogo ya miradi na uwekezaji, tunajua kuwa :

- Kuna uwekezaji wa muda mfupi, wa kati na wa muda mrefu..

- Kuna miradi ya muda mfupi, wa kati na wa muda mrefu.

Shirika letu la ndege " ATCL" kama mashirika mengine ya ndege duniani hutoa Huduma na pia kwa taifa ni uwekezaji au mradi wenye kuleta faida kwa muda mrefu ( Long term).

Huwezi kununua NDEGE Leo, alafu kesho ukategemea kuvuna pesa eti faida.

ATCL kupata hasara sio jambo la Ajabu kabisa, Kwa muda huu wa miaka 5-7 tusitegemee itatengeneza faida maana ile ni Project ya Long term na sio short term kama kununua unga wa ngano na kuuza maandazi barabarani.

Kwa miaka hii mitatu hathari za corona zitakuwa ni mwiba kwa biashara za Airlines na hata Shirika letu la ATCL litasurvive kidogo na kwakua lina soko zuri la ndani.

Kwa miaka hii mitano mashirika karibia yote ya ndege makubwa Emirates airlines, Ethiopia Airlines, Kenya Airways, American airlines, south afrika Airlines, British Airlines yote yametengeneza hasara kwa sababu ya Madhara ya muda mrefu ya Covid 19.

Ni mjinga Pekee au mtu asiye na uelewa wakutosha kwenye swala la Airlines na mtu mwenye chuki binafsi ambaye ataizodoa serikali kuhusu hasara ya ATCL.

Kwa watu wazoefu wa mambo ya Airlines...

Hii ni hasara ndogo sana kwenye airline industry.

Industries zote za airlines zilikua very Fragile hasa kwenye kipindi hichi cha Corona..

Mashirika yote duniani yame record hasara kubwa zaidi kuliko ATCL kipindi hiki cha covid 19.

Ukizisoma Hesabu zilizokaguliaa za Precision Air kwa zaidi ya miaka 10 haijawahi kuwa na Positive Cash flowing wala kuwa na devidened kwa shareholders wake.

biashara ya ndege ni complex kidogo

The way corporate loses are calculated sio kwamba lazma hawakutengeneza faida.

Iko hivi : kama Air tanzania kwa mwaka 2020/21 kulingana na ndege ziliviozunguka walitarajia kupata 30 billion against operation cost of 5 billion, wakaja wakapata 20 billion, accounts report mwisho wa mwaka itasoma wamepata 10 bilion loss but in essence walipata 15 bilioni profit but because they didnt reach the target itasoma loss.

• TUWARUDISHE DARASANI KIDOGO

- HASARA KATIKA UENDESHAJI WA NDEGE.

Kwa Mujibu wa Ripoti ya IATA Bara la Afrika Limepoteza Kiasi Cha $ Bilion 8 Katika Soko la BIASHARA ya Ndege Kwa Mwaka 2020.

Uendeshaji wa Ndege sio sawa na Gari, Ndege inategemea sana Soko la Abiria na Soko la Mizigo Kutoka Sehemu MBALIMBALI

Katika Shirika Lolote la Ndege Linategemea Vyanzo MBALIMBALI vya Mapato :

- Upatikanaji wa Abiria.

- Upatikanaji wa Mizigo ya Kutosha.

- Muunganiko wa BIASHARA Baina ya Shirika na Shirika au Nchi na Nchi (Airlines Code share Agreement).

- Vyuo vya Mafunzo vya Shirika(Mfano Air Tanzania Training Center).

-Ruzuku toka Serikali Kuu(Subsidiary)

• FAIDA ZA MOJA KWA MOJA za Shirika Lolote la Ndege(Direct Benefits) :

- Upatikanaji wa Mapato MBALIMBALI kwa Wakati na Kujiendesha.

• FAIDA ZISIZO ZA MOJA KWA MOJA yaani Indirect Benefits) :

- Ku Boost National Development and Economy.

- Ku Boost Tourism Trade.

- Ku facilitate Passenger and Cargo Transportation.

- Kupunguza Gharama za Usafiri wa anga Hasa Kwenye Domestic and International Trade.

Kwa Shirika Letu la Air TANZANIA Lenye Idadi ya Ndege tisa "9" ikiwemo Ndege 6 Mpya(Boeing 787-8 Moja,Dash 8 400 Bombardier Tatu na Airbus A220-300 Mbili zenye Jumla ya Thamani ya USD 488.6 Million na Life span ya Miaka 27-30).

Tusitegemee Faida ya Haraka Hasa Kutokana na Janga la corona Kwa Sababu Mashirika Mengi Makubwa yamepata HASARA Kubwa Kutokana na ukosefu wa Abiria na Mizigo na Kufungwa kwa Nchi MBALIMBALI Kutokana na Janga Hili na kumbuka Kama Shirika(Air Tanzania) lilikuwa na Mikakati Mikubwa ya Safari za kwenda Mashariki ya Mbali Hasa Guenzhou China,Bombay India na Nchi MBALIMBALI ikiwemo London Uingereza...

Kutokana na Majanga Haya Automatic Lazima Mapato yashuke kwa Kiwango Kikubwa Hasa na Hali Halisi ya Soko na Uendeshaji wa Vyombo Hivi vya Usafiri Hasa Malipo ya wafanyakazi,Ukarabati wa Vyombo,Malipo ya parking ya Viwanja vya Ndege,Malipo ya anga na Tozo MBALIMBALI za aviation Industry.

Nenda Kenya Airways,Egpty Air,South African Airways,Ethiopia Airlines ...Kote Huko Utakuta Hasara kubwa Katika Uendeshaji..

Ni muhimu sana tuwe tunafuatilia taarifa, wakati ATCL yetu (shirika linalofufuliwa) likitajwa kupata hasara ya shilingi Bilioni 60 kwa mwaka mmoja, na baadhi ya watu kuifanya kuwa ajenda kubwa na jambo la kushangaza sana, nataka mfuatilie pia hasara za baadhi ya mashirika makongwe na makubwa zaidi barani Afrika.

- Mathalani, Shirika la Ndege la Kenya (Kenya Airways) limepata hasara ya zaidi ya Shilingi za Kitanzania Bilioni 700 (mara 11 ya hasara ya ATCL) katika kipindi hicho hicho ambacho ATCL imepata hasara ya tzs Bilioni 60.

- Na shirika la ndege kongwe zaidi Afrika, Ethiopian Airlines, limepata hasara ya zaidi ya Shilingi za Kitanzania Tzs Trilioni 1.1 (Bilioni 1,100) ambayo ni hasara kubwa mara 18.3 zaidi kuliko ATCL.

Sote hatufurahii hasara hata kama sisi tuna hasara ya Bilioni 60, lakini kwa sababu mbili tu za sasa... uchanga wa ATCL na dunia kuzongwa na KORONA zinaweza kuifanya ATCL ijikongoje, wakati mashirika makubwa kama KE Airlines na ETH Airlines yakizongwa pia na korona.

Pia kwa mwaka jana peke yake, mashirika makubwa zaidi ya ndege duniani, kama – Delta Air Lines, American Airlines, Lufthansa Group, United Airlines, Air France-KLM, na IAG yamerekodi hasara kubwa kabisa kihistoria ya zaidi ya Dola za Marekani Bilioni 110 ambayo ni zaidi ya shilingi trilioni 2,500 za Tanzania.

Mwisho wa siku na katikati ya changamoto hizi, tunakubaliana kuwa ATCL inahitaji mikakati na mbinu za hali ya juu kibiashara ili itoke hapo ilipo, ikiwemo kuacha kabisa kufanya kazi kwa mazoea.

Tuache kuingiza siasa kwenye sensitive issues.

Ahsanteni sana!.
 
Siyo mpenzi wa serikali kufanya biashara ila...

Ku reason na watu ambao ni ama hawataki au hawana uwezo wa kufanya hivyo.

An exercise in futility.
 
Sawa mzee umeandika sana ila nina asali moja

Kati ya maandishi yako na CAG nani anajua kuwa ile si hasara bali ni huduma?

Ina maana Qatar Airlines na mashirika mengine huwa yapo tayari kuwa na moyo wa mshumaa kwa jamii kuliko nafsi yake.?

Usitake kuniaminisha kuwa ile ripoti wataalam wamempotosha CAG kutofautisha hasara, faida na huduma kwa miaka hii mitano na miaka ile waliyoiita ya mwenda wazimu
 
Mkuu Nyani Ngabu shida ni kwamba kwa muda wote wa miaka 5 tuliaminishwa shirika linatengeneza faida sana hadi kufikia kiwango linatoa gawio kumbe ni uongo sasa wananchi lazima wajiulize je mapambio yale yalilenga kitu gani hasa?

Wale walioshauri tununue kwa mkopo taratibu pamoja na aina za ndege za kununua walionekana ni wasaliti hawaitakii mema nchi sasa muda huwa ni mwalimu mzuri sana.
 
Hakuna jipya uliloandika. Tunajua yote. Zaidi sana umetuongezea hasira. Kwanza tumedanganywa na serikali yenyewe kuwa ATCL imeanza kuleta faida lakini CAG ameleta uchunguzi tofauti. Ndiyo maana wananchi wanahoji "je mwendazake angekuwepo hii ripoti ya CAG ingetolewa ilivyo au ingefanyiwa editing?". Pili, kuna uwazi, uwajibikaji, weredi na ...... upi katika kuliendesha shirika hili tofauti na awali lilipokufa?

Huko bandarini tu, pamoja na kufuatwa mara kwa mara, bado TAKUKURU linamkata njemba "mtimuliwa" akiwa na begi la mamilioni ya dola nyumbani kwake!!! Huko kwingine je, kumejaa wazalendo? Je, ni kweli baada ya miaka 20 -30 ndiyo faida itaanza kuonekana au na ndege zenyewe zitakuwa hazipo? All grounded!!!.

Ofisi ya CAG imesheheni wabobezi wa ukokotoaji wa mahesabu. Wanajua kukokotoa profit and loss za investments/projects. Si mahayawani. Wanajua pia depreciations nk . Ripoti yao inazingatia yote hayo. Usiwafundishe kazi eti ATCL ni investment/project ya
muda mrefu hivyo usitegemee faida sasa!!! Unataka kutuambia CAG na ofisi yake ilienda shule kusomea ujinga?!?
 
People are questioning the way in which the investment in the purchase of the planes was done. Wanauliza kulikuwa na haraka gani ya kununua ndege kubwa na ghali [ DREAMLINER} ilihali tulikuwa bado kukidhi soko la ndani[ Domestic market] na soko la jirani zetu[ regional market]. DREAMLINER ni ndege ya masafa marefu, kuirusha kwenda mwanza na kurudi ni hasara tupu operationally.

Tumeinunua lakini ndege ni underutilized hivyo inatutia hasara. Ikiwezekana hata hizo ndege ambazo Jiwe aliziagiza ziwe cancelled kwani ATCL kwa wakati huu haina shida ya capacity, shida iko kwenye manpower ya kuliendesha shirika kiufanisi.

Hakuna mtu mwenye akili timamu anakataa nchi kuwa na shirika lake la ndege; lakini Shirika ni lazima liwe na BODI NA MANAGEMENT YENYE WELEDI ili liendeshwe kwa ufanisi,na sio kupeana zawadi ili mradi wateuaji na wateule walifanya kazi pamoja huko TANROADS.!!! Hiyo hasara iliyopatikana miaka yote hiyo ingeweza kuwa ndogo zaidi kama professionalism was adhered to!
 
Bujibuji,

Ili tupate faida ktk biashara ya usafiri wa anga inabidi tuwekeza mapesa mengi sana kwa muda mrefu.

Faida ya mashirika ya ndege huwa ni ndogo sana, na siyo ya uhakika. Mfano mdogo ni jinsi mashirika mengin ya ndege yalivyoyumba kutokana na janga la corona.

Mpaka sasa hivi tumeshawekeza shilingi za kitanzania trillion 2. Hiyo ni kwa ndege ambazo tayari zimeshafika nchini.

Binafsi nadhani haikuwa busara kujiingiza ktk mradi huu.

Natofautiana na wewe ulipotolea mfano wa "huduma" ya mikopo ya elimu ya juu, huduma / biashara ya shirika la umeme...

Natofautiana na wewe kwasababu usafiri wa ndege, kwa mazingira ya Tz, tungeweza kuyaachia makampuni binafsi, lakini mikopo ya elimu ya juu, na shirika la umeme siyo rahisi kuyaachia makampuni binafsi.

Trillion 2 zilizotumika kununua ndege zingeelekezwa ktk sekta, au miradi, inayotoa faida ndani ya muda mfupi, na inayogusa wananchi wengi ukilinganisha na shirika la ndege.

NB:

..Nina akili timamu na ninapinga serikali yetu kununua ndege.
 
Faida ya kuwa na shirika la ndege iko wapi kwingine kama haiko kwenye 'balance book'?
Point ya watu ni ule uongo kwamba kulikuwa na faida. Ila ni kweli faida ya kuwa na shirika hai la ndege haiko kwenye balalance book pekee. Ni vizuri kufufua ATCL.
 
Nasimama upande wa JPM,

Wanaomshangilia huyu mama, nasubiri atakapoteleza kidogo mtakavyomshambulia, watanzania hatujawahi ridhika hata aongoze malaika.
 
Back
Top Bottom