Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,617
- 113,835
Wanabodi,
Leo ni Sikukuu ya Muungano, imeamuliwa kuidhinishwa kimya kimya.
Naitafakari kidogo siku hii nikiangazia umuhimu wa siku hii na kuilinganisha ya siku ya uhuru.
Katika taifa lolote, siku muhimu kuliko zote ni siku inayoitwa National Day, iwe ni siku ya uhuru au Mapinduzi, umuhimu wa national day ndio siku taifa husika lilipoanza au siku ya muhimu sana kwa taifa husika kuliko siku nyingine yoyote.
Kwa Tanzania, siku muhimu ya kwanza ni ambayo ndio tunaiita Tanzania National Day ni siku ya Uhuru na Jamuhuri ambayo huadhimishwa kwa paredi ya Uhuru kila tarehe 9 Desemba ya kila mwaka.
Kutokana na umuhimu wa siku hii, siku hii imekuwa ikiheshimiwa sana na kuadhimishwa miaka yote kwa paredi ya uhuru, bila kukosa hadi rais Magufuli alipoingia na Awamu yake ya Tano, kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi hii, maadhimisho ya siku hii kwa paredi ya uhuru yalisitishwa na badala yake tukaandimisha kwa kufanya usafi.
Akina sisi watu wa kujiuliza, tukajiuliza mamlaka ya rais wa JMT kufuta siku muhimu kama hii just by press release ya Kurugenzi yake ya mawasiliano bila a decree ameupata wapi?.
Baada ya bandiko hili, decree ilitayarishwa ndipo ikatolewa.
Baada ya kufutwa kwa paredi ya uhuru, sherehe kadhaa zilikuja kufutwa ikiwemo Muungano. Hoja ya kufuta maadhimisho haya ni kubana matumizi na kuto justify lavish spending kwa shughuli za cosmetics tuu badala ya developments. Hili ni jambo jema.
Hata hivyo angalieni kilichokuja kutokea kwa sherehe hizi hizi za Muungano mwaka uliofuatia.
Baada ya kufuta maadhimisho ya Uhuru ile 2015, sherehe zote za uhuru zilizofuatia ziliadhimishwa kwa sherehe. Leo tena maadhimisho ya Muungano, yamefutwa, kwa ku save money halafu subirini kufuru za maadhimisho mwaka ujao wa Uchaguzi Mkuu, tutakumbusha tulikuwa tuna save nini na tunafanya nini!. Kiukweli kuna vitu tunafanya ili tuu kuonyeshea ku save money, lakini tunapokuja ku spend twice as much on similar things, tunaonekana ni watu wa ajabu.
Japo maadhimisho ya Uhuru ndio sherehe yenye hadhi kubwa kuliko zote kwa taifa letu, in reality sherehe yenye maana kubwa kwa Tanzania ni Muungano na sio Uhuru.
Maadhimisho ya Muungano ni muhimu kuliko Uhuru kwa sababu Muungano ndio kuzaliwa kweli kwa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania. Ile sherehe ya Uhuru na Jamuhuri tuyayoiadhimisha sio uhuru wa Tanzania, ni uhuru wa Tanganyika ambayo imeishakufa na kuzikwa baada ya kuzaliwa Tanzania.
Maadhimisho ya Muungano ndio maadhimisho makubwa kwa Tanzania yote Bara na Visiwani enzi za Nyerere, Nyerere na Karume walikagua gwaride pamoja. This is the most significant national event, nalo limeahirishwa hivi hivi tuu just like that, no decree no nini!. Msije shangaa decree ikitoka kesho baada ya kuzungumzwa humu kama ile ya kufuta maadhimisho ya Uhuru.
Kama Zanzibar wamefuta jumla maadhimisho ya Uhuru wake kwa sababu ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, jee kuna ubaya na sisi tukafuta jumla maadhimisho ya Uhuru na Jamuhuri kwa sababu ni za Tanganyika na badala yake Tanzania National Day iwe siku ya Muungano, Tanzania ilipozaliwa na sio tunaadhimisha uhuru wa Tanzania siku ya uhuru wa Tanganyika badala ya kusheherekea Muungano ambao ndio siku ya kweli ya JMT ilipo zaliwa?.
Nini muhimu zaidi kati ya kuadhisha uhuru wa Tanganyika ambayo imeishakufa na kuuita Uhuru wa Tanzania, wakati kiukweli Tanzania imezaliwa April 26, 1964?.
Nawatakia Mapumziko mema ya Muungano.
Paskali
Leo ni Sikukuu ya Muungano, imeamuliwa kuidhinishwa kimya kimya.
Naitafakari kidogo siku hii nikiangazia umuhimu wa siku hii na kuilinganisha ya siku ya uhuru.
Katika taifa lolote, siku muhimu kuliko zote ni siku inayoitwa National Day, iwe ni siku ya uhuru au Mapinduzi, umuhimu wa national day ndio siku taifa husika lilipoanza au siku ya muhimu sana kwa taifa husika kuliko siku nyingine yoyote.
Kwa Tanzania, siku muhimu ya kwanza ni ambayo ndio tunaiita Tanzania National Day ni siku ya Uhuru na Jamuhuri ambayo huadhimishwa kwa paredi ya Uhuru kila tarehe 9 Desemba ya kila mwaka.
Kutokana na umuhimu wa siku hii, siku hii imekuwa ikiheshimiwa sana na kuadhimishwa miaka yote kwa paredi ya uhuru, bila kukosa hadi rais Magufuli alipoingia na Awamu yake ya Tano, kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi hii, maadhimisho ya siku hii kwa paredi ya uhuru yalisitishwa na badala yake tukaandimisha kwa kufanya usafi.
Akina sisi watu wa kujiuliza, tukajiuliza mamlaka ya rais wa JMT kufuta siku muhimu kama hii just by press release ya Kurugenzi yake ya mawasiliano bila a decree ameupata wapi?.
Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria, ongoza kwa 'presidential decrees'!
Wanabodi, Tanzania ni nchi inayofuata Katiba na kuendeshwa kwa utawala wa sheria, hivyo itaongozwa kwa mujibu wa Katiba, sheria taratibu na kanuni!, no one is above the law!. Katika kufuata sheria hizo, taratibu na kanuni, pia kuna mamlaka ambayo katiba imempa rais wetu wa JMT kuyatekeleza at...
www.jamiiforums.com
Baada ya bandiko hili, decree ilitayarishwa ndipo ikatolewa.
Amri ya Rais Kuifuta Siku ya Uhuru Haijataja Usafi!. Jee Usafi ni Amri au ni Ridhaa Tuu?!.
Wanabodi, Ile Amri ya Rais Kuifuta Sikukuu ya Uhuru ni hii hapa na Amri Hiyo Haikutaja Sababu yoyote ya msingi ya kuifuta siku hiyo, wala haijataja kuwa watu watatakiwa kufanya usafi kwa siku hiyo!. Swali ni jee hili la kuitumia siku hiyo kwa kufanya usafi ni amri au ni ombi?. Kwa...
www.jamiiforums.com
Baada ya kufutwa kwa paredi ya uhuru, sherehe kadhaa zilikuja kufutwa ikiwemo Muungano. Hoja ya kufuta maadhimisho haya ni kubana matumizi na kuto justify lavish spending kwa shughuli za cosmetics tuu badala ya developments. Hili ni jambo jema.
Hata hivyo angalieni kilichokuja kutokea kwa sherehe hizi hizi za Muungano mwaka uliofuatia.
Spending So Much Kwenye Muungano: Does This Justify Tulipofuta Uhuru Just To Save ?!.
Wanabodi, Hii ni thread ya kuhoji Spending So Much Kwenye Sherehe Muungano: Does This Justify Tulipofuta Sherehe za Uhuru Just To Save and Now we Spend So Much kwenye Sherehe ?!. Nilikuwa natafakari gharama zilizotumika kufanikisha maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano jana pale Dodoma. Mimi...
www.jamiiforums.com
Baada ya kufuta maadhimisho ya Uhuru ile 2015, sherehe zote za uhuru zilizofuatia ziliadhimishwa kwa sherehe. Leo tena maadhimisho ya Muungano, yamefutwa, kwa ku save money halafu subirini kufuru za maadhimisho mwaka ujao wa Uchaguzi Mkuu, tutakumbusha tulikuwa tuna save nini na tunafanya nini!. Kiukweli kuna vitu tunafanya ili tuu kuonyeshea ku save money, lakini tunapokuja ku spend twice as much on similar things, tunaonekana ni watu wa ajabu.
Japo maadhimisho ya Uhuru ndio sherehe yenye hadhi kubwa kuliko zote kwa taifa letu, in reality sherehe yenye maana kubwa kwa Tanzania ni Muungano na sio Uhuru.
Maadhimisho ya Muungano ni muhimu kuliko Uhuru kwa sababu Muungano ndio kuzaliwa kweli kwa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania. Ile sherehe ya Uhuru na Jamuhuri tuyayoiadhimisha sio uhuru wa Tanzania, ni uhuru wa Tanganyika ambayo imeishakufa na kuzikwa baada ya kuzaliwa Tanzania.
Maadhimisho ya Muungano ndio maadhimisho makubwa kwa Tanzania yote Bara na Visiwani enzi za Nyerere, Nyerere na Karume walikagua gwaride pamoja. This is the most significant national event, nalo limeahirishwa hivi hivi tuu just like that, no decree no nini!. Msije shangaa decree ikitoka kesho baada ya kuzungumzwa humu kama ile ya kufuta maadhimisho ya Uhuru.
Kama Zanzibar wamefuta jumla maadhimisho ya Uhuru wake kwa sababu ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, jee kuna ubaya na sisi tukafuta jumla maadhimisho ya Uhuru na Jamuhuri kwa sababu ni za Tanganyika na badala yake Tanzania National Day iwe siku ya Muungano, Tanzania ilipozaliwa na sio tunaadhimisha uhuru wa Tanzania siku ya uhuru wa Tanganyika badala ya kusheherekea Muungano ambao ndio siku ya kweli ya JMT ilipo zaliwa?.
Nini muhimu zaidi kati ya kuadhisha uhuru wa Tanganyika ambayo imeishakufa na kuuita Uhuru wa Tanzania, wakati kiukweli Tanzania imezaliwa April 26, 1964?.
Nawatakia Mapumziko mema ya Muungano.
Paskali