Je, ni kweli utumwa ulitwaa mbegu bora ya waafrika?

Papa D

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
753
182
Bara la Afrika limekuwa likikumbwa na matatizo yanayofanana mfano: angalia Uchaguzi wa Tanzania, Ivory coast, Zimbabwe, Kenya, Sudan na kwingine. imefika wakati baadhi ya watu wanajiaminisha kwamba hali hii inatokea kwa sababu Waafrika wenye akili, nguvu na mawazo ya kimapinduzi walichukuliwa utumwani. waliobaki walikuwa waoga na wenye uwezo mdogo kiakili na wachache wenye vinasaba vya akili walobaki wanaonekana mbele ya Wenzeo kama Waleta vurugu, wagomvi na vibaraka wa wazungu. Je, kuna ukweli wowote katika hili? kama kuna ukweli, tufanyeje? kama hakuna ukweli je, mfumo mbovu wa maisha tulonao ni stahiki yetu?
 
Kwi kwi kwi..

huenda ni kweli bana..kwa wale mlosoma vitabu vya Oral tradition vya wayahaudi mnakumbuka story ya Yusufu ? alionesha potential kubwa kaka zake wakamuonea kijicho wakamuuza utumwani. Don't quote me, i am not a source.
 
Nimelazimika kuuliza hili swali kwani nimechunguza tabia za watu mbalimbali hapa Bongo hasa wale wanaojiita Matajiri na Wasomi nikaona wengi wao ni Wakwamishaji wala si wajenzi!!!! hebu angalia mfano Ngereja, Prof. Peter Msola, Prof. Juma Kapuya! Jk na wengine wengi! halafu angalia mtu kama Lipumba, Slaa, Sitta, Kilango, Malecela, Warioba, Dr. Salmin na Selelii jinsi wanavyoshambuliwa! na Kupingwa!
 
Utumwa ulichukua zaidi labour force. Wanaume wengi wenye maumbo makubwa na nguvu walichukuliwa kwenda utumwani. Angalia Mabondia na Wachezaji wa Basketball wa Marekani jinsi walivyo ma-giant. Waliacha vijeba na bahati mbaya siyo ujeba wa maumbo tu bali hata ujeba wa akili.
 
Mkishindwa hamkosi kutafuta visingizio. Vita vya kwanza na vya pili vya dunia vilisababishwa na ukabila barani Ulaya. Suluhisho wakagawa nchi kwa makabila yao. Ujerumani kwa wajerumani. Ugiriki kwa wagirki n.k

Wamejenga nchi na taasisi nzuri katika kila nchi na sasa wamehamua kuungana tena.

Afrika mnalazimishana kuishi pamoja. Matokeo mnatumia muda mwingi kusuluhisha matatizo na sio kujenga nchi.
 
Utumwa ulichukua zaidi labour force. Wanaume wengi wenye maumbo makubwa na nguvu walichukuliwa kwenda utumwani. Angalia Mabondia na Wachezaji wa Basketball wa Marekani jinsi walivyo ma-giant. Waliacha vijeba na bahati mbaya siyo ujeba wa maumbo tu bali hata ujeba wa akili.

Diet ndio inayowafanya waMarekani wawe warefu. Hata wazungu waMarekani ni warefu. Ugali na maharage kila siku ni lazime udumae tu.
 
Diet ndio inayowafanya waMarekani wawe warefu. Hata wazungu waMarekani ni warefu. Ugali na maharage kila siku ni lazime udumae tu.

Zakumi my friend, diet mchango wake ni mdogo sana. Size ya Wamarekani inasababishwa kwa kiasi kikubwa na genetics. Wazungu kwa wastani ni warefu kushinda Waafrika. Na enzi za utumwa wafanyabiashara ya utumwa walichagua watu wenye miili mikubwa mikubwa wakiamini kuwa hao ndo wanaweza zaidi shuruba ya kazi ngumu.

Baada ya Waafrika wengi kuwa Marekani kwa mamia ya miaka, wengi wao wamechanganya sana damu na wazungu na watu wa asili nyingine na hivyo kupelekea wao kuwa na features tofauti na Waafrika walioko Afrika.

