Crocodiletooth
JF-Expert Member
- Oct 28, 2012
- 18,804
- 21,245
Huyo unayembeza ndiye kiongozi aliyefanya kazi kubwa mno kuunganisha nchi,japo yule mwizi alikuwa anapunguza unene wa barabara ili ajinufaishe huku akitengeneza mabarabara yanayo bonyea hovyo,ache JK Apumue ale bata zake tartiibu.Kama hujui unasema sijui. Mwizi ni yule anayekimbilia kumnawilia mwenzake wakati aliiba hadi twiga kapandisha ndege. Fedha za viroba, Richmond, Epa, Kagoda, China, akaweka na waziri asiyesoma kuwa waziri wa elimu, elimu ikafa, hadi baraza la mawaziri likvunjwa kwa maana pm alijiuzuru ili kumlinda yeye. Fedha zote hizi ni ufisadi na wizi wa hadharani. Alikopa mikopo isiyojulikana ni ya nini na ilifanya nini. Nchi ilikuwa inachuzwa kama peremende. Nani asiyejua? Acheni dhambi za kuficha uharifu kwa sababu ya partialities.