ITIKADI ni imani; Membe amepotoka na amefanya uamuzi wa kijinga

TandaleOne

JF-Expert Member
Sep 4, 2010
1,644
709
Watu wameendelea kutoa maoni yao kuhusu uamuzi wa aliyekuwa Kada na Kiongozi mwandamizi wa Chama na Serikali, Mzee wangu Bernerd Membe kujitoa rasmi katika Chama cha Mapinduzi, nimeonelea kuwa ni jambo lenye manufaa nami nikaungana na watanzania wengine katika kutoa mtazamo wangu katika kadhia hiyo. Kwa ufupi sana.

Jambo la kwanza kubwa ni kuhusu ITIKADI, tumefundishwa na kuelewa kuwa itikadi ya Chama Cha Siasa ni imani, imani inayojengwa katika misingi, falsafa na nadharia ya namna bora na sahihi ya kuongoza watu na kuendesha nchi. Imani mahala pake ni moyoni, huko ndiko inakohifadhiwa. Aliyeamini huitwa MUUMINI na daima, katika siku zote za maisha yake muumini ataiishi, atailinda na kuifia imani yake. Uamuzi wa Mzee wangu unanirudisha katika fikra nzito nikiwaza Mzee MEMBE aliamini katika nini, je alikuwa mkweli katika imani yake..? imani iliyomlea, iliyomkuza, ikamjenga na kumuinua daraja akawa mtu katika watu.

Jambo la pili, kwa mtu wa taaluma yake, inatia mashaka juu ya ubobezi wake, upofu wa mipango yake na upoyoyo wa mikakati yake na ujinga wa maamuzi yake. Inawezekana vipi, mtu mwenye fikra zilizo sawa akapita katika njia ya waliopotea, akiwa anajua katika dhati ya moyo wake kuwa njia hiyo it's heading nowhere. Alijaribu Mrema mwaka 1995 akiwa anabebwa na makundi ya watu na watu wakisukuma gari yake, hakufanikiwa, Ameendelea kujaribu Seifu Sharif, hatofanikiwa, Alijitosa Mzee Lowasa 2015 akiungwa mkono na makundi ya Vijana na wabeba mikoba ya noti, hakufanikiwa...,how could he make it with a bunch of paid actors kijijini kwake chiponda..how..?

Mimi sio mtu wa kuyumba katika misimamo yangu, nimeiishi imani na itikadi yangu na hata ninapopambana huwa ninapambania imani ninayoiishi na si vinginevyo, sikuwahi kuwa adui wa mtu kwa kufuata mkumbo na sikuwahi kuwa rafiki wa mtu kwa kufuata mkumbo..ninapambana na yeyote kwa wakati wowote pale ninapoona MISINGI ya imani ninayoiamini inachezewa .

Kama vile tunapokuwa katika mafanikio katika carrier zetu, pale tunapopata majaribu, tuwe bold and strong enough kupambania yale tunayoamini hayako sawa katika kulinda, kujenga na kuendeleza Imani/Itikadi zetu. Mzee Membe kwa uamuzi wake amejivua hata ile heshima kidogo aliyobakiwa nayo katika jamii yake na hata kwa wale tuliomuamini na kudhani ni mtu jasiri, mwelevu na mwenye maono, amethibitisha kuwa ni mtu dhaifu, muoga, asiye na msimamo na mpotevu.

Natoa wito kwa wanachama wenzangu wa CCM na wananchi wenzangu. Tuendelee kuilinda Imani ya Chama Chetu kwa gharama yeyote.

Mpaka sasa CCM bado ni Chama bora kabisa na imani yake ni THABITI.
 
Nape Moses Nnauye wewe ni Mwanasiasa mnafiki sana! Huna unachosimamia zaidi ya tumbo lako hilo kubwa kama "jiroba".

Ulimwita Rais Magufuli mshamba kwenye liked clip ukiongea na Kinana!Baada ya kubanwa ukaomba msamaha huku kamasi zikikutoka na ukiwa umepigishwa " kwata" kuingia Ikulu mithili ya Kibaka!

Uamuzi wa Bernard Membe ni mahesabu ya mtu mwenye maarifa hata hasipopata Urais leo.

Lakini ukweli ni kwamba Membe amejijengea heshima kwa kukataa "kuabudu sanamu"!

Bernard Membe is a hero popote atakapokuwa Nape kaa ukijua hilo.
 
Nape Moses Nnauye wewe ni Mwanasiasa mnafiki sana! Huna unachosimamia zaidi ya tumbo lako hilo kubwa kama "jiroba".
Ulimwita Rais Magufuli mshamba kwenye liked clip ukiongea na Kinana!Baada ya kubanwa ukaomba msamaha huku kamasi zikikutoka na ukiwa umepigishwa " kwata" kuingia Ikulu mithili ya Kibaka!..
Kuabudu Sanamu waliyoichonga wenyewe,wakiwa kwenye mfumo huwa ni vipofu juu ya mifumo mibovu wanayoshindwa ibadili ,wakiwa nje ya mfumo akili huwa sawa
 
Kwa taarifa yako ww husimamii imani wala itikadi yoyote, unalinda mlo, na ndio maana mwanaume mzima uliishia kuomba msamaha wa kijinga, kwa kuhofia ugumu wa maisha.

