Salamu ndugu zangu wana JF,
Naomba kuanza na swali lifuatalo kuwa "Wanawake wa nchi hii watabadilika lini na wao kuwa chachu ya mabadiliko yanakuja katika nchi yetu?Nimeamua kuuliza swali hili kwa sababu karibu 90% ya wanawake wanakisupport chama cha cha Mapinduzi (CCM) wakati wao ndio wanaokumbana na matatizo kibao katika maisha haya ya kila siku.Kwa mfano tu tembelea wodi za akina mama wajawazito katika hospitali za serikali na vituo vya afya unaweza kulia kutokana na huduma mbovu wanazopata huko wanalala chini tena kwa kujibana au kujiegesha,yaani mama mjamzito mmoja analala huku mwingine akisubiri mwenzake anyanyuke na yeye aegeshe mgongo angalau naye alale (Nenda hospitali ya Mount Meru utajionea hali ilivyo mbaya mpaka utawonea huruma. huo ni mfano tu wa mambo wanayoyapitia hawa mama zetu.
Suala la huduma ya maji.Ninafahamu ya kuwa suala la kupata huduma ya maji safi ni haki ya kila mtanzania mahali popote pale alipo katika ardhi ya nchi hii na ni wajibu wa serikali kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma ya maji safi.Lakini kuna maeneo mengi katika nchi hii ambapo wanawake wanaamka alfajiri na mapema kufuata maji umbali mrefu sana pengine zaidi ya km 7 na maji yenyewe si safi kwa ajili ya matumizi ya binadamu.Kwa mfano tu kuna baadhi ya wilaya za mkoa wa Mwanza kama vile Sengerema kuna maeneo wanawake wanatembea umbali wa zaidi ya km 10 kutafuta maji na wilaya hiyo ni kiwakilishi cha maeneo mengine mengi tu ambayo wanawake wanapata dhahama hii ya kukosa maji safi.
Pia wanawake wengi ni wamama wa nyumbani kwa maana ya kwamba wanabaki nyumbani kutegemea kuhudumiwa na waume zao kwa mahitaji yao ya msingi.Kwa wengi waliopo mijini wanategemea waume zao kwaachia fedha za matumizi lakini wanapoachiwa fedha kidogo wanalalamika.
Pamoja na hayo yote na mengine mengi ambayo sijataja,wanawake ndio waa kwanza kuitetea na kuisupport CCM wakati kwa muda wote ambao CCM imekuwa mdarakani imeshindwa kutatua haya matatizo ambayo yamekuwa sugu kwa nchi hii.Tembea sehemu nyingi utaona wanawake wamevaa vilemba vya CCM pamoja na kanga.
Hivi ndugu zangu hawa mama zetu watafunguka lini na kuacha kuwatetea hawa wakoloni weusi wanaoendelea kuinyonya nchi hii? Naomba nisaidiwe kujibiwa swali langu.
Naomba kuanza na swali lifuatalo kuwa "Wanawake wa nchi hii watabadilika lini na wao kuwa chachu ya mabadiliko yanakuja katika nchi yetu?Nimeamua kuuliza swali hili kwa sababu karibu 90% ya wanawake wanakisupport chama cha cha Mapinduzi (CCM) wakati wao ndio wanaokumbana na matatizo kibao katika maisha haya ya kila siku.Kwa mfano tu tembelea wodi za akina mama wajawazito katika hospitali za serikali na vituo vya afya unaweza kulia kutokana na huduma mbovu wanazopata huko wanalala chini tena kwa kujibana au kujiegesha,yaani mama mjamzito mmoja analala huku mwingine akisubiri mwenzake anyanyuke na yeye aegeshe mgongo angalau naye alale (Nenda hospitali ya Mount Meru utajionea hali ilivyo mbaya mpaka utawonea huruma. huo ni mfano tu wa mambo wanayoyapitia hawa mama zetu.
Suala la huduma ya maji.Ninafahamu ya kuwa suala la kupata huduma ya maji safi ni haki ya kila mtanzania mahali popote pale alipo katika ardhi ya nchi hii na ni wajibu wa serikali kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma ya maji safi.Lakini kuna maeneo mengi katika nchi hii ambapo wanawake wanaamka alfajiri na mapema kufuata maji umbali mrefu sana pengine zaidi ya km 7 na maji yenyewe si safi kwa ajili ya matumizi ya binadamu.Kwa mfano tu kuna baadhi ya wilaya za mkoa wa Mwanza kama vile Sengerema kuna maeneo wanawake wanatembea umbali wa zaidi ya km 10 kutafuta maji na wilaya hiyo ni kiwakilishi cha maeneo mengine mengi tu ambayo wanawake wanapata dhahama hii ya kukosa maji safi.
Pia wanawake wengi ni wamama wa nyumbani kwa maana ya kwamba wanabaki nyumbani kutegemea kuhudumiwa na waume zao kwa mahitaji yao ya msingi.Kwa wengi waliopo mijini wanategemea waume zao kwaachia fedha za matumizi lakini wanapoachiwa fedha kidogo wanalalamika.
Pamoja na hayo yote na mengine mengi ambayo sijataja,wanawake ndio waa kwanza kuitetea na kuisupport CCM wakati kwa muda wote ambao CCM imekuwa mdarakani imeshindwa kutatua haya matatizo ambayo yamekuwa sugu kwa nchi hii.Tembea sehemu nyingi utaona wanawake wamevaa vilemba vya CCM pamoja na kanga.
Hivi ndugu zangu hawa mama zetu watafunguka lini na kuacha kuwatetea hawa wakoloni weusi wanaoendelea kuinyonya nchi hii? Naomba nisaidiwe kujibiwa swali langu.