MNYISANZU
JF-Expert Member
- Oct 21, 2011
- 7,048
- 1,102
Warning: No facts,no right to contribute ! Edward Lowassa alipoenda UDSM pamoja na JK kwenye maadhimisho ya miaka 50 ya UDSM wanafunzi wa UDSM walimzomea sana JK na pia walimwonyesha mabango yenye ujumbe kuhusu madai yao mbalimbali. Lowassa hakuzomewa hata kidogo licha ya baadhi ya watu ikiwemo some members wa JF kudai ni fisadi. Cha kushangaza wakati Lowassa anatoka kwenye ukumbi wa Nkrumah wanafunzi hao wa UDSM a.k.a The home of intellectuals walimshangilia sana Lowassa na hata kufikia hatua ya kumwomba awasaidie ktk kutatua kero zao. Swali linalokuja hapa ni je kwanini EL alishangiliwa? na je hii inaleta picha gani kwa jamii ya Kitanzania? na je hawa wasomi ni mazuzu na hawaelewi kitu? je wapo kwenye pay roll ya Lowassa?. Tukio lingine ni pale alipokuwa anaelekea Mwanza kwenye harambee ya kanisa katoliki. Lowassa alipofika Shinyanga wakazi wa kule waliuzuia msafara wake na kutaka kuongea nae japo kidogo. Wakazi wa eneo husika walifikia hadi hatua ya kutaka kulisukuma gari lake! ila jamaa kwa busara zake aliwasihi wananchi wauache msafara wake uendelee kwani alikuwa na haraka na safari yake. maswali mengi sana yanazaliwa hapa lakini kuu zaidi ni je kwanini Lowassa anakubalika sana kanda ya ziwa[ evidence zinazothibitisha hili zipo]. Na pia kwanini huyu jamaa anakubalika sana miongoni mwa viongozi wa dini na wafuasi wao? Na je ni upi umuhimu wa kanda ya ziwa katika kuamua rais awe nani katika uchaguzi mkuu? Matukio ni mengi yanayoonyesha kukubalika kwa huyu mtu anayeitwa na Nape na pia baadhi ya members wa JF kuwa ni fisadi. Facts only is required here, kama huna point soma tu na upite zako.