BISMILLAAHIR-RAHMAANIR-RAHIYM.
Imesemwa kuwa AMANA BANK ni Bank inayofuata sheria za Kiislamu. Katika sheria hizo kuna MLANGO wa biashara na fedha. Masuala ya njia za kuuza na kunua, vipomo, reahani (Bond) zawadi, ushirika, umiliki n.k yameelezwa katika kipengele hicho.
Katika kupitia kwangu baadhi ya Links nimeona kitu kikubwa kinachobishaniwa ni riba. Baadhi ya wachangiaji wanadhani kwamba Bank haziwezi kufanya kazi bila ya Riba!
Kwanza ni vizuri kuijuwa Riba Katika mtazamo wa Uislamu.
RIBA ni ziada ya mali inayoongezwa zaidi ya mali iliyokopeshwa. Mfano leo mtu anakopesha kilo moja au debe moja au shilingi mia moja lakini akataka mlipaji akija kulipa alipe zaiadi ya kilo moja, debe moja au shilingi mia moja. Na kuna baadhi ya watu kila unapochelewa kulipa wanaongeza kiwango cha riba (interest). Mfano anakopesha leo 100,000/= (laki moja kwa mwezi mmoja atataka riba ya asilimia ishirini (20%) na kama utachelewa kulipa inakuwa katika mtindo huu:
Mwezi wa 1 100,000 + 20% = 120,000
Mwezi wa 2 120,000 + 20% = 144,000
Mwezi wa 3 144,000 + 20% = 172,000 na kuendelea
Hapa utanona kuwa anayefaidika ni mkopeshaji na mkopaji ndiye anayenyonywa.
Tukumbuke kuwa Mtu hakopi ila kwa kubanwa na shida. Katika IMANI zetu na kanuni za Muumba inatakiwa kwamba mwnye nacho amsaidie asiye nacho ili DUNIA iwe sehemu bora ya kuishi kwa watu wote. Kwa kanuni hiyo tulitegemea kuwa Matajiri/Benki/Saccos/Viccoba n.k zisaidie kuwatoa watu katika udhalili kwa kuwakopesha MITAJI/BIDHAA bila ya RIBA. Kama tunjuavyo kuwa DINI zote zinakataza riba.
Katika uislamu kunaruhusiwa Biashara/Huduma.
Tuchukue mfano wa mkopo wa laki moja (100,000/=). Unapokwenda kutaka mkopo katika Bank za kiislamu watakuuliza unahitaji mkopo wa kufanya kitu gani. Wao wana mikopo tofauti. Mfano:
1. Biashara.
2. Ujenzi.
3. Masomo n.k
Kila mkopo una kanuni na taratibu zake. Kama ni biashara katika mkopo wa 100,000/= Bank wanaweza kukubaliana na wewe wakununulie bidhaa unazohitaji, halafu wanakuuzia kwa mkopo wakiwa wameweka faida yao, mfano 20%. mtakapokubaliana muda wa kurudisha mkopo huo yaani 120,000/= hakuna ziada ya malipo hata kama utachelewa kulipa ilimradi unawasiliana na bank na kuwapa taarifa ni kwa vipi unachelewa kurudisha mkopo waliokupa, ukitilia maanani kuwa wana dhamana yako uliyoweka kama 'BOND'
Na ujenzi ni mfano kama huo. Katika masomo na mfano wake kuna mikopo inaitwa KARDHATUN HASANAH (mkopo mwema) huu unakopeshwa bila ya ziada yoyote juu yake na inakuwa kwa kipindi maalum pamoja na dhamana (Bond)
Vilevile kuna bidhaa kama za USHIRIKA WA KIBIASHARA, UDHAMINI na huduma zote halali zinazoingiza faida.
Hii ni kusema kwamba kuendesha Bank/Saccos/Vicoba inawezekana kama tukiweka mbali UFISADI.
Imesemwa kuwa AMANA BANK ni Bank inayofuata sheria za Kiislamu. Katika sheria hizo kuna MLANGO wa biashara na fedha. Masuala ya njia za kuuza na kunua, vipomo, reahani (Bond) zawadi, ushirika, umiliki n.k yameelezwa katika kipengele hicho.
Katika kupitia kwangu baadhi ya Links nimeona kitu kikubwa kinachobishaniwa ni riba. Baadhi ya wachangiaji wanadhani kwamba Bank haziwezi kufanya kazi bila ya Riba!
Kwanza ni vizuri kuijuwa Riba Katika mtazamo wa Uislamu.
RIBA ni ziada ya mali inayoongezwa zaidi ya mali iliyokopeshwa. Mfano leo mtu anakopesha kilo moja au debe moja au shilingi mia moja lakini akataka mlipaji akija kulipa alipe zaiadi ya kilo moja, debe moja au shilingi mia moja. Na kuna baadhi ya watu kila unapochelewa kulipa wanaongeza kiwango cha riba (interest). Mfano anakopesha leo 100,000/= (laki moja kwa mwezi mmoja atataka riba ya asilimia ishirini (20%) na kama utachelewa kulipa inakuwa katika mtindo huu:
Mwezi wa 1 100,000 + 20% = 120,000
Mwezi wa 2 120,000 + 20% = 144,000
Mwezi wa 3 144,000 + 20% = 172,000 na kuendelea
Hapa utanona kuwa anayefaidika ni mkopeshaji na mkopaji ndiye anayenyonywa.
Tukumbuke kuwa Mtu hakopi ila kwa kubanwa na shida. Katika IMANI zetu na kanuni za Muumba inatakiwa kwamba mwnye nacho amsaidie asiye nacho ili DUNIA iwe sehemu bora ya kuishi kwa watu wote. Kwa kanuni hiyo tulitegemea kuwa Matajiri/Benki/Saccos/Viccoba n.k zisaidie kuwatoa watu katika udhalili kwa kuwakopesha MITAJI/BIDHAA bila ya RIBA. Kama tunjuavyo kuwa DINI zote zinakataza riba.
Katika uislamu kunaruhusiwa Biashara/Huduma.
Tuchukue mfano wa mkopo wa laki moja (100,000/=). Unapokwenda kutaka mkopo katika Bank za kiislamu watakuuliza unahitaji mkopo wa kufanya kitu gani. Wao wana mikopo tofauti. Mfano:
1. Biashara.
2. Ujenzi.
3. Masomo n.k
Kila mkopo una kanuni na taratibu zake. Kama ni biashara katika mkopo wa 100,000/= Bank wanaweza kukubaliana na wewe wakununulie bidhaa unazohitaji, halafu wanakuuzia kwa mkopo wakiwa wameweka faida yao, mfano 20%. mtakapokubaliana muda wa kurudisha mkopo huo yaani 120,000/= hakuna ziada ya malipo hata kama utachelewa kulipa ilimradi unawasiliana na bank na kuwapa taarifa ni kwa vipi unachelewa kurudisha mkopo waliokupa, ukitilia maanani kuwa wana dhamana yako uliyoweka kama 'BOND'
Na ujenzi ni mfano kama huo. Katika masomo na mfano wake kuna mikopo inaitwa KARDHATUN HASANAH (mkopo mwema) huu unakopeshwa bila ya ziada yoyote juu yake na inakuwa kwa kipindi maalum pamoja na dhamana (Bond)
Vilevile kuna bidhaa kama za USHIRIKA WA KIBIASHARA, UDHAMINI na huduma zote halali zinazoingiza faida.
Hii ni kusema kwamba kuendesha Bank/Saccos/Vicoba inawezekana kama tukiweka mbali UFISADI.