Je kuna umuhimu wa kupima magonjwa ya kurithi (Genotype) kabla ya kufunga ndoa?

stock-footage-hispanic-doctor-showing-x-rays-to-couple-using-laptop.jpg


Najua kwamba wengi wetu hukimbilia kupima ukimwi kabla ya kufunga ndoa na wenzi wao, lakini sijawahi kusikia wapenzi wakipima genes za magonjwa ya kurithi kipimo ambacho nadhani kinafanywa kwa kutumia DNA Test.

Nakumbuka baba yangu aliwahi kunisimuli kwamba zamani wao ilikuwa kabla ya posa kupelekwa ni lazima kila upande ujiridhishe kama familia husika ilikuwa haina magonjwa ya kurithi kama vile sickle cell, kifafa nk.

Tofauti na zamani siku hizi watu wengi wamehamia mijini kutokana na mabadiliko ya kiuchumi ambapo kuna muingiliano wa makabila. Siku hizi watu wamekuwa wakioana kwa kukutana mijini tu na hakuna hata mmoja anajua kuhusu familia ya mwenzake, hivyo watu wamekuwa kama vile wanacheza bahati nasibu.

Lakini pia mababu zetu walikuwa wakichunguza tabia mbaya zinazotembea katika familia husika inayotaka kuoa binti yao au familia kijana wao anapotaka kuoa, tabia mbaya zilizokuwa zikichunguzwa ni ulevi kupindukia, wizi, mkono wa kupiga kwa wanaume, uzinzi, ushirikina nk. Haya hayahitaji vipimo vya kitabibu, kwa sababu mara nyingi historia inahukumu.

Kwa kuwa siku hizi ni vigumu kwa baadhi ya wapenzi wanaotaka kuoana wanatoka katika makabila tofauti au mikoa tofauti, je kuna umuhimu sasa wa wanandoa kufanya vipimo vya maradhi ya kurithi (genotype) ili kuepuka kupata watoto wenye matatizo hayo?


Naomba changamoto zenu wadau:
snowhite, Paloma, Fixed Point, Kongosho, gfsonwin, Preta, DEMBA, Heaven on Earth, Lisa, Nivea, Teamo, miss chagga, miss neddy, lara 1, King'ast, AshaDii, Munkari, MankaM, mayenga, Mwita Maranya, Jiwe Linaloishi, Kiranga, Nyani Ngabu, The Boss, Asprin, Arushaone, Mzee wa Rula, Filipo, Erickb52, charminglady

Am just curious Mkuu@Mtambuzi , ingekuwaje kama mama ngina enzi zile mmekolea kwenye uchumba mkaenda kupima then mkajikuta carriers wa wagonjwa fulani,vp mngeachana???
 
Yeah hata mimi naona umuhimu ni mkubwa sana lakini jaribuni kufikiria na upande wa pili je mtu akiachwa kutoka n a hilo tatizo atajisikiaje na jamii itamchukuliaje maana lazima fununu zitasambaa future yake itakuwaje huyu mtu je hatokata tamaaa akiamua kugombea uongozi huko mbele hilo tatizo halitatumika kama kete dhidi yake kupima ni kucreate migogoro zaidi yote tumwachie mungu
 
mhm! lisemwalo lipo na kama halipo liko njiani linakuja
kweli nimeamini nachukiwa sana
 
Umuhimu ni mkubwa sana ndugu..teknolojia imekua na wataalam wapo,ila vifaa hakuna.
mama akiwa mjamzito na mtoto akaonekana ana tatizo la kurithi, uwezekano wa kukorect hizo defective genes mtoto akiwa bado tumboni upo. ila sirikali inasema vifaa ni ghali sana....
SCIENCE BEHIND POLITICS.
 
