Je wajua - Spice Islander imeua watu kuliko Titanic?!

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,150
18,810
Ni kitu ambacho kinasikitisha kila ninapokifikiria, kwamba disaster ya Spice Islander ya Zanzibar iliua watu wanaokadiriwa kuwa 2800, wakati ile ya Titanic iliua watu wapatao 1500. Na ni kweli watoto na wanawake wengi sana walikufa Spice Islander ukilinganisha na Titanic. Machozi yananilengalenga nikifikiria kina mama katika Spice Islander wakiwa hawana la kufanya bali kukumbatia watoto wao waliokuwa wakilia kwa woga na kujiandaa kufa nao, wakijua hakuna ambalo wangeweza kufanya kujiokoa wao na watoto wao wadogo. Nafikiria ningekuwaje ikiwa mwanangu mdogo na mama yake wangekuwa katika hali ile, ndoto gani ningeota kila usiku nikilala; ninajaribu kuwaokoa?

Kwa nini basi dunia ilikaa kimya juu ya Spice Islander ukilinganisha na Titanic? Ina maana dunia inajali zaidi gharama ya meli zilizohusika kuliko roho za binadamu zilizopotea?

Na viongozi wetu wamesahau kama vile lilikuwa tu ni jambo la kawaida. Imekuwaje binadamu tumekuwa wanyama kiasi hiki?
 
  • Thanks
Reactions: amu
inaweza ukawa sawa mkuu lakini ukumbuke dunia yetu ni kubwa na binadamu wana tabia ya kujiangalia zaidi kabla ya kutegemea kuonwa na wakazi wengine wa dunia. Ndio maana kuna maeneo tofauti ya utawala.
Wazungu kama wao wilitangaza sana Titanic na kushughulika nayo kwa sababu ilikuwa imewabeba wao, na baada ya hapo ndio maana wanajitahidi kuweka sheria za vyombo vya majini na kuzifuata kikamilifu.
Pia ukumbuke wao wanaamini kuwa sisi hatuthamini maisha na sio ajabu siku ule msiba wa Spice Islander wanasiasa walikuwa kwenye siasa zao wakati wamekufa watu zaidi ya 2800 lakini uliona siku basi lilivyogonga ukuta Uswizi likiwa na watoto kutoka Belgium, EU nzima iliomboleza.
Hivyo usiwalaumu wazungu bali jilaumu mwenyewe na viongozi wetu kwa kuwa kama tulivyo (kutojali maisha).
 
Yeah, nilikuwa namsomesha mtu kuhusu hili. Halafu huko Malaysia/ Singapore/ The Phillipines watu wanakufa kila mwezi karibu hata hatusikii sana. Ukiwa na mshiko hata historia unaweza kuiandika unavyotaka.

Halafu hata hapa nchini ajali za barabarani zinaua watu wengi zaidi ya za majini, lakini za majini hutokea mara chache na zinaua wengi kwa mpigo.

Lakini utaona HIV/AIDS na ajali za majini zinapewa kipaumbele zaidi.
 
2800? WENGI SANA ,
EH MUNGU NA SERIKALI ILITANGAZA WANGAPI?
Hivi vyote vinachaNGIWA NA KUWA NA TAKWIMU HAFIFU NA KUTOKUWA WAWAZI.
 
Hii Habari ilipaswa kuwepo kwenye Jukwaa la kimataifa kwa sababu Zanzibar ni nchi. Mungu awaweke marehemu wote sehemu wanazostahili motoni/peponi,
 
mimi mkuu nitakuuliza tu swali moja...hivi ajali ya Titanic ilikugusa vipi? hata kama ilitokea ukiwa hujazalia ila najua habari zake utakua unazifahamu
 
Ni kitu ambacho kinasikitisha kila ninapokifikiria, kwamba disaster ya Spice Islander ya Zanzibar iliua watu wanaokadiriwa kuwa 2800, wakati ile ya Titanic iliua watu wapatao 1500. Na ni kweli watoto na wanawake wengi sana walikufa Spice Islander ukilinganisha na Titanic. Machozi yananilengalenga nikifikiria kina mama katika Spice Islander wakiwa hawana la kufanya bali kukumbatia watoto wao waliokuwa wakilia kwa woga na kujiandaa kufa nao, wakijua hakuna ambalo wangeweza kufanya kujiokoa wao na watoto wao wadogo. Nafikiria ningekuwaje ikiwa mwanangu mdogo na mama yake wangekuwa katika hali ile, ndoto gani ningeota kila usiku nikilala; ninajaribu kuwaokoa?

Kwa nini basi dunia ilikaa kimya juu ya Spice Islander ukilinganisha na Titanic? Ina maana dunia inajali zaidi gharama ya meli zilizohusika kuliko roho za binadamu zilizopotea?

Na viongozi wetu wamesahau kama vile lilikuwa tu ni jambo la kawaida. Imekuwaje binadamu tumekuwa wanyama kiasi hiki?
Hata wewe ni kama walimwengu wengine tu. Leo tarehe 21/5/2012 ni miaka 16 kamili tokea MV Bukoba ipinduke na kuzama, ila wewe umekumbuka Titanic na kusahau MV Bukoba iliyoua watanzania wengi.
 
Hata wewe ni kama walimwengu wengine tu. Leo tarehe 21/5/2012 ni miaka 16 kamili tokea MV Bukoba ipinduke na kuzama, ila wewe umekumbuka Titanic na kusahau MV Bukoba iliyoua watanzania wengi.

Kwa hiyo ulitaka nilinganishe MV Bukoba na Spice Islander? Japo kifo hata cha mtu mmoja ni majonzi, nadhani unapaswa kuwa na akili ya kuona kwa nini nililinganisha Spice Islander na Titanic. Na hapa naongelea tukio la karibuni ambalo limetokea tukiwa na JF. Kama wewe unaona ni vema kulinganisha MV Bukoba na Titanic go ahead, anzisha thread. Fikiria kabla ya kukurupuka na kutuhumu.
 
mimi mkuu nitakuuliza tu swali moja...hivi ajali ya Titanic ilikugusa vipi? hata kama ilitokea ukiwa hujazalia ila najua habari zake utakua unazifahamu

Watu8, disaster ya Titanic ilinifanya nione kama watu walishtushwa na kilichotokea na hata kuchukua hatua stahili kuhakikisha haijirudii tena, na nikidhani yote haya yalitokana na idadi kubwa ya watu iliyopotea. Nilitarajia dunia pia itashtushwa na idadi ya watu iliyopotea Spice Islander. Naona labda sikuwa sahihi, issue ilikuwa ni mali iliyopotea. Labda ndio maana uchunguzi wa kina na gharama unafanywa ndege ikianguka - japo idadi ya abiria si kubwa kama wanaokuwa katika meli, bali kwa kuwa gharama ya ndege ni kubwa sana.
 
Kitu gani kimekufanya uikumbuke MV SPICE ISLANDERS wakati leo tunaadhimisha miaka 16 ya kuzama kwa meli ya mv BUKOBA, au we ni mzanzibari?
 
Hata wewe ni kama walimwengu wengine tu. Leo tarehe 21/5/2012 ni miaka 16 kamili tokea MV Bukoba ipinduke na kuzama, ila wewe umekumbuka Titanic na kusahau MV Bukoba iliyoua watanzania wengi.

Kwani Wapemba wangapi walifia kwenye MV Bukoba hadi aikumbuke?.
Wapemba ni wabaguzi sana jombaa!!
 
Why does Titanic hold the record? And i keep asking myself, hawa weupe ni wa bei ghali sana? wanadiriki hata kubadilishana mweupe mmoja kwa mamia, hivi exchange rate ya mtu mweusi kwa mweupe ikoje?
 
Why does Titanic hold the record? And i keep asking myself, hawa weupe ni wa bei ghali sana? wanadiriki hata kubadilishana mweupe mmoja kwa mamia, hivi exchange rate ya mtu mweusi kwa mweupe ikoje?

mtu mmoja mweupe ni sawa na watu elfu kumi weusi!
 
Kwa hiyo ulitaka nilinganishe MV Bukoba na Spice Islander? Japo kifo hata cha mtu mmoja ni majonzi, nadhani unapaswa kuwa na akili ya kuona kwa nini nililinganisha Spice Islander na Titanic. Na hapa naongelea tukio la karibuni ambalo limetokea tukiwa na JF. Kama wewe unaona ni vema kulinganisha MV Bukoba na Titanic go ahead, anzisha thread. Fikiria kabla ya kukurupuka na kutuhumu.
Unakasirika nini? Nimekuuliza hivyo kwa vile pamoja na kuwa umeanzisha thread yako ambayo kimsingi ina mantiki umelinganisha Spice Islander na Titanic na kusahau MV Bukoba tena katika siku ya kumbukumbu ya ajali hiyo. Ndio maana nasema hata wewe ni kama hao unaowalaumu kwa kupuuza Spice Islander wakati nawe unakumbuka Titanic tuu.
Aliye kurupuka bila kufikiri ni wazi ni wewe.
 
Why does Titanic hold the record? And i keep asking myself, hawa weupe ni wa bei ghali sana? wanadiriki hata kubadilishana mweupe mmoja kwa mamia, hivi exchange rate ya mtu mweusi kwa mweupe ikoje?

inategemea nani anayefanya hiyo exchange.
 
Back
Top Bottom