Jersey yaipiku Uswisi: Ni kule Chenge alikohifadhi vijisenti, matrilioni kibao yabainika

hivi safari ya Zitto kufuatilia mabilioni Uswiss yana tija kwa nani? Nanukuu " Lema anapaswa kujua kuwa ajenda zinazompa umaarufu Zitto sio kususia posho bali masuala muhimu kama kufuatilia mabilioni ya wa tz yaliyofichwa Uswiss"

Acheni kutudanganya. Watanzania tusikubali kudanganyika.

Zito anafuatilia mabilioni ya uswis kama nani? Kwa mamlaka gani?

Naomba kuuliza, je mjumbe wa halamashauri ya kijiji au balozi wa nyumba kumi anaweza kufuatilia akaunti ya mtendaji wa kijiji hata kwenye beki ya wanachi ya NMB ya wilayani kwake? Je ikiwa Barcleys (T) itakuwaje?

Zito ni nani katika international arena?

Waandishi mnajidharaulisha na mkidharauliwa kama stahili ya matendo yenu mnakuja mnakuja juu. Vipi?

Zito kama mtu binafsi hana uwezo wala mamlaka ya kufuatilia hizo pesa, labda awe na backing ya institution yenye mamlaka ya kufanya hivyo. Iwapo mataifa yanashindwa Zito aweze wapi?
 
Zitto hana nia ya dhati?

Zitto hana umaarufu?

Zitto si lolote bila chadema?

Well hayo yote tunaweza kujibu kwa jibu moja jepesi kuwa Zitto ni bora kuzidi wawakilishi wengi wa watanzania, si kwa kukataa tu kupokea posho also kwa kuonyesha kuwa si lazima upigane ngumi kuonyesha kuwa wewe unauchungu wa nchi hii.

Labda wengi mtakuwa watu wa kusahau ila Zitto Zuberi wakati wakiwa na wachache zaidi pale bungeni kama wawakilishi wa chadema ndio walifanya mambo mengi zaidi ya kukosoa serekali mpaka mtanzania kama wewe leo hii unakuja kufahamu kuwa ulikuwa unaibiwa, unanyonywa huna haki na mengine mengi.

Nijitihada zao hao wachache leo hii unaona bungeni watu wengine kama hao kina Lema na wengine wengi kwa kuwa wananchi waliamini kuwa tukizidisha nguvu zaidi mambo mengi yatakwenda huko bungeni, ila nini matokeo nowdays imekuwa ni kususa, kupigana matusi na kadhalika well kama Zitto anaonekana mnafiki kwenye kujitoa kwenye ujinga huu then bora abaki kuwa hivyo.

Well nina imani bado hata akienda UDP chama chenye muwakilishi mmoja bungeni au TLP still ZZK ataendelea kuwa bora kwa kuwa ana fahamu nini mpinzania ana paswa kufanya, huwezi kuwa mpinzani bora kwa kususa hutuba ya rais bungeni, huwezi kuwa muwakilishi kwa kurusha ngumi ndio tusema wewe ndio muwakilishi bora.

So hao ambao mnawaaminisha ni bora watuonyeshe ubora wao kwenye kutusaidia huko bungeni, watu wa kupigiwa mfano wapo kama kina LISSU, Mnyika, Mdee na wengine wengi wanasukuma gurudumu huko si wabunge ambao every day wao wapo kupigana na meya wa jiji lake?
 
Yaani mapesa yetu yaliyoibiwa na kufichwa Uswiss hata yakirudi na wezi wakajulikana haitakuwa na manufaa kwa Watanzania na CDM?! Is that what you're talking?

Kama ni ukweli basi Judge Werema was right when he said that MPs are the MOST intelligent person in Tanzania!

Frankly speaking umenikatisha tamaa kabisa na analogy yako. Kwa mtaji i huu tusahau kabisa kuiondoa CCM madarakani, kama ma-THINK TANK WA CDM ndiyo nyinyi (read SPIN DOCTORS OF CDM)
 
Baada ya kusoma kwa makini thread nyingi kuhusu sakata la Lema & Zitto, pamoja na makala isemayo "Mbunge Lema mfuasi wa siasa nyepesi" ktk gazeti la raia Mwema la jana 6/11/2013. Nimesukumwa kutoa mchango wangu kama ifuatavyo; Nakubaliana na wote waliosema kuwa kitendo cha Lema kwa Zitto hakina tija kwa chadema na taifa. Pamoja na kukubaliana nao pia nia hoja kwa upande wa pili, hivi safari ya Zitto kufuatilia mabilioni Uswiss yana tija kwa nani? Nanukuu " Lema anapaswa kujua kuwa ajenda zinazompa umaarufu Zitto sio kususia posho bali masuala muhimu kama kufuatilia mabilioni ya wa tz yaliyofichwa Uswiss"

hapo kwenye nyekundu, hivi kweli hujui hayo mabilioni yatamsaidia nani?au umeamua kujitoa ufahamu ilin tu uonekane na wewe umeandika post? hebu acha unafiki na uzandiki kuwa huru na tumia akili yako siyo ya mtandao mnaouunda kumchafua Zitto kitu ambacho hakitawasaida kamwe.

Huhitaji kuwa na PHD kujua kuwa safari za Zitto kufuatilia mabilioni Uswiss hakuna tija kwa CDM, taifa au walalahoi wa TZ. Tujiulize maswali machache; 1. Je serikali ilikuwa haijui kama kuna mabilioni ya watazania yaliyofichwa Uswiss? 2. Je serikali ina nia ya kweli ya kurudisha mabilioni yaliyofichwa Uswiss? 3. Je Zitto anaikumbusha serikali, anaishawishi serikali au anaisimamia serikali ilikurudisha mabilioni hayo?

1.je kama serikali inajua kuna mabilioni yamefichwa nje na ikaamua kukaa kimya,je wengine pia wakae kimya kwavile serikali imeakaa kimya?je serikali haijui kuwa wananchi wa eneo fulani hawana maji,hawana huduma za afya,hawana shule mbona wabunge hufuatilia mambo hayo na hukusema serikali mbona inajua?
2.ukiwa mnafiki uwe unajipanga, sasa unataka Zitto huyo huyo aikumbushe,aisimamamie serikali ili mabilioni yarudi wakati huo huo unasema hayana tija kwa taifa,chama chenu na wananchi,ya nini sa kufuatilia(unafiki mbaya)


Madhalani Zitto akafanikiwa, je mabilioni hayo yatarudishwa katika akaunti ipi, ya Zitto au atarudinazo katika mfuko?. Km mzee wa vijisenti alikubali hakuna hatua iliyochukuliwa kwanini Zitto hakuanza na Mzee wa vijisenti? Je chenji ya radar iliporudi ilipelekwa wapi?

kweli wewe ni mbumbumbu,kajipange upya huna jipya hata hoja zako dhaifu sana.
sasa hata kama hela radar ilioprudi ilifanya nini na unakuja hapa kujidai unamkosoa Zitto mimi nakuona kama bogus,nakushauri nenda kajifue upya,peruzi sana ukiishaiva ndio urudi uje hapa jukwaani tofauti na hivyo utakuwa unadharaulika tu.

Zitto pigania mabadiliko ya mfumo ambao ndiyo chanzo cha ufisadi huo sio kupoteza muda wa kufuatilia mabilioni Uswiss ambazo waliozipeleka wako katika serikali (mfumo), isitoshe hata zikirudi bado zinaingia katika mifuko ya hao hao waliozipeleka.

Kama hayo mabilioni yalitoroshwa kutoka katika makampuni, je zikirejeshwa zikapelekwa kwenye kilimo huko hakuna makampuni?. Ni heri kama ungeenda kuhamasisha wananchi M4C vijijini ilikubadili mfumo.

tutajie hayo makampuni
na wewe ni heri ukakaa na kujitathimini juu ya ushabiki wako usio na manufaa yoyote,kijana jifunze kuwa muumini wa misingi na sio kuwa muumini wa makundi,watu na kufuata upepo tu.

BTW
Join Date: 22nd October 2013
Posts:12
Rep Power:305
Likes Received:6
Likes Given:0

nyinyi ndio wale wale mliotumwa kuja kuchafua watu humu.
 
Baada ya kusoma kwa makini thread nyingi kuhusu sakata la Lema & Zitto, pamoja na makala isemayo "Mbunge Lema mfuasi wa siasa nyepesi" ktk gazeti la raia Mwema la jana 6/11/2013. Nimesukumwa kutoa mchango wangu kama ifuatavyo; Nakubaliana na wote waliosema kuwa kitendo cha Lema kwa Zitto hakina tija kwa chadema na taifa. Pamoja na kukubaliana nao pia nia hoja kwa upande wa pili, hivi safari ya Zitto kufuatilia mabilioni Uswiss yana tija kwa nani? Nanukuu " Lema anapaswa kujua kuwa ajenda zinazompa umaarufu Zitto sio kususia posho bali masuala muhimu kama kufuatilia mabilioni ya wa tz yaliyofichwa Uswiss"

Huhitaji kuwa na PHD kujua kuwa safari za Zitto kufuatilia mabilioni Uswiss hakuna tija kwa CDM, taifa au walalahoi wa TZ. Tujiulize maswali machache; 1. Je serikali ilikuwa haijui kama kuna mabilioni ya watazania yaliyofichwa Uswiss? 2. Je serikali ina nia ya kweli ya kurudisha mabilioni yaliyofichwa Uswiss? 3. Je Zitto anaikumbusha serikali, anaishawishi serikali au anaisimamia serikali ilikurudisha mabilioni hayo?

Madhalani Zitto akafanikiwa, je mabilioni hayo yatarudishwa katika akaunti ipi, ya Zitto au atarudinazo katika mfuko?. Km mzee wa vijisenti alikubali hakuna hatua iliyochukuliwa kwanini Zitto hakuanza na Mzee wa vijisenti? Je chenji ya radar iliporudi ilipelekwa wapi?

Zitto pigania mabadiliko ya mfumo ambao ndiyo chanzo cha ufisadi huo sio kupoteza muda wa kufuatilia mabilioni Uswiss ambazo waliozipeleka wako katika serikali (mfumo), isitoshe hata zikirudi bado zinaingia katika mifuko ya hao hao waliozipeleka.

Kama hayo mabilioni yalitoroshwa kutoka katika makampuni, je zikirejeshwa zikapelekwa kwenye kilimo huko hakuna makampuni?. Ni heri kama ungeenda kuhamasisha wananchi M4C vijijini ilikubadili mfumo.

Mfumo ukimaanisha kuitna ccm madarakani? Kama ni ndoto za kuitoa ccm kupitia chama hiki kinachnongozwa kinafiki, kinachoshindwa kuwawajibisha mafisadi kama wanavyodai wachache kuwa kuna viongozi mafisadi ndani ya chadema basi nadhubutu kusema unaota ndoto za mchana. Muacheni zitto afanye kazi yake ya kuwasaidia walalahoi nanyie wengine pigeni m4c yenu mkisubiri ndoto yenu kutimia.
 
Zitto hana nia ya dhati?

Zitto hana umaarufu?

Zitto si lolote bila chadema?

Well hayo yote tunaweza kujibu kwa jibu moja jepesi kuwa Zitto ni bora kuzidi wawakilishi wengi wa watanzania, si kwa kukataa tu kupokea posho also kwa kuonyesha kuwa si lazima upigane ngumi kuonyesha kuwa wewe unauchungu wa nchi hii.

Labda wengi mtakuwa watu wa kusahau ila Zitto Zuberi wakati wakiwa na wachache zaidi pale bungeni kama wawakilishi wa chadema ndio walifanya mambo mengi zaidi ya kukosoa serekali mpaka mtanzania kama wewe leo hii unakuja kufahamu kuwa ulikuwa unaibiwa, unanyonywa huna haki na mengine mengi.