[B said:

Watu wengine kwa kukurupuka hawajambo.
Hivi unawezaje kuchangia pale ambapo umebaguliwa na huhitajiwi kufanya hivyo??
Kwa taarifa yako kama hujatajwa hapo juu nilipokazia kwa rangi ya bluu na umechangia uzi huu,
Ujue umekurupuka.
Hiyo ni kwa mujibu wa Mleta hoja.
 
stock-footage-hispanic-doctor-showing-x-rays-to-couple-using-laptop.jpg


Najua kwamba wengi wetu hukimbilia kupima ukimwi kabla ya kufunga ndoa na wenzi wao, lakini sijawahi kusikia wapenzi wakipima genes za magonjwa ya kurithi kipimo ambacho nadhani kinafanywa kwa kutumia DNA Test.

Nakumbuka baba yangu aliwahi kunisimuli kwamba zamani wao ilikuwa kabla ya posa kupelekwa ni lazima kila upande ujiridhishe kama familia husika ilikuwa haina magonjwa ya kurithi kama vile sickle cell, kifafa nk.

Tofauti na zamani siku hizi watu wengi wamehamia mijini kutokana na mabadiliko ya kiuchumi ambapo kuna muingiliano wa makabila. Siku hizi watu wamekuwa wakioana kwa kukutana mijini tu na hakuna hata mmoja anajua kuhusu familia ya mwenzake, hivyo watu wamekuwa kama vile wanacheza bahati nasibu.

Lakini pia mababu zetu walikuwa wakichunguza tabia mbaya zinazotembea katika familia husika inayotaka kuoa binti yao au familia kijana wao anapotaka kuoa, tabia mbaya zilizokuwa zikichunguzwa ni ulevi kupindukia, wizi, mkono wa kupiga kwa wanaume, uzinzi, ushirikina nk. Haya hayahitaji vipimo vya kitabibu, kwa sababu mara nyingi historia inahukumu.

Kwa kuwa siku hizi ni vigumu kwa baadhi ya wapenzi wanaotaka kuoana wanatoka katika makabila tofauti au mikoa tofauti, je kuna umuhimu sasa wa wanandoa kufanya vipimo vya maradhi ya kurithi (genotype) ili kuepuka kupata watoto wenye matatizo hayo?


Naomba changamoto zenu wadau:
snowhite, Paloma, Fixed Point, Kongosho, gfsonwin, Preta, DEMBA, Heaven on Earth, Lisa, Nivea, Teamo, miss chagga, miss neddy, lara 1, King'ast, AshaDii, Munkari, MankaM, mayenga, Mwita Maranya, Jiwe Linaloishi, Kiranga, Nyani Ngabu, The Boss, Asprin, Arushaone, Mzee wa Rula, Filipo, Erickb52, charminglady
genotype diseases #genetic diseases.
 
Am just curious Mkuu@Mtambuzi , ingekuwaje kama mama ngina enzi zile mmekolea kwenye uchumba mkaenda kupima then mkajikuta carriers wa wagonjwa fulani,vp mngeachana???
Ha ha ha ha aaaa Mimi nilioa kizamani aisee, nilipomuona mama Ngina kwa mara ya kwanza nilimweleza baba yangu akaniambia nimpe muda atanijibu. Kwa kuwa mama ngina kwao ni kijiji cha jirani na kwa bahati nzuri baba anaye rafiki katika kijiji hicho alifanya safari na kwenda kufanya uchunguzi akisaidiwa na rafiki yake na alipojiridhisha kwamba familia hiyo haina matatizo ya aina yoyote ukiwemo ulozi akanipa taarifa na posa ikatumwa halafu tukaoana.

Kama angegundua kuna tatizo basi angeniambia na kwa kuwa hatukuwa na mahusiano wakati huo ingekuwa ni rahisi kufanya uamuzi bila kumuumiza mtu.
 
Hmm...kwa kweli hapo ni mtihani maana sasa mtu sijui utakomea wapi katika kuchunguza.

Wengine akina sisi ambao ni wachunguzi kupita kiasi twaweza kumwona kila mtu ana kasoro (jambo ambalo ni kweli kwa sababu ni vigumu sana kwa binadamu yeyote yule kuwa timilifu) kama tukianza kuangalia familia nzima na si mhusika tu.

Kuchunguza kwingi kwaweza kukufanya ukose kabisa kwa kusita sita baada ya kuona kasoro. Kasoro haziwezi kukosekana na si zote ambazo zinaweza kugundulika. Kimbembe hapo.

Kama wasemavyo Wazungu, he who hesitates is lost!

Daahh siku ingine unaandika kama sio wewe vile
 
Mh mbona hata sijui....embu ninong'oneze nami nijue

chocolate nzuri bana! inaongeza stimulation,, eenh! stimulation za kufanya pepa! hahahaaa!!

matured people understand fast..!
 
[/COLOR]Watu wengine kwa kukurupuka hawajambo.
Hivi unawezaje kuchangia pale ambapo umebaguliwa na huhitajiwi kufanya hivyo??
Kwa taarifa yako kama hujatajwa hapo juu nilipokazia kwa rangi ya bluu na umechangia uzi huu,
Ujue umekurupuka.
Hiyo ni kwa mujibu wa Mleta hoja.

mzee Mtambuzi.. ile listi ya wana JF mizigo a.k.a haulage a.k.a goods iko wapi?
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli kuna ugumu sana kuachana, lakini mnaweza amua msizae labda.

Yaani mtoto chini ya miaka 5, akiwa na sickle cell ni kazi sana kumlea. Kwanza anapewa dawa za kunywa karibu kila siku. Ona tu watu wazima wanaotumia ARVs wanavyolalamikia hii kudwa kila siku.

Bado kulazwa mara kwa mara na drip za damu, kwa kweli mie labda napenda sana watoto. Dhamira yangu haiwezi kubeba hili, nilijua kuwa kabisa mwanangu anaweza pata tatizo afu nikapuuzia, it will kill me.

Many of us emotions drive our hearts and minds, cdhani kama leo hii just assuming Kongosho umeenda kupima then u find yule zombie wako ambaye amekuwa husband material(quoting frm a post) na wewe ni carriers wa ugonjwa fulani, i dont think kama it will stop u from getting married..,recently tumekuwa victims sana and its all because of the notion Love conquers all
 
Bora wewe hijachangia

[/COLOR]Watu wengine kwa kukurupuka hawajambo.
Hivi unawezaje kuchangia pale ambapo umebaguliwa na huhitajiwi kufanya hivyo??
Kwa taarifa yako kama hujatajwa hapo juu nilipokazia kwa rangi ya bluu na umechangia uzi huu,
Ujue umekurupuka.
Hiyo ni kwa mujibu wa Mleta hoja.
 
Kuna watoto wanateseka na sickle cell, albanism kwa ukaidi wa wazazi tu.
Hata kama mmependana lakini kuna umuhimu wa kufikiria kama mnahitaji kuwa na watoto, kama ndio bora msioane, kama watoto si lazima oaneni.

Ya nini uzae mtoto anayeteseka wakati ungeweza kuzuia? Kuna mtu namfahamu walipima na kuambiwa ni sickle cell carriers, still wakaoana na watoto wamezaa. Sasa mtoto mmoja kila siku kalazwa, anatia huruma kama nini, na bado mdogo sana.

tatzo watu wanapima ila hawapo tayari kufanya maamuzi magumu.
 
Baba yangu kuna umuhimu huo lakini ninahisi bado itapingwa kwani niionavyo ni njia ya kizungu tu ya kutafutiana wake. Haina tofauti na ile iliyokuwa inafanywa na wazazi sema tu kwa kuwa hii ina jina lenye kutelezesha ulimi na unaweza kuligoogle hahahaha.................. Hebu nambie wewe vijana wa kisasa wenye kupenda mademu wakali wa matawi, kampata mwenye ukali wote, pesa n.k umwambie usimuoe kwa kuwa huyo Jenotipe kasema mkeo ana genes za kisukari? Si atakwambia dawa si zipo?

.....hahhahh.... #Soulmate unakumbuka mdada na kifafa cha meno na mkaka anaugulia "wehhh!? acha....!" ???

Naaam, dawa zipo bana..... Kiapo cha 'For better or worse' kinahusu hapa ;)


#MosQw !to.
 
Back
Top Bottom