Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,338
- 9,762
Mahakama Kuu Kanda ya Iringa leo imemwachia huru Maria Ngoda aliyehukumiwa miaka 22 jela kwa kosa la kukutwa na vipande 12 vya nyama ya swala Novemba 3, 2023, Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT), Jokate Mwegelo ameeleza.
Bi. Ngoda ameachiwa baada ya kushinda rufaa iliyosimamiwa na UWT.
Pia soma > Kumfunga Maria jela miaka 22 kisa nyama ya swala ni matokeo ya kuwa na wanasheria waliokosa hekima na busara
----
Ndugu zangu Watanzania,
Umoja wa wanawake wa CCM Tanzania chini ya uongozi wa Mheshimiwa mama marry chatanda kama mwenyekiti pamoja na katibu mkuu wake Mheshimiwa Jokate Mwegelo, imefanikiwa kumrejeshea tabasamu na furaha mama Maria wa Iringa ambaye alikuwa amefungwa kifungo cha muda mrefu kwa madai kuwa alikutwa na nyama ya porini kinyume na sheria.
Leo februari 16 ndio ilikuwa siku ya hukumu baada ya umoja huo wa CCM kumkatia rufaa mama huyo mnyonge na aliyehitaji msaada wa hali na mali ambapo mahakama imetoa hukumu na kumuachia huru mama huyo mnyonge aliyetetewa na chama cha Mapinduzi kinachowajali, kuwatetea na kuwasemea wanyonge.
Hii ndio sababu ya CCM kuendelea kuwa kimbilio la wanyonge na kuendelea kuungwa mkono na kupigiwa kura za ndio kwa kishindo kila uchaguzi. Sasa unafikiri ni vipi mama huyu ambaye amebubujikwa machozi ya furaha baada ya kutolewa gerezani atashindwa kuipigia kura CCM?
Ni vipi ataacha kuiunga mkono CCM? Ni vipi ndugu, jamaa, marafiki na watoto wake wataacha kuipenda CCM iliyo mtetezi wa wanyonge?
Bi. Ngoda ameachiwa baada ya kushinda rufaa iliyosimamiwa na UWT.
Pia soma > Kumfunga Maria jela miaka 22 kisa nyama ya swala ni matokeo ya kuwa na wanasheria waliokosa hekima na busara
----
Ndugu zangu Watanzania,
Umoja wa wanawake wa CCM Tanzania chini ya uongozi wa Mheshimiwa mama marry chatanda kama mwenyekiti pamoja na katibu mkuu wake Mheshimiwa Jokate Mwegelo, imefanikiwa kumrejeshea tabasamu na furaha mama Maria wa Iringa ambaye alikuwa amefungwa kifungo cha muda mrefu kwa madai kuwa alikutwa na nyama ya porini kinyume na sheria.
Leo februari 16 ndio ilikuwa siku ya hukumu baada ya umoja huo wa CCM kumkatia rufaa mama huyo mnyonge na aliyehitaji msaada wa hali na mali ambapo mahakama imetoa hukumu na kumuachia huru mama huyo mnyonge aliyetetewa na chama cha Mapinduzi kinachowajali, kuwatetea na kuwasemea wanyonge.
Hii ndio sababu ya CCM kuendelea kuwa kimbilio la wanyonge na kuendelea kuungwa mkono na kupigiwa kura za ndio kwa kishindo kila uchaguzi. Sasa unafikiri ni vipi mama huyu ambaye amebubujikwa machozi ya furaha baada ya kutolewa gerezani atashindwa kuipigia kura CCM?
Ni vipi ataacha kuiunga mkono CCM? Ni vipi ndugu, jamaa, marafiki na watoto wake wataacha kuipenda CCM iliyo mtetezi wa wanyonge?