Nijitihada zao hao wachache leo hii unaona bungeni watu wengine kama hao kina Lema na wengine wengi kwa kuwa wananchi waliamini kuwa tukizidisha nguvu zaidi mambo mengi yatakwenda huko bungeni, ila nini matokeo nowdays imekuwa ni kususa, kupigana matusi na kadhalika well kama Zitto anaonekana mnafiki kwenye kujitoa kwenye ujinga huu then bora abaki kuwa hivyo.

Well nina imani bado hata akienda UDP chama chenye muwakilishi mmoja bungeni au TLP still ZZK ataendelea kuwa bora kwa kuwa ana fahamu nini mpinzania ana paswa kufanya, huwezi kuwa mpinzani bora kwa kususa hutuba ya rais bungeni, huwezi kuwa muwakilishi kwa kurusha ngumi ndio tusema wewe ndio muwakilishi bora.

So hao ambao mnawaaminisha ni bora watuonyeshe ubora wao kwenye kutusaidia huko bungeni, watu wa kupigiwa mfano wapo kama kina LISSU, Mnyika, Mdee na wengine wengi wanasukuma gurudumu huko si wabunge ambao every day wao wapo kupigana na meya wa jiji lake?

Mkuu Tayseer ll alama umeongea maneno kiujenzi sana mkuu. Ubarikiwe na sisi wazalendo tuendelee kuwapa moyo hivyohivyo wapambanaji wakweli.
 
Last edited by a moderator:
zitto hana umaarufu wowote kama mnavyodhani

kama anaumaarufu si ajitoe cdm aanzishe chama chake tuone watakaomfuata huko!

Lol kumbe wewe unajadili umaarufu? Samahani sijui unaweza nipa maana ya umaarufu? Manake hata ulichoandika kinajikanganya.
 
William Malecela nae ana $$$$$$ zake kule Grand Cayman

Labda useme za Bwana'ke. Lenyewe halina uwezo wa kumiliki hata sent tano ya kwake binafsi aliyoichuma kwa jasho ukiacha hizi za kupewa na Mh. "Ma'mdogo". Kubwa zima!!!
 
Halafu karibu mafisadi wote wametokana na ile elimu ya kikoloni na ya kipindi cha mwalimu Nyerere.
 
Yote yanayofanyika hata uongozi wa juu unayajua.Alafu eti m2 anatoa hotuba kwa kusema, eti tumejizatiti kuwaondoa watendaji wabovu. Mbona usiwaondoe hawa waliojilimbikizia hayo mapesa kama wewe huusiki pia.
 
Nilishaandika hapa kwamba Zitto anyamaze kimya mpaka atakapomaliza uchunguzi. Akimaliza aende full force mpaka kutaja majina kwa ushahidi.

Sasa kelele zake zimefanya watu wahamishe hela kitoka Uswizi.
 
Mi nafikiri kwa yeyote yule aliyeficha fedha hizo iwe ni Uswis au visiwani Ireland,huko huko!Huo ni uhaini.Kila siku mnahubiri Tanzania ni nchi maskini kumbe ni uongo na unafiki mkubwa.Hapa naomba niseme kinachokosekana ni utashi wa kuamua maamuzi magumu ya kuwashughulia hawa wazee wa vijisenti kwa kuhofia upotevu wa hela hizo.Sasa sijui hoja hii kwa mwenye akili timamu ina uzito?
Ngoja niwaambie wenzangu,hawa watu wamejiandaa kuja kuitawala nchi kwa njia yoyote ile au chama chochote kwa sababu hapo baadaye hakuna atakaye weza kuwahimili au kuwazuia.Kwa sababu watakuwa wameshika uchumi wote wa nchi.Hebu tukae na kusubiri.
 
Kwa mbali ndugu ZITTO namfanananisha na watu waliokuwa na uchungu na nchi hii kina EDWARD MORINGE SOKOINE.Nikimkumbuka waziri huyu naambulia uchungu mkubwa moyoni.
 
Wa-Danganyika tumelala usingizi Mafisadi wanachota pesa za walala hoi Masikini utafikiri zipo kisimani hazina wenyewe Ewe Mungu liokoe hili Taifa la wanyonge Uwaangamize Mafisadi ameen.
 
Back
Top Bottom