Je, Raila Odinga atamsaidia kampeni John Pombe Magufuli?

Bobuk

JF-Expert Member
Oct 8, 2010
5,870
3,270
Raila Odinga aliyekuwa Waziri Mkuu katika Serikali ya Kenya ni rafiki mkubwa wa John Pombe Magufuli.

Wakati wa kampeni za uchaguzi nchini Kenya, wakati huo Raila Odinga akiwania urais wa Kenya kwa Muungano wa ODM, John Pombe Magufuli alikwenda nchini Kenya na kupanda majukwaani kumnadi mgombea wa ODM, Bwana Raila Odinga.

Alipoulizwa John Pombe Magufuli kama yeye akiwa waziri wa SMT, nchi jirani kabisa na Kenya kwenda kumnadi mgombea wa chama kimojawapo nchini Kenya, sio kwanza kuifarakanisha Kenya na Tanzania, lakini pia kuingilia mambo ya ndani ya nchi nyingine?

John Pombe Magufuli alikiri kwenda Kenya na kumfanyia kampeni rafiki yake Raila Odinga. Lakini John Pombe Magufuli alijitetea kwamba alikwenda Kenya kama Pombe Magufuli na wala sio kama Waziri wa SMT.

Baada ya uchaguzi mkuu wa Kenya Bwn. Raila Odinga alishindwa na mgombea wa Jubilee Bwn Uhuru Kenyatta ambaye sasa ndiye Rais wa Jamhuri ya Kenya. Huku Bwn Raila Odinga wa ODM akiwa Kiongozi Mkuu wa Upinzani Kenya.

Swala la kujiuliza, Je Bwn Raila Odinga atakuja naye kumpigia kampeni mgombea wa CCM ambaye ni rafiki yake wa siku nyingi bwana John Pombe Magufuli?

Kama John Pombe Magufuli na Raila Odinga wana mambo ya kufanana, Je hiyo ni ishara pia kwamba John Pombe Magufuli naye atashindwa na Lowassa mgombea aliyetoka chama tawala na kuhamia upinzani i.e. muungano/ushirikiano wa UKAWA?

Kumbuka Uhuru Kenyetta akiwa mgombea wa Jubilee alimuangusha Raila Odinga aliyekuwa waziri mkuu kwenye serikali iliyokuwa inamaliza mda wake.

Historia ya John Pombe Magufuli inakwenda kuandikwa kama ilivyokuwa historia ya rafiki yake mkubwa Bwn Raila Odinga wa Kenya.
 
Maskini Magufuli akishindwa kupata urais muda huu ndio basi tena, maana bahati ya kuokota dodo kwenye mnazi haijagi mara mbili
 
Unauliza maswali halafu unahitimisha wewe mwenyewe kwa kuyajibu maswali yako!

Hoja zako haziendani na unachotaka kukijengea hoja achilia mbali mazingira ya kisiasa kati ya Tanzania na Kenya.

Hatuwezi kwa sasa kufahamu kama Raila Odinga atakuja kupiga kampeni na ukitaka kufahamu zaidi, jaribu kutafuta mahojiano ya Raila Odinga na kituo cha Azam TV kuhusu Magufuli.

Kwa kukusaidia ndondoo, Kama ni suala la Uwaziri, hata Uhuru Kenyatta alikuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri katika wizara mbali mbali lakini kikubwa zaidi, hakutoka kwenye chama tawala.

Unasahau Uhuru Kenyatta alishawahi kugalagazwa kwenye Uchaguzi Mkuu!

Unasahau Uhuru Kenyatta alishawahi kuongoza wananchi katika kuipinga Katiba Mpya wakati Lowassa alishawahi kuongoza wananchi katika kuipitisha Katiba Inayopendekezwa.

Unasahau Lowassa alishawahi kujiudhuru Uwaziri Mkuu kwa sababu ya rushwa na utumiaji mbaya wa madaraka ya Waziri Mkuu. Sijawahi kusikia kuhusu Uhuru Kenyatta.
 
Raila Odinga aliyekuwa Waziri Mkuu katika Serikali ya Kenya ni rafiki mkubwa wa John Pombe Magufuli.

ngoja niweke hesabu

MAGUFULI NI RAFIKI YAKE RAILA ODINGA AMBAYE NI RAFIKI SANA WA BARAK OBAMA RAISI WA MAREKANI

Kwa hiyo

MAGUFULI=RAILA ODINGA=BARAK OBAMA

Kwa hiyo RAISI OBAMA ni rafiki yake Raila odinga ambaye ni rafiki yake Magufuli.

Kwa hiyo Magufuli ni rafiki yake Obama ambaye ni rafiki yake Raila.

Hesabu ukizujua raha sana.Na marafiki huwa hawatupatani kwenye shida na raha
 
[QUOTE=YEHODAYA;ngoja niweke hesabu

MAGUFULI NI RAFIKI YAKE RAILA ODINGA AMBAYE NI RAFIKI SANA WA BARAK OBAMA RAISI WA MAREKANI

Kwa hiyo

MAGUFULI=RAILA ODINGA=BARAK OBAMA

Kwa hiyo RAISI OBAMA ni rafiki yake Raila odinga ambaye ni rafiki yake Magufuli.

Kwa hiyo Magufuli ni rafiki yake Obama ambaye ni rafiki yake Raila.

Hesabu ukizujua raha sana.Na marafiki huwa hawatupatani kwenye shida na raha

kwahiyo apo unataka kuzungumzia nn kwenye izo hesabu zako
 
ngoja niweke hesabu

MAGUFULI NI RAFIKI YAKE RAILA ODINGA AMBAYE NI RAFIKI SANA WA BARAK OBAMA RAISI WA MAREKANI

Kwa hiyo

MAGUFULI=RAILA ODINGA=BARAK OBAMA

Kwa hiyo RAISI OBAMA ni rafiki yake Raila odinga ambaye ni rafiki yake Magufuli.

Kwa hiyo Magufuli ni rafiki yake Obama ambaye ni rafiki yake Raila.

Hesabu ukizujua raha sana.Na marafiki huwa hawatupatani kwenye shida na raha

Kwa hiyo unataka kusema Magufuli akipita na Sheria ya Ushoga itapitishwa?
 
Hicho ndicho kitu pekee cha maana ulichoona cha kuuliza? Ushoga hata marekani haujawahi pitishwa na Obama bunge ndilo lilipitisha
Magufuli ha ha ha rafiki wa Obama,ushoga unanukia.Angalau Kenyatta kakataa live.Huyu Magufuli sijui kama atamkatalia swaiba ake
 
Back
Top Bottom