Je unayajua haya ya Tanganyika kabla ya uhuru?

..harakati za kuupinga ukoloni hazikuanzia DSM peke yake.

..maeneo mengi tu mikoani walikuwa wameanzisha harakati za namna moja ua nyingine kumpinga mkoloni.

..alichoweza kufanya Mwalimu ni kuzipa sura ya UTANGANYIKA na kuleta umoja ktk harakati hizo.

..katika harakati za kudai uhuru na Tanu na Mwalimu walipata msaada toka kwa watu mbalimbali hata wale ambao haikutegemewa wangesaidia. sijui kama unafahamu mchango wa Machifu mbalimbali, au shirika la kidini la kikatoliki la Maryknoll.

..maandiko ya Mohamed Said yako kuwakweza zaidi watu wa Pwani, na kupuuza mchango wa wananchi wa maeneo mengine ya Tanganyika ktk harakati za uhuru.

Great thinker asante umeongea yote muhimu, kama haelewi basi anaelimu ya chini ya darasa la nne
 
Mkuu nakubaliana na wewe wote hao wametoka Tabora na kwa kuongezea wakubwa wengi Serikalini wamesoma Tabora boys na girls, lakini Serikali kuu ndio yenye kupeleka maendeleo sehemu zinazohusika na sio kina Lipumba na Kina Samwel Sitta na sina kumbukumbu huyu Samweli Sitta alikuwa Waziri wa nini kwa miaka mingi unayoisema wewe.

Ila faraja kwa kundi lililokuwa kidete kwenye harakati za ukombozi ni kuwa JK ataiwezesha Bagamoyo kuwa moja ya sehemu ya kibiashara na kuongeza pato la mwanachi wa Bagamoyo.


Samuel Sitta aliwahi kuwa ofisi ya mwanasheria mkuu, aliwahi kuwa waziri wa ujenzi na miundombinu nafikiri kipindi cha mwinyi au kabla ya hapo, na baadaye alikuwa mkurugenzi wa Tanzania investement center (TIC), Spika, na sasa waziri wa EA. Kwa hiyo mkoa wa Tabora haujatengwa kimadaraka. Na ni kweli serikali kuu ndio inayopeleka maendeleo huko kwa kushirikiana na wananchi wa huko, na hao viongozi akina Kapuya na Sitta walikuwa sehemu ya serikali kuu.
Bottom line ni kuwa umasikini uliopo Tabora hauna tofauti na sehemu nyingine. Bahati nzuri nimetembelea mikoa yote ya Tanzania bara. Hali inatisha kwa umasikini kule vijijini. Umasikini kule hauchagui kabila wala dini. Nchi inahitaji mikakati mipya ya utendaji, si kwa Tabora au Kigoma au Shyinyanga tu, bali ni nchi nzima.
 
Samuel Sitta aliwahi kuwa ofisi ya mwanasheria mkuu, aliwahi kuwa waziri wa ujenzi na miundombinu nafikiri kipindi cha mwinyi au kabla ya hapo, na baadaye alikuwa mkurugenzi wa Tanzania investement center (TIC), Spika, na sasa waziri wa EA. Kwa hiyo mkoa wa Tabora haujatengwa kimadaraka. Na ni kweli serikali kuu ndio inayopeleka maendeleo huko kwa kushirikiana na wananchi wa huko, na hao viongozi akina Kapuya na Sitta walikuwa sehemu ya serikali kuu.
Bottom line ni kuwa umasikini uliopo Tabora hauna tofauti na sehemu nyingine. Bahati nzuri nimetembelea mikoa yote ya Tanzania bara. Hali inatisha kwa umasikini kule vijijini. Umasikini kule hauchagui kabila wala dini. Nchi inahitaji mikakati mipya ya utendaji, si kwa Tabora au Kigoma au Shyinyanga tu, bali ni nchi nzima.

Usichoke kufikiri ukishakuwa na uhakika utajibu hoja.

Well mbona Julius hakuijenga Butiama? Umeona yaliyomkuta aliekuwa Waziri wa fedha baada ya kujenga anapotoka? na kwa bahati mbaya ameangushwa mwaka jana? Kujenga taifa ni uzalendo na kujenga unapotoka ni ufisadi ndugu.
 
Mawazo yako yakiegemea udini basi kila kitu ukikiona utakichukulia udini, swali linaloulizwa kwanini historia yetu haielezi kilipotoka TANU? inaonyesha CCM inamiaka ya karibia 100 tangu ilipoanzishwa iliwa inaitwa TAA, TANU na sasa CCM. Kwanini harakati za ukombozi hazielezewi kuwa zilianza tangu 1929? huo udini unaujua wewe maana tumeona hapo juu kuna kina John Rupia na [FONT=Arial,Helvetica][SIZE=-1]Kasela Bantu. Sasa sijui hao ni wa dini gani?[/SIZE][/FONT][SIZE=-1]
[/SIZE]
Ndugu yangu. Hawa wenzetu wameshaamua kujitia upofu wasiokuwa nao. Ila wanayo sababu na haikuanza sasa. Lengo na nia yao ni kuwatisha waislamu na kuwakatisha tamaa, na katika hilo huenda wakafanikiwa kwa baadhi ila je na wale baadhi wakiujua huo mtego itakuwaje? Nashangaa sana ninapomuona mtu anaeimba nyimbo asizozijua huku akishangilia! Kwa maana hajui katika nyimbo zile kama anatukana ama anajitafutia uadui asiokuwa nao bila kujua! Wapo Wakristo wengi tu wanaojua nini maana ya Utanzania. Na ni wachache sana kama ilivyo upande wa Waislamu wanaoeneza chuki dhidi ya wengine. Tofauti iliyopo ni kwamba wale wa upande ule wana vyombo vya habari vingi na vikisema hawavisemi! wa upande uliobaki wana vichache sana ila vinapovijibu vile vinaonekana vichochezi! (WAKWELI WANGELIVISEMA VYOTE)

Nawasisitiza siku zote hapa BASI HATA KAMA HATUTAKI BASI NA TUWE WAKWELI! Ni kwa sababu ya Tanzania si sababu ya dini. Je mnadhani amani ya Tanzania ikipotea katika misingi hiyo atakaenufaika au kuhasirika ni nani?
 
Ndio maana kulikuwa na Paul Rupia na Kasela Bantu, hawa ndio waliosahaulika kwenye historia tukufu na sio waislamu peke yao mfano rupia alijitolea kwa hali na mali kwa ajili ya chama wakati wa harakati za uhuru, baadae mwanzo wa miaka ya 1961 kulikuwa na kina Oscar Kambona historia ya huyu "mkristo" mwanaharakati wa uhuru imefinyangwa pia. Ndugu zetu wakristo tunahitaji historia ya kweli kwa ajili ya vizazi vijavyo hakuna swala la udini hapa.
Kwa makusudi kabisa inabidi wachache wafe ili wengi wanufaike! Usidhani wale walisahaulika kwa bahati mbaya ndugu yangu... Lazima utengeneze tatizo kwanza kisha ufumbuzi wake upatikane!
 
Wewe ndio unahuo uusemao na sio hao waliomkaribisha mwalimu na inaonyesha waliokaribisha Mwalimu walikuwa na dhamira ya kuikomboa Tanganyika kutoka kwenye makucha ya wakoloni. Lakani Mwalimu alipata kunena Source kitabu kinaitwa Kwaheri ukoloni, kwaheri uhuru kitafute ukisome kipo bure mtandaoni.
Watanzania tuna sifa kubwa ya kupenda kujisomea, na tukisoma paragraph moja tunajua yote yaliyomo kitabuni! Ndio maana wengi wanasoma hawaelewi na wanakuwa wabishi kwa wasioyajua!
 
Watanzania tuna sifa kubwa ya kupenda kujisomea, na tukisoma paragraph moja tunajua yote yaliyomo kitabuni! Ndio maana wengi wanasoma hawaelewi na wanakuwa wabishi kwa wasioyajua!

Je watanganyika-watanzania wanawajua kina Clement. Mtamila, Dr Michael Lugazia, John Rupia, Dr Vedasto Kyaruzi, Dr Luciano Tsere, Dome Budohi, Dennis Phombeah, Zuberi Mtemvu, Ali Mwinyi Tambwe, Tatu bint Mzee Mwinyijuma Mwinyikambi, Sheikh Mohamed Ramia wa Bagamoyo, Katika kitabu cha historia ya TANU. 1954 - 1977, Dar es salaam, Kivukoni Ideologcal College, 1981 kitabu hiki kimewaacha hao wote waliotajwa hapo juu na kwa ufupi imekuwa ni kama historia yake mwenyewe mwl nyerere na sio historia ya Tanu.
 