Membe anajua fika kwa sasa hakuna mwanaccm anasimamia itakadi, bali wote mnasimamia mlo, na yeye hayupo kwenye mlo. Ni kipi cha kumfanya ajinyenyekeze huko ccm wakati hayuko kwenye mlo kama ww?
 
Wrong Identity, TandaleOne sio Nape.
Na hata ikiwa ni Nape, ingefaa zaidi ukajielekeza katika hoja kuliko kumjadili mtoa hoja.
Watu wajinga kama wewe Nape lazima muwekwe open watu wawajue mapema mnachosimamia! Mnasimamia matumbo yenu huku mkihadaa watu kuwa mna maarifa huku ni zero brain!

Ona huko twitter unavyojidhalilisha kwa kulamba miguu ili husitoswe kwenye Ubunge wa Mtama.
 
Kwa taarifa yako ww husimamii imani wala itikadi yoyote, unalinda mlo, na ndio maana mwanaume mzima uliishia kuomba msamaha wa kijinga, kwa kuhofia ugumu wa maisha. Membe anajua fika kwa sasa hakuna mwanaccm anasimamia itakadi, bali wote mnasimamia mlo, na yeye hayupo kwenye mlo. Ni kipi cha kumfanya ajinyenyekeze huko ccm wakati hayuko kwenye mlo kama ww?
Huu ni Ujuha.
 
Watu wajinga kama wewe Nape lazima muwekwe open watu wawajue mapema mnachosimamia!
Mnasimamia matumbo yenu huku mkihadaa watu kuwa mna maarifa huku ni zero brain !
Ona huko twitter unavyojidhalilisha kwa kulamba miguu ili husitoswe kwenye Ubunge wa Mtama.
Naomba tukujue na wewe...jiweke open basi.
 
Labda usichokifahamu kuwa Mgombea mkuu wa Chama cha Upinzani kunakuja na umaarufu mkubwa wa ndani na nje ya nchi, na hicho ndicho wanachokitafuta, anajua hawezi kushinda na kuiondoa CCM ni kama Tundu Lisu tu, attention seeking, Lowasa sasa hivi ni maarufu sana nje na ndani ya nchi sababu hiyo, ...
 
Huu ni Ujuha.

Jianaume lizima na likitambi la lishe hovyo, unaogopa maisha mpaka unaenda kumsujudia mwanaume mwenzio, saa hii unaleta post ya kibwege kujifanya unasimamia itakadi. Mpuuzi mkubwa.
 
Nape Moses Nnauye ( Tandaleone) wewe ni Mwanasiasa mnafiki sana! Huna unachosimamia zaidi ya tumbo lako hilo kubwa kama "jiroba".
Ulimwita Rais Magufuli mshamba kwenye liked clip ukiongea na Kinana!Baada ya kubanwa ukaomba msamaha huku kamasi zikikutoka na ukiwa umepigishwa " kwata" kuingia Ikulu mithili ya Kibaka!
Uamuzi wa Bernard Membe ni mahesabu ya mtu mwenye maarifa hata hasipopata Urais leo.
Lakini ukweli ni kwamba Membe amejijengea heshima kwa kukataa "kuabudu sanamu"!
Bernard Membe is a hero popote atakapokuwa Nape kaa ukijua hilo.

Siku akiwa analala na maumivu na majonzi na kujutia uamzi wake, wakati huo wewe unapamba kwa nje eti ni jasiri hawezi kunyeyekea wakati yeye anaumia.
Mlimtaja kinana ni jasiri, siku alipoomba msamaha mkaanza kumtusi,
Msubilini tu baada ya uchaguzi embe ataji less kuomba kusamehewa sasa aibu itabaki kwako.
 
Swala La member liko kiinteligensia zaidi,ukweli mchezo unaofanyika unaitwa "divide and rule" vyama pinzani kuweni na mikakati katika hili
 
Labda usichokifahamu kuwa Mgombea mkuu wa Chama cha Upinzani kunakuja na umaarufu mkubwa wa ndani na nje ya nchi, na hicho ndicho wanachokitafuta, anajua hawezi kushinda na kuiondoa CCM ni kama Tundu Lisu tu, attention seeking, Lowasa sasa hivi ni maarufu sana nje na ndani ya nchi sababu hiyo, ...

Magufuli anaweza ushindani?
 
Jianaume lizima na likitambi la lishe hovyo, unaogopa maisha mpaka unaenda kumsujudia mwanaume mwenzio, saa hii unaleta post ya kibwege kujifanya unasimamia itakadi. Mpuuzi mkubwa.
Ni itikadi sio itakadi.
 
Labda usichokifahamu kuwa Mgombea mkuu wa Chama cha Upinzani kunakuja na umaarufu mkubwa wa ndani na nje ya nchi, na hicho ndicho wanachokitafuta, anajua hawezi kushinda na kuiondoa CCM ni kama Tundu Lisu tu, attention seeking, Lowasa sasa hivi ni maarufu sana nje na ndani ya nchi sababu hiyo, ...
Usimfananishe Lissu na vitu vya kijinga bwashee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom