Mjuni Lwambo
JF-Expert Member
- Apr 25, 2012
- 9,422
- 8,877
Mkuu, sio kweli kuwa hawajui, huo kusema ni dini ya amani ni unafiki tu wazi, wamechinja mtu geita waziwazi halafu unakuja kuambia watu ni dini ya amani, you must be joking.
Mleta uzi, nadhani pa kuanzia, inatakiwa ujiulize yafuatayo:
- Kuna uovu wa wazi kabisa kama vile kuchoma makanisa, na kuua kunakofanyika na baadhi ya waislam kwa jina la uislam, Je, waislam ambao hawaamini kuwa hayo yanayofanyika ndiyo uislam wenyewe, wamefanya nini ili kujitenga nao, kama wanaona dini yao inafungamanishwa na matendo maovu?
- Kuna mafundisho ya chuki na kuhamasisha mauaji ya viongozi wa kikristo, mafundisho hayo yanafanywa na mashekhe kama akina Ilunga, Ponda na wengineo, waislam hao wanaodai kuwa uislam ni dini ya amani, wamefanya nini kuzuia, au hata kujitenga na mafundisho hayo, na kuudhihirishia umma kwa uwazi kabisa kuwa mafundisho hayo ni kinyume cha uislam nao wanayapinga?
- Viongozi wakuu wa dola, hawakuchaguliwa kwa imani zao bali kwa uwezo na kanuni zilizowekwa na Watanzania wote, lakini ni ukweli usiopingika kuwa ni waislam kwa imani zao. Kwa nini wamekuwa na kigugumizi kusimamia sheria inapotokea ni viongozi wa dini yao ndiyo wanaohamasisha uovu huo?
- Nadharia inastahili kufuatiwa na vitendo la sivyo nadharia hutupwa, na matendo yatatengeneza nadharia. Nadharia ni kuwa uislam ni dini ya amani lakini matendo yanaonesha kuwa kuna matukio mengi sana ya shari na mauaji duniani kote yanayofanywa na makundi yanayojitambulisha yenyewe kuwa ni makundi ya kiislam. Kwenye mafundisho ya uislam kuna upungufu gani hata nadharia isiwe inaendana na matendo?
- Hapa kwetu vurugu za mwanzo kabisa zilisohusisha uchomaji wa mabucha ya nguruwe, zilifanyika wakati wa utawala wa Mwinyi, na ndipo kwa mara ya kwanza tulianza kusikia mafundisho ya chuki yanayofanywa na baadhi ya mashekhe wa kiislam dhidi ya ukristo. Wakati wa Mkapa mambo hayo yalififia sana. Sasa yameibuka tena wakati wa Jakaya. Je, kuna uhusiano gani wa vurugu na mafundisho ya chuki ya viongozi wa kiislam na uongozi wa Rais muislam?