Inflation drops to 4.5 pct – a five-year low-The Guardian

Bongolander

JF-Expert Member
Jul 10, 2007
5,067
2,197
Wakuu nime-copy paste hii kitu kutoka wb ya guardian. I wonder kama ni kweli inflation imeshuka kwa kuwa sijaona mabadiliko yoyote ya kushuka kwa bei ya vitu. Ninachokumbuka ni kuwa wakati wa mfungo wa ramadhani bei ya nguruwe ilishuka sana.

Sielewi CPI yetu inakokotolewa vipi na kwa vigezo gani, na kama kweli kikapu cha kukukokotolea CPI ni cha mboga na chakula tu.

I do not know whether it went down from 12% by 4.5% to 7.5%or it went down by 7.5% to 4.5% from 12%. Kiingereza na statistics vimenipiga chenga, naomba wajuzi mtusaidie kuelewa suala hili, hapa chini kuna kipande cha habari yenyewe.

16th October 2010

Tanzania`s year-on-year inflation rate slowed last month to its lowest level since November 2005, mainly due to weaker food prices, the National Bureau of Statistics said yesterday.
It attributed the fall chiefly to the weakening of food prices.
The bureau said that, at 55.9 per cent, food constituted the largest portion of the basket of goods the nation uses to calculate inflation