Je, mboga za majani zinazolimwa Dar zina sumu inayochangia matatizo ya nguvu za kiume, cancer, bawasiri, vidonda vya tumbo, n.k?

NetMaster

JF-Expert Member
Sep 12, 2022
1,454
4,853
Unaweza ukawa unakula ugali na mboga za majani na ukajiona unakula chakula chenye afya kumbe uhalisia ni kwamba unajiongezea sumu zaidi mwilini.

Sehemu kubwa ya mboga za Darisalama zinatoka mabonde ya Mto Msimbazi, Mandela road bonde lililoko kituo cha garage, Jangwani, Kigogo sambusa na maeneo ya Tandale na kwingineko
maji yanayopita kwenye mabonde haya ni machafu, yenye kemikali toka viwandani, yenye vinyesi toka vyooni nk ndio hayo hayo yanayotumika kumwagilia mbogamboga hizi wanazokula wakazi wengi wa jiji hili.

Kwa vyovyote vile, maji haya yakipimwa ni wazi yatakutwa na kiwango kikubwa cha sumu mbalimbali zinazoingia katika miili ya wakazi wengi wa Dar.

Uchafu unaoutupa kwenye mito ipitayo kwenye haya mabonde ni mwingi sana, mabetri ya magari na simu yenye tindikali, mizoga ya wanyama, pedi za wanawake, nk nk vyote hivi vimebeba kemikali zenye sumu kali.


Sumu hizi si ajabu ndizo huchangia matatizo kama upungufu wa nguvu za kiume, bawasiri, vidonda vya tumbo, vijana kuwahi kuota mvi, n.k.

Tusipochukua tahadhari tutaishia kuongeza vyumba pale Ocean road kwenye ile hospital ya kansa
 
Mboga za majani za Kibasila Seconday enzi hizo mwaka 2005 maji ya Sewage System ya Serengeti breweries.
 
Mumeanza Kuwakataza Chipsi Mukasema Zinapnguza Nguvu Za Kiume Mukaja Kwenye Mabroila Mukasema Wananenepesha Makalio Ya Wanaume Na Matiti Leo Munakuja na Mboga Za Majani Et Zinapnguza Nguvu Za Kiume Wallah Watu Wa Dar Mtafika Mbinguni Mumechoka 🤣🤣
 
Watu wanatiririsha Mavi ya vyoo vya Bar & Guest kwenye hio mito ni Mavi watu wanakula kwa kiwango kikubwa ndio mbolea
 
Unaweza ukawa unakula ugali na mboga za majani na ukajiona unakula chakula chenye afya kumbe uhalisia ni kwamba unajiongezea sumu zaidi mwilini.

Sehemu kubwa ya mboga za Darisalama zinatoka mabonde ya Mto Msimbazi, Mandela road bonde lililoko kituo cha garage, Jangwani, Kigogo sambusa na maeneo ya Tandale na kwingineko
maji yanayopita kwenye mabonde haya ni machafu, yenye kemikali toka viwandani, yenye vinyesi toka vyooni nk ndio hayo hayo yanayotumika kumwagilia mbogamboga hizi wanazokula wakazi wengi wa jiji hili.

Kwa vyovyote vile, maji haya yakipimwa ni wazi yatakutwa na kiwango kikubwa cha sumu mbalimbali zinazoingia katika miili ya wakazi wengi wa Dar.

Uchafu unaoutupa kwenye mito ipitayo kwenye haya mabonde ni mwingi sana, mabetri ya magari na simu yenye tindikali, mizoga ya wanyama, pedi za wanawake, nk nk vyote hivi vimebeba kemikali zenye sumu kali.


Sumu hizi si ajabu ndizo huchangia matatizo kama upungufu wa nguvu za kiume, bawasiri, vidonda vya tumbo, vijana kuwahi kuota mvi, n.k.

Tusipochukua tahadhari tutaishia kuongeza vyumba pale Ocean road kwenye ile hospital ya kansa
Nguvu za kiume ni tatizo? Bawasiri ni tatizo?
 
Hilo la kula madawa haliepukiki, sio kutoka viwandani mengine tunanunua dukani na kupuliza kwa ridhaa yetu, ushawahi ona nyanya ya Ilula inavyopulizwa dawa au tikiti kule Chanika, nikiweka picha hapa unaweza ukalia wallah, cancer haipo mbali na life yetu mkuu.
 
Tulitaka kufanyia project ya hyo kitu tukapigwa full stop na mwenyekiti wa eneo tukaachana nao ila kwa kuyaangalia tu sio Salama.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom