Mbona hata huko majuu kwenye elimu za ukweli hayo majoho huvaliwa kuanzia ngazi ya chini kabisa.
Kama tumeiga mifumo ya elimu zao sioni ubaya tukiiga hayo mavazi kwenye ngazi tofauti za elimu.
After all ni majoho tu. Cha muhimu zaidi ni elimu aipatayo mtu.
Binti yangu ka graduate chekechea juzi kavaa joho na cheti juuu, ni shidaa hata hawaelewi maana ya hilo joho na cheti.
Na wewe pia Una Mtoto duh, kweli Dunia imefika mwisho au Ulimuiba Hosptalini?
Uko sahihi kabisa nilimuiba hospitalini.
Muache ufinyu wa mawazo,
Embu thamani ya digrii yenyewe iko wapi, wengi wamekwenda kujifunza "extra culiculum"" badala ya utaalam.
Mfano wanachuo kucheza picha za ngono .
Leo hii wanvyuo wote wameshusha thamani ya elimu kuliko ilivyotarajiwa kabisaaa .
Kujiuza mpaka thamani ya chips , leo unaniambia niheshim joho na wakati mvaaji mwenyewe ni kilaza wa stadi za maisha/?
Kingine leo unavaa joho mwakani unanigongea sigara mimi mgonga debe ntaliheshimu vipi joho na wakati ulie livaaa huna uhakika wa maisha?
In a course of 100 graduates, ni 10 pekee ndio wanadeserve hiyo degree. Wengi wamekariri tu na ukija kwenye real life ndipo utakapowaonea huruma. Hadi yule aliyesoma Bachelor ya Small Business and Entrepreneurship anatafuta kazi ya kuajiriwa..
Wabongo utawaweza?
Badala ya kujiuliza ubora wa elimu yetu ukoje watu wanajikita kwenye majoho.
Halafu hata kama mtu unajikita kwenye majoho, kukataza watoto kuvaa majoho ni habari zile zile za "watoto ni taifa la kesho" wakati watu wanaishi leo.
Kama joho ni kitu kizuri, basi ni kitu kizuri kwa wakubwa na watoto.
Hizi ndizo zile habari za kufanya elimu kuwa ngumu na kufikiri ndio kufanya elimu kuwa bora.
Linchi limekaa miaka kibao chuo kikuu kimoja tu, mwalimu anayefelisha sana ndiye anaonekana mzuri.
Unnecessary exclusivity.
Tuongelee elimu, joho hata vibaka wanaweza kufoji.
wewe sio mbongo ??
Wabongo utawaweza?
Badala ya kujiuliza ubora wa elimu yetu ukoje watu wanajikita kwenye majoho.
Halafu hata kama mtu unajikita kwenye majoho, kukataza watoto kuvaa majoho ni habari zile zile za "watoto ni taifa la kesho" wakati watu wanaishi leo.
Kama joho ni kitu kizuri, basi ni kitu kizuri kwa wakubwa na watoto.
Hizi ndizo zile habari za kufanya elimu kuwa ngumu na kufikiri ndio kufanya elimu kuwa bora.
Linchi limekaa miaka kibao chuo kikuu kimoja tu, mwalimu anayefelisha sana ndiye anaonekana mzuri.
Unnecessary exclusivity.
Tuongelee elimu, joho hata vibaka wanaweza kufoji.
Hiyo ndio shida ya mfumo wa elimu wa kitanzania,mitihani migumu ndio kudhani kwamba wanafanya elimu ionekane bora. mwalimu anakuja darasani anajigamba semista hii lazima nishike watu 200 kwenye somo langu kweli anafanya hivyo.
Nakumbuka miaka kadhaaa iliyopita nikiwa darasa la saba mwalimu wa hesabu alileta maswali ya Quadratic equation ya kutumia general formula wakati hayo mambo yanafundishwa kidato cha pili,wote tukapata sifuri,mwl akafanya watu waiogope hesabu na kuichukia.
Huo ni utamaduni wa elimu ya kitanzania,mwalimu anaetunga mtihani mgumu tena wa kufelisha watu ndio mzuri,niliwahi kufundisha shule moja ya taasisi ya dini kwa muda, mwisho wa mhula nikatunga mtihani wa hesabu na geografia watoto wakafaulu sana,nikaitwa na mwl mkuu,mwl wa taaluma na mkuu wa idara kuhojiwa kwa nini nimetunga mtihani rahisi wakati haukua rahisi ila nilijikita kwenye mambo niliowafundisha.
Mwisho wakanitimua kazi eti natunga mitihani rahisi,yani niwatungie tu kitu ambacho sijawahi kufundisha au hakiko katika mtaala wao ili wasifaulu sana.
Joho la ukweli ambalo nilivaa mimi lilikuwa na vipandevitatu = mortarboard (bonnet for PhD) or hat, gown, and hood. Bila utatu huujoho halina hadhi ya academic excellence katika levels za juu. Hata kwenyeKipaimara watoto wanavaa majoho lakini hayana utatu au chungu bila mafigamatatu hakifanyi kazi. Tuondoe wasiwasi ila siku wasiohusika na academicexcellence in a higher level, inabidi kuandamana!
Natia shaka na degree yako kama ulivaa joho bila kuwa criticalna ku-question maana ya vile vipande vitatu na utofauti wake katika rangi hasahood, na kwa nini wale wa PhD wanapigiwa na ala za brass band!!!!