Mohamed Shossi,

..hicho ni kikundi kidogo tu cha wananchi waliokuwa DSM.

..tatizo la hivi vitabu vilivyoandikwa so far ni kwamba waandishi wake wanaongozwa na ushabiki.

..harakati za uhuru zilishika kasi ktk sehemu zote za Tanganyika.
 
View attachment KWAHERI%20UKOLONI%20KWAHERI%20UHURU%20FREE%20DOWNLOAD%20-%20HARITH%20GHASSANY[1].part3.rar
View attachment KWAHERI%20UKOLONI%20KWAHERI%20UHURU%20FREE%20DOWNLOAD%20-%20HARITH%20GHASSANY[1].part1.rar
View attachment KWAHERI%20UKOLONI%20KWAHERI%20UHURU%20FREE%20DOWNLOAD%20-%20HARITH%20GHASSANY[1].part2.rar

wewe ndio unahuo uusemao na sio hao waliomkaribisha mwalimu na inaonyesha waliokaribisha mwalimu walikuwa na dhamira ya kuikomboa tanganyika kutoka kwenye makucha ya wakoloni. Lakani mwalimu alipata kunena source kitabu kinaitwa kwaheri ukoloni, kwaheri uhuru kitafute ukisome kipo bure mtandaoni.

kwaheri ukoloni kwaheri uhuru
 
Ndio maana kulikuwa na Paul Rupia na Kasela Bantu, hawa ndio waliosahaulika kwenye historia tukufu na sio waislamu peke yao mfano rupia alijitolea kwa hali na mali kwa ajili ya chama wakati wa harakati za uhuru, baadae mwanzo wa miaka ya 1961 kulikuwa na kina Oscar Kambona historia ya huyu "mkristo" mwanaharakati wa uhuru imefinyangwa pia. Ndugu zetu wakristo tunahitaji historia ya kweli kwa ajili ya vizazi vijavyo hakuna swala la udini hapa.

Dear Shossi,

safi sana kwa kazi nzuri hii ya kuelimisha jamii, niko pamoja na wewe !!! NAPENDA UKWELI KWA GHARAMA YOYOTE ILE! Nyerere was another criminal sawa kabisa na waislamu waliofanya mkutano juzi na kutoa matamko ya kijinga kabisa

ukitaka ku-mdescribe Nyerere basi ndio alieleta haya yote tunayoyapinga leo! Nyerere is facing charges of violating human rights! claiming that his ideas was best compared to others was absurd!

However, in other side many Muslims today are suffering from inferiority complex, they dont try to redeem themselves from the problems.They are doing nothing at all to make their lives and their generation worth!!

I believe you (thread starter) you have good intention to discuss this matter, you want truth! recently, these kinds of dicussion have been common with a diverse purposes.

PLease while these discussions are progressing all muslim activist/educated kindly educate other muslims about the reality of this life, It is pity to see muslims (majority) are waiting to get something from the main gate of Bakhresa, it is sad to see many muslims schools are not performing good, it is sad indeed that all these things are being defended by pointing fingers to Nyerere!!! so sad!!

Nyerere has done more than harm in this little country, however, we should fight as a champions and progress like winners!
 
Nafikiri kutakuwa na umuhimu pia, wa kuorodhesha mashujaa wetu wote waliopigana vita ya Uganda 1978/79, badala ya kuwajua akina Mayunga, Twalipo na wengine wachache.
 
Nafikiri kutakuwa na umuhimu pia, wa kuorodhesha mashujaa wetu wote waliopigana vita ya Uganda 1978/79, badala ya kuwajua akina Mayunga, Twalipo na wengine wachache.
Baba zetu mpaka leo viziwi kwa mizinga
 
nami nikupongeze Mkuu kwa kuiweka hoja barazani hata kama wanaochangia wanaingiza dhana ya udini lakini ujumbe unafika. wazo ninalolipata katika maelezo yako la msingi ni juu ya historia ya nchi yetu, je inavyofundishwa na kuelezwa ndivyo ilivyo kweli?
nadhani tunalazimika kuelewa pia mazingira yaliyokuwepo wakati nchi zetu hizi za kiafrika zinapata uhuru. vita baridi baina ya mashariki na magharibi viliathri sana uhifadhi wa taarifa sahihi za matukio yaliyoambatana na uhuru wa nchi zetu.
ukiacha suala la Tanganyika hata zanzibar bado historia inaacha maswali mengi yasiyo na majibu? kwa mfano kwa nini historia ya zanzibar haimtaji John Okelo? je ni kweli kwamba Karume ndiye aliyeendesha na kufanikisha mapinduzi ya kumng'oa sultani zanziba? na vipi kuhusu mchango wa marehemu Babu?
na ukiacha nchi zetu hizi mbili vuka na kuangalia majirani, kuna maswali mengi kwa mfano Patrice Lumumba, Samora Machel na hata haya ya Rwanda na Burundi vifo vya marais je ukweli unawekwa wazi?
kwa hiyo bado tuna mengi ya kujifunza ya ndani na nje. sijui kama kweli waafrika tunao uhuru kamili au tunaongozwa bado na ukoloni mambo leo, wanayoyataka ndiyo yanakuwa.
Not yet Uhuru!!
 
Ngoja nikusanye nguvu hapa si pa kuingia kichwa kichwa, but I believe anyone is allowed to rewrite the history by writing a book with all the forgotten heroes and facts, angalizo dini zetu zibaki huko huko kwa mahekalu yetu, Tanganyika haina dini ila watanganyika wana dini zao. So dini iliyokua ya Mr. Nyerere ilikua yake sio ya nchi, dini ya Mr. Kikwete ni yake sio ya nchi. Dini yangu ni yangu si ya nyumba yangu.
 
Nafikiri kutakuwa na umuhimu pia, wa kuorodhesha mashujaa wetu wote waliopigana vita ya Uganda 1978/79, badala ya kuwajua akina Mayunga, Twalipo na wengine wachache.

Si imeandikwa ya kuwa mzee Kawawa Lsimba wa nyika" ndio shujaa wa vita vya kagera?
 
Mohamed Shossi,

..hicho ni kikundi kidogo tu cha wananchi waliokuwa DSM.

..tatizo la hivi vitabu vilivyoandikwa so far ni kwamba waandishi wake wanaongozwa na ushabiki.

..harakati za uhuru zilishika kasi ktk sehemu zote za Tanganyika.

Utakuwa umefanya jambo la mbolea ukiwataya na wa mwanza, arusha na bukoba mpaka mbeya. Ninazokiandika hapa ni kuwa kuna watu walikuwa kwenye harakati za kudai uhuru lakini historia haiwataji mahala popote hao ninaowajua na wewe ongeza wa kwako unaowajua wa mikoa mingine. Au kanusha pale lumumba sio ilipozaliwa Tanu na ni chimwaga dodoma unaruhusiwa pia!
 
Utakuwa umefanya jambo la mbolea ukiwataya na wa mwanza, arusha na bukoba mpaka mbeya. Ninazokiandika hapa ni kuwa kuna watu walikuwa kwenye harakati za kudai uhuru lakini historia haiwataji mahala popote hao ninaowajua na wewe ongeza wa kwako unaowajua wa mikoa mingine. Au kanusha pale lumumba sio ilipozaliwa Tanu na ni chimwaga dodoma unaruhusiwa pia!

jamani hawa walioongoza harakati za uhuru ni vizuri wote wakatajwa na kukumbukwa, mi sioni tatizo. hata historia ya zanzibar inafichaficha baadhi ya wanaharakati wake. but wanasiasa si miungu ni watu na wanaweza kuwa wanafiki. tusikatae kuwa kuna majin ahayatajwi sana ila pia tusibishe kuwa hatuwezi kumtaja kila aliyepigania uhuru, manake orodha yaweza kuwa ndefu kama mlima kilimamnjaro wakitajwa wote. mohamed ana hoja nyingi moja ikiwa vuguvugu lilianzia mikoa ya pwani, hilo nalo si la kubezwa, bali lapaswa kuboreshwa zaidi kuwa kuzingatia na mapambano ya mahsujaa wengine wa nchi yetu kutoka sehemu nyingine mbali na pwani kama akina mkwawa, isike, mirambo, nk

