sengobad
JF-Expert Member
- Aug 13, 2017
- 8,086
- 7,456
TTCL, UDART hata wakifa hauwezi kulinganisha na TanescoIpo TTCL UDART laiti TTCL ingekuwa peke yake sokoni mvua ikinyesha kungekua hakuna mawasiliano
TTCL, UDART hata wakifa hauwezi kulinganisha na TanescoIpo TTCL UDART laiti TTCL ingekuwa peke yake sokoni mvua ikinyesha kungekua hakuna mawasiliano
Sio kweli kuwa marekani kuna vyama 2 vya siasa vipo zaidi ya 50 sema hauwezi kuvisikia ni kama chama cha Dovutwa nk, kuna Green Party, Libertarians, Constitution Party and Natural Law Party.Shida kubwa sio shirika,bali nidhamu katika mtiririko wa kimajukumu.
Nchi hii mwanasiasa ana maamuzi kuliko mtaalamu.
Nchi hii pia,hata uwe na PhD ya kitu flani
Lakini amini usiamini std 7,4m4 mwenye cheti Cha veta aliyepenya kwenye siasa na kumpata cheo ndo huyo huyo atakaetaka mawazo yake yafanyiwe kazi na sio utaalamu.
Mpangilio huo hakuna wa kulaumiwa zaidi ya Ccm inayokataa mchakato wa Katiba mpya.
Kama democrasia inafana,mbona Marekani yenye wananchi zaidi ya 200m wana vyama viwili na pia Katiba Yao ni kwamba,haijalishi unatokea malengo gani.ila ukifika White House. Unakutana na sela za Nchi,na sio sela za chama Wala za kwako binafsi.
Kwetu tumejaza vyama mfu rukuki ambavyo havina tija Kwa taifa ambavyo mnufaika ni huyu jinamizi CCM.
Viongozi wa kisiasa wamekuwa ndo wenye sauti kuliko wataalamu.
Hivyo,usikute tatizo la Tanesco linaanzia Kwa wanasiasa.
Watumishi mtawasurubisha bule,ila tatizo lipo kemwenye vyeo vya KISIASA.Na sio kwenye vyeo vya kiutendaji.
umeandika vizuri sana tena kwa kurelax aise...Sisi wengine tinaangalia zaidi vitendo kuliko hadithi.
1) Makamba alisema kuwa umeme umekuwa wa shida kwa sababu wakati wa kipindi cha awamu ya 5, hakukuwa na service ya mitambo, hivyo mitambo sasa hivi inafanyiwa matengenezo, baada ya matengenezo, mgao utakuwa historia. Je, tatizo la umeme lilikuwa historia au ni maisha ya kila siku?
2) Baadaye Makamba alisema kuwa, kuna upungufu wa maji. Tatizo la mgao litaisha mabwawa yakijaa maji. Je, tatizo la mgao wa umeme limeisha?
3) Mvua zilipoanza kunyesha, hadithi ikabadilika, ikawa tatizo la umeme linasababishwa na miundombinu, hasa nguzo kuoza. Wakasema tatizo litaisha baada ya kukamilisha ubadilishaji wa nguzo kutoka za miti na kuwa za zege. Baada ya hilo zoezi kukamilika maeneo mengi, kumekuwa na utofauti wowote?
4) Sahizi hadithi imebadilika na kuwa linasubiriwa bwawa la Nyerere, kuanzia mwezi wa pili tatizo la umeme litakwisha, tena hiyo ni kauli ya Rais. Mwezi wa pili ni wiki tu hii ijayo, wewe unaona kuna hata dalili?
Matatizo humalizwa kwa kutenda siyo kwa ngonjera za mdomoni. Kuna watu Serikalini na huko TANESCO wanataka kumaliza tatizo la umeme kwa hadithi za mdomoni!!
nafikiri ndani ya shirika kuna mazalia ya upinzani hao ndio shidaHao sio Tanesco ni CCM
Yaweza kua kweli,wafanye uchunguzi,huenda kunahujuma zinafanywa kwa makusudi kumchonganisha mama.nafikiri ndani ya shirika kuna mazalia ya upinzani hao ndio shida
Hawa Tanesco ni wapumbavu sana ni moja ya shirika la hovyo.
Huku mtaani mnaua biashara za watu kwa tabia zenu za kifala hizi.
Umeme umekuwa anasa kazi hazifanyiki, mitaji ya watu inayumba kwa mambo yenu haya ya kipuuzi.
Hawa jamaa sijui wana akili za namna gani huu umeme umekua wa kuchajia simu tu sio wa kufanyia biashara haiwezekani umeme unarudi muda wa kulala sio muda wa biashara.
Hatuwezi endelea kwa style kama hii ya hawa wajinga Tanesco.
Bila shaka watakuwa wanaandaa hadithi nyingine ya kuja kuwaambia watu huo mwezi wa pili.Pole mkuu.... Imebaki miezi miwili tuondokane na changamoto ya mgao wa umeme (kulingana na maagizo ya mama) japo sioni kama hilo linaenda kuwezekana
Nadhani hujawahi kutana na maswaibu ya Polisi wetu kaka, Tanesco wana Nafuu kubwa sanaHao Ndo mwanzo wa mdororo mkubwa wa kiuchumi hapa nchini pmj na viongozi wa serikalini......mbaya Zaidi wanatuaminisha kuwa nchi kuwa ya wachuuzi Ni bora Zaidi kuliko kuwa ya viwanda kisa wanakusanya kodi nyingi kutoka kwa wafanyabiashara
Nakubaliana Nawe kuwa hii Ni taasisi ya hovyo Sana sana
Mie tenaaa........harakati zangu zinanikutanisha Sana na hao jamaa ......unafuu wao na tanesco Ni kwamba wao hawapo moja kwa moja kwenye ukuaji au ujenzi wa uchumi wetu hivyo hawana athari kubwa kwa maendeleo yetu japo nao Ni hovyoNadhani hujawahi kutana na maswaibu ya Polisi wetu kaka, Tanesco wana Nafuu kubwa sana