Je hakuna ufisadi ndani ya TRA receipt machines?

Qualbalasad

Senior Member
Jul 14, 2011
131
41
Nimekuwa nikijiuliza sana kuhusu utoaji wa mashine ya stakabadhi/risiti kutoka TRA, Hii ikiwa ni mashine zilizoagizwa kutumika ili kukusanya kodi kwa njia bora zaidi, kwangu mimi nifikiri kuwa machine hizi zingeagizwa na kugaramikiwa na TRA kama nyenzo ya idara hii ya ukusanyaji wa kodi.

Inaonekana kuwa TRA imepanga wakala wa kuingiza mshine hizo, na kuuzwa kwa wafabishara wenye viwango vya VAT, Je huyu wakala ni nani na amepata je tenda hiyo? Je hapa hakuna 40% ya mtu wa serekalini? kwa kuwa mashine hizi hununuliwa kwa fedha taslimu, na hurudishwa katika mapato ya kodi. Je hii si ulaji wa kodi kupitia njia hii?

Nomba kuwakilisha
 
Ufisadi utakosekana vipi TRA ?

lakini si unajua TRA ni chaka la akina nani?

na DG pale si unajua ni nani?

Ingekuwa anaitwa Mohamed Athumani ungeona moto wake
 
Hakuna kitu chochote ambacho ktk nchi ambacho si biashara ya walio madarakani, kwa hakika hapo ufisadi upo ktk hili, ukifikiri kwa makini utaona kuwa cash ndio inayoitajika, ijapokua wanakubali kuwa watarejesha fedha za manunuzi kwa kupunguza ktk tozo la kodi.

Hii ni kwa kuwa wenye % zao wachukue mapema, Serikali inakopa kwa mfanyabisha kwenye vitendea kazi vya kukusanyia kodi, mbona hawakukopa ndege mbovu, wala kununua rada kwa bei halisi kwa mkopo? Unaweza kuona serikali inawabana wafanyabiashara wa ndani na sio wa nje.
 
Back
Top Bottom