Japhet Maganga wa CWT akamatwa kwa kufanya fujo

Mjanja M1

JF-Expert Member
Oct 7, 2018
3,660
12,304
KATIBU Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Japhet Maganga, na wenzake 10 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani hapa kwa tuhuma za kufanya fujo kwenye mkutano wa Baraza Kuu la chama hicho wakati wakipitisha bajeti ya mwaka.

Tukio hilo lilitokea baada ya baraza hilo kuazimia kumsimamisha kazi Maganga kutokana na kupoteza sifa baada ya kufukuzwa kazi na mwajiri wake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Martin Otieno, amethibitisha kukumatwa kwa kiongozi huyo pamoja na wenzake wakati wa mkutano huo.

“Tulipata taarifa kuwa kuna watu wanafanya fujo tukaenda kudhibiti kabla hayajatokea madhara. Kwenye mkutano huo sisi hatufahamu ilikuwaje zikatokea fujo. Ukitaka kufahamu zaidi waulizwe CWT wenyewe,” amesema Kamanda Otieno.

Source - Nipashe
 
Unajua nawe ni verified member wa JF? Sasa mbona unajifanyia hivi?
Huu ni mjadala mpana ambao tena ni wa kitaifa na bado umenajisiwa kwa muda mrefu, badala ya kuhoji ametanguliza matusi... Niambie kama Verified member hapataswi kujibu mapigo?.
 
Wewe ni mpumbavu na mjinga nashaanga hadi upo verified unaongea km mtu asiyekuwa na elimu

Wajaluo asili yao ni kenya na Tanzania hasa mkoa wa mara Tanzania na magharibi mwa kenya
Weka hoja yako vizuri nikujibu tena kwa mifano, kutanguliza matusi hainizuii kukujibu kwa matusi hata kama Niko Verified....after all verification nimeomba mwenyewe, sikulazimishwa!
 
KATIBU Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Japhet Maganga, na wenzake 10 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani hapa kwa tuhuma za kufanya fujo kwenye mkutano wa Baraza Kuu la chama hicho wakati wakipitisha bajeti ya mwaka.

Tukio hilo lilitokea baada ya baraza hilo kuazimia kumsimamisha kazi Maganga kutokana na kupoteza sifa baada ya kufukuzwa kazi na mwajiri wake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Martin Otieno, amethibitisha kukumatwa kwa kiongozi huyo pamoja na wenzake wakati wa mkutano huo.

“Tulipata taarifa kuwa kuna watu wanafanya fujo tukaenda kudhibiti kabla hayajatokea madhara. Kwenye mkutano huo sisi hatufahamu ilikuwaje zikatokea fujo. Ukitaka kufahamu zaidi waulizwe CWT wenyewe,” amesema Kamanda Otieno.

Source - Nipashe
Hatimaye Mwamba kanasa mtegoni..
Hongera kwake maana kapambana Sana..
 
Wewe ni mpumbavu na mjinga nashaanga hadi upo verified unaongea km mtu asiyekuwa na elimu

Wajaluo asili yao ni kenya na Tanzania hasa mkoa wa mara Tanzania na magharibi mwa kenya
Rubbish! Hebu toa uthibitisho wa kuwa wajaluo asili yao iko Tanzania.
 
Rubbish! Hebu toa uthibitisho wa kuwa wajaluo asili yao iko Tanzania.
Mikoa yote ya mipakani ina jamii zinazoshare majina hata makabila yao. Wamakonde wapo Msumbiji na Mtwara, Wanyasa wapo Tanzania na Malawi........kuna majina ya kihaya yapo pia Uganda ingawa wale wa kabila la kule Uganda hawaitwi Wahaya.

Wajaluo wapo wilaya ya Rorya mkoani Mara, ni mpakani na Kenya. Ni jamii moja na Wajaluo wa Kenya, ila wapo Wajaluo Watanzania wengi sana. Ukitafuta asili, hata Kenya Wajaluo si asili yao.
 
Mikoa yote ya mipakani ina jamii zinazoshare majina hata makabila yao. Wamakonde wapo Msumbiji na Mtwara, Wanyasa wapo Tanzania na Malawi........kuna majina ya kihaya yapo pia Uganda ingawa wale wa kabila la kule Uganda hawaitwi Wahaya.

Wajaluo wapo wilaya ya Rorya mkoani Mara, ni mpakani na Kenya. Ni jamii moja na Wajaluo wa Kenya, ila wapo Wajaluo Watanzania wengi sana. Ukitafuta asili, hata Kenya Wajaluo si asili yao.
Point yako imesimama kwa kunyooka. Kama hivyo ndivyo ingawa inahitaji uthibitisho wa asili ya mtu, kwa nini majina ya asili kama hayo ya kijaluo kwa watu wa mikoa ya magharibi hasa Kigoma yanatiliwa shaka na idara ya uhamiaji?
 
Back
Top Bottom