Kwa hiyo ukubwa wa miili ya Wamarekani kwa kiasi kikubwa sana inachangiwa na genetics na kwa kiasi kidogo na diet. Ila pia diet wapatayo wazazi inachangia ubora wa genes watakazomrithisha mtoto wao.
 
Zakumi my friend, diet mchango wake ni mdogo sana. Size ya Wamarekani inasababishwa kwa kiasi kikubwa na genetics. Wazungu kwa wastani ni warefu kushinda Waafrika. Na enzi za utumwa wafanyabiashara ya utumwa walichagua watu wenye miili mikubwa mikubwa wakiamini kuwa hao ndo wanaweza zaidi shuruba ya kazi ngumu.

Baada ya Waafrika wengi kuwa Marekani kwa mamia ya miaka, wengi wao wamechanganya sana damu na wazungu na watu wa asili nyingine na hivyo kupelekea wao kuwa na features tofauti na Waafrika walioko Afrika.

Kwa hiyo ukubwa wa miili ya Wamarekani kwa kiasi kikubwa sana inachangiwa na genetics na kwa kiasi kidogo na diet. Ila pia diet wapatayo wazazi inachangia ubora wa genes watakazomrithisha mtoto wao.

Aksante kwa ufafanuzi mzuri wa hoja yangu. Mungu akubariki.
 
Zakumi my friend, diet mchango wake ni mdogo sana. Size ya Wamarekani inasababishwa kwa kiasi kikubwa na genetics. Wazungu kwa wastani ni warefu kushinda Waafrika. Na enzi za utumwa wafanyabiashara ya utumwa walichagua watu wenye miili mikubwa mikubwa wakiamini kuwa hao ndo wanaweza zaidi shuruba ya kazi ngumu.

Baada ya Waafrika wengi kuwa Marekani kwa mamia ya miaka, wengi wao wamechanganya sana damu na wazungu na watu wa asili nyingine na hivyo kupelekea wao kuwa na features tofauti na Waafrika walioko Afrika.

Kwa hiyo ukubwa wa miili ya Wamarekani kwa kiasi kikubwa sana inachangiwa na genetics na kwa kiasi kidogo na diet. Ila pia diet wapatayo wazazi inachangia ubora wa genes watakazomrithisha mtoto wao.

Mkuu:

Sentensi yako ya Mwisho ina-debunk yale unayonibishia. Kwanini makabila yanayofuga ng'ombe na kula vyakula ninavyotokana na maziwa (dairy) products ni warefu kuliko wengine?

Na kuhusu kuwa wazungu walichagua watumwa hapo sio sahihi. Empire za kiAfrika kama vile za Ashante zilikamata watumwa na kuwauzia wazungu. Hivyo huwezi kusema Empire za watu dhaifu zilikamata waAfrika wenzao wenye nguvu na kuwauza utumwani.

Ukweli ni kuwa waAfrika waliochukuliwa utumwani na wale waliobaki walitoka kwenye the same genetic pool. Na watu weusi
 
Mkuu:

Sentensi yako ya Mwisho ina-debunk yale unayonibishia. Kwanini makabila yanayofuga ng'ombe na kula vyakula ninavyotokana na maziwa (dairy) products ni warefu kuliko wengine?

Hapana! Hai debunk chochote. Nilichofanya ni ku-acknowledge mchango wa genetics pamoja na diet. Na vitu hivo viwili mchango wake kwenye mwili wa mtu ni wa viwango tofauti. Genetics is always the prime determinant on how a person will look like. But diet also has a contribution in determining someone's genetics though not a significant one as you have alluded.


Na kuhusu kuwa wazungu walichagua watumwa hapo sio sahihi. Empire za kiAfrika kama vile za Ashante zilikamata watumwa na kuwauzia wazungu. Hivyo huwezi kusema Empire za watu dhaifu zilikamata waAfrika wenzao wenye nguvu na kuwauza utumwani.

Ukweli ni kuwa waAfrika waliochukuliwa utumwani na wale waliobaki walitoka kwenye the same genetic pool. Na watu weusi

Kwani ni watu wa aina gani waliokuwa wakiuzwa kwa wazungu? Mojawapo si walikuwa wale walioshindikana kuishi kistaarabu na jamii i.e. wafungwa n.k.

Na hata kama watumwa walitoka kwenye same genetic pool, wafanyabiashara ya utumwa walichagua wale waliokuwa na potential ya kuwafanyia kazi yenye manufaa. And that is a historical fact!!
 
Hapana! Hai debunk chochote. Nilichofanya ni ku-acknowledge mchango wa genetics pamoja na diet. Na vitu hivo viwili mchango wake kwenye mwili wa mtu ni wa viwango tofauti. Genetics is always the prime determinant on how a person will look like. But diet also has a contribution in determining someone's genetics though not a significant one as you have alluded.




Kwani ni watu wa aina gani waliokuwa wakiuzwa kwa wazungu? Mojawapo si walikuwa wale walioshindikana kuishi kistaarabu na jamii i.e. wafungwa n.k.

Na hata kama watumwa walitoka kwenye same genetic pool, wafanyabiashara ya utumwa walichagua wale waliokuwa na potential ya kuwafanyia kazi yenye manufaa. And that is a historical fact!!

Mkuu:

Hapa tunaweza kutoka nje ya mada bure kwa kutafuta vizingizio kwanini waAfrica Wanaboronga. Watumwa mwengi walioenda katika nchi za Marekani wametoka West Africa.

Genetically hakuna disadvantage yoyote watu wa West Africa waliyopata baada ya watu kuchukuliwa kwenda utumwani. Hivyo discrepancy yoyote hile itakuwa kwenye diet, mazingira na huduma za Afya.

Chukua mfano wa WaSenegal, WaNigeria, WaAngola, WaCameroon n.k. Nionyesheni kama watu wafupi waliachwa na kuchukuliwa warefu.

Kama mnataka historical facts. Watumwa hawakwenda Marekani pekee yake. Chukua waHaiti na Wajamaica. Urefu wa watu wa Jamaica na Haiti hauna tofauti na kaka na dada zao waliobaki West Africa.

Anyway, thread Je, ni kweli utumwa ulitwaa mbegu bora ya waafrika? . Hii ndio thesis ya thread hii. Tumia facts zako kuonyesha this is the case or not. Usiendelee kupinga hoja zangu bila kuunganisha na thesis. Usipofanya hivyo utakuwa unatafuta visingizio tu wakati Nyani Ngabu alishasema: Ndivyo Mlivyo.
 
Zakumi said:
Anyway, thread Je, ni kweli utumwa ulitwaa mbegu bora ya waafrika? . Hii ndio thesis ya thread hii. Tumia facts zako kuonyesha this is the case or
not. Usiendelee kupinga hoja zangu bila kuunganisha na thesis. Usipofanya hivyo utakuwa unatafuta visingizio tu wakati Nyani Ngabu alishasema: Ndivyo Mlivyo.

Nyani Ngabu husema "Miafrika Ndivyo Tulivyo"..hiyo ni inclusive statement kwa hiyo kama utamrejea NN basi huna budi kumrejea kwa usahihi!

Sasa tuje kwenye mada husika. Mimi nasema si kweli. Nasema si kweli kwa sababu hao descendants wa watumwa, hususan wale waliokuja kuunda mataifa na serikali zao wenyewe kiuchumi na hata kijamii hawafanyi vizuri kihivyo kuliko nchi nyingine huru za Kiafrika.

Angalia Haiti kulivyo na dhiki. Hata Jamaica na kwenyewe hakuna lolote. Kutwa kucha wanaikimbia nchi yao. Wamejazana Uingereza, Canada, New York, Florida, na kwingineko. Kwao kungekuwa kuzuri wala wasingehama.

Haya tuje Marekani, Cuba, Brasil, Colombia na kwingineko ambako watumwa walipelekwa, utaona kuwa watu wengi wenye dhiki kwenye nchi hizo ni hao hao descendants wa watumwa. Sasa wao kama ndo mbegu bora in terms of ingenuity and brilliance then I don't know what mbegu bora is.

By extension kuna weusi wengi ambao wamenufaika na utajiri wa baadhi ya hizo nchi za Americas lakini ukweli unabaki palepale kuwa wengi bado wako chini sana kwenye totem pole.

So kuna uwezekano mkubwa sana kuwa mheshimiwa NN yuko sahihi kabisa ktk kauli mbiu yake!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom