Is it true jamani...........?

MwanajamiiOne

Platinum Member
Jul 24, 2008
10,470
6,563
Hi

I hope wote tu wazima.

Eti ni kweli kuwa ndoa is an institution easy to enter but hard to get out of it?... nimeliwaza hili baada ya kuwa nashuhudia mifarakano mingi katika institution hii. Wanandoa wa jinsia zote wanalalamika juu ya kuonewa, kudharauliwa na kutendewa mambo mengi yasio faa na wenzi wao mf. kucheat, kupigwa, matusi na kashfa za kila mfano.

Kinachonishangaza mimi ni kuwa je katika karne hii ya kila mtu kuwa na haki ya kuishi kwa amani na raha mtu anakubalije anyanyaswe na binadamu mwenzie tena aliyekutana naye ukubwani akiwa na meno yake 32 bila kujua ameyapataje au yaliotaje?? inakuwaje akubali kupigwa, kudhalilishwa na kukoseshwa furaha na amani katika dunia kisa mume/mke?

Je ni kweli penzi (love) linaweza kukufanya ukubali haya toka kwa mwenzi wako? na kama ndio inakuwaje basi lielemee upande mmoja tu kwa maana ya kwamba kama mvumiliaji anafanya hivyo kwa ajili ya penzi then huyo mnyanyasaje huwa hana penzi (sijui hata kama nimeuliza sawa naona nachanganyikiwa tu!!)

Baada ya kuwaza hayo nikafikia conclusion kuwa ndoa -kwa maana ya zile halali zilizofungwa kihalali (si vimada/ hawara/buzi /ATM wala girlfriend/boyfriend) ni kitu kikubwa sana kuliko tunavyokifikiria wakati tunaingia katika institution hii. Je ni kile kiapo ndicho kinatufanya tuvumilie au?

Tafadhalini naomba mtizamo wako katika hili
 
...yote yanatokana na addiction ndugu yangu wee, addiction mbaya usiombe!!!...

ukishazoea kulala naye na kuamka naye, hata mkikoseana unaona aaarrrgghh, acha tuendelee kuumana na kupulizana, ...siku nyingine mnanuniana hata sababu hamuijui, ...siku nyingine mnakimbizana kidali po chumbani, almuradi siku hazigandi!...
 
Back
Top Bottom