Jesca Kishoa: Rais atangaze rasmi watoto wa mawaziri kusoma shule za serikali

Yani hapo ndio tutamjua mnafiki ni nani.Nikweli haiwezekani ukawa ubataka kurekebisha kitu na uchungu unausikia kwa majirani tu wewe kwako haukugusi.Watoto wa wakubwa wakianza kusoma hizo shule basi ubora wa elimu wa hizo shule utapanda kwa haraka sana.
 
Umenena vyema Mh mbunge. Angalau wangetenga shule maalum za serikali kwa ajili ya watoto wa viongozi wakuu / waandamizi wa serikali, ili iwe rahisi kwa usalama wao,ikiwemo usafiri,malazi na chakula. Viongozi hao wenye watoto watachangia gharama za uendeshaji(watu wengine wenye uwezo watoto wao waruhusiwe pia). Tunao mfano wa mabalozi na wanadiplomasia wengine kuwa na shule kwa ajili yao.
Watoto wa Nyerere , Mwinyi,Sokoine na viongozi wengine wa enzi zao tulisoma pamoja,tulicheza pamoja,tulifanya usafi na kilimo wote,tulikula wote chakula cha shule, tulilala bweni moja,JKT wote tulikwenda. Tunajua mfumo umebadilika,tunahubiri ujamaa lakini tunaishi kibepari, ndo maana napendekeza shule maalum ya serikali kwa ajili hiyo.

Mkuu haupo serious....Sasa kukitengwa shule maalum (Za watoto wa viongozi) ndo itasaidia kuboresha elimu katika shule ambazo sio maalum (Za akina sisi)!!!?...., whats the difference with private school then?
 
Kwanini rais na sio waziri wa elimu au wananchi?

Hivi hakuna cha maana mpaka tuna taka kutunga sheria za jinsi mzazi atakavyo raise familia yake!

Mambo mengine yapo mikononi mía wananchi. Kama mbunge hatoi mchango wowote bungeni wa kuboresha elimu na zaidi ya hapo watoto wake wanasoma shule binafsi wamtose kwenye kura.
 
Back
Top Bottom