nijuavyo mie TAA ilianzishwa kama chama cha starehe na burudani na baadaye kikabadili malengo yake na kuwa ya kisiasa consequently jina likabadilika nalo kuwa TANU na lilizaliwa lummba, hapo sidhani kama panahitaji ubishi. inawezekana kuwa kujiunga kwa vijana wasomi kama mwalimu nyerere, kuliongeza chachu ya kudai uhuru na kujiamini zaidi. inaonekana hata wazee wetu wale akina sykes na wengine anaowataja mohamed walimwamini mwalimu pia na kumpisha akamate madaraka ndani ya tanu kirahisi. ni jamabo zuri kuaminiana na linaimarisha mshikamano. ila napata shida kuhusu hisia za udini zinaibukia wapi. nionavyo mimi badala ya kufikiri amambo kidinidini, ni bora tukasalia katika hoja ya msingi ya kuwatambua na kuwaenzi mashjaa wetu wote wa uhuru kadiri inavyowezekana
 
this isn good history of our country for the generation to come lakini kwa sasa watu wameacha kabisa uzalendo vitu kama hivi vilitakiwa viwe kwenye shule zetu za msingi lakini elimu imechakachuliwait is good piece of information kwa generation ya waliozaliwa kuanzia 80s

huu upuuzi niliusikia radio imman,crap!
 
nami nikupongeze Mkuu kwa kuiweka hoja barazani hata kama wanaochangia wanaingiza dhana ya udini lakini ujumbe unafika. wazo ninalolipata katika maelezo yako la msingi ni juu ya historia ya nchi yetu, je inavyofundishwa na kuelezwa ndivyo ilivyo kweli?
nadhani tunalazimika kuelewa pia mazingira yaliyokuwepo wakati nchi zetu hizi za kiafrika zinapata uhuru. vita baridi baina ya mashariki na magharibi viliathri sana uhifadhi wa taarifa sahihi za matukio yaliyoambatana na uhuru wa nchi zetu.
ukiacha suala la Tanganyika hata zanzibar bado historia inaacha maswali mengi yasiyo na majibu? kwa mfano kwa nini historia ya zanzibar haimtaji John Okelo? je ni kweli kwamba Karume ndiye aliyeendesha na kufanikisha mapinduzi ya kumng'oa sultani zanziba? na vipi kuhusu mchango wa marehemu Babu?
na ukiacha nchi zetu hizi mbili vuka na kuangalia majirani, kuna maswali mengi kwa mfano Patrice Lumumba, Samora Machel na hata haya ya Rwanda na Burundi vifo vya marais je ukweli unawekwa wazi?
kwa hiyo bado tuna mengi ya kujifunza ya ndani na nje. sijui kama kweli waafrika tunao uhuru kamili au tunaongozwa bado na ukoloni mambo leo, wanayoyataka ndiyo yanakuwa.
Not yet Uhuru!!

Shossi, mada yako ni nzuri na inalenga kujua ukweli, umekataa kuendelea na historia iliyochakachuliwa kwa kaslahi binafsi!! Upande wangu mimi naona haya hayatufai kwa sasa; kwani tuna jukumu zito la kuhakikisha nchi inakombolewa toka makucha ya watu kama Iddi Amin!! Hakiak CCM na JK nikama nduli Iddi Amini.

Tuache ku-divert attention, chuma kimeshika mtoto, waTZ wotre sassa priority ni kudai katiba mpya. Haya naona watu wanahamisha hamasa kwenye mjadala ambao muafaka haupo; tutaWEZA KUREKEBISHA HISTORIA YA NCHI HII PALE NDULI iDDI aMINI TAKAPOKUWA NJE YA MADARAKA. hIVYO SHIME WOTE, TUMUONDOE HUYU PAKA SHUME KWA USTAWI WA NCHI YETU,:amen:
 
Pia tuache kudanganyana kwamba "Kwa heri ukoloni, kwa heri uhuru" ndiyo historia halisia. Naona kitabu nacho kimeegemea zaidi hearsay na utakasaji wa madhambi ya Waarabu kote bara na visiwani.
 
Back
Top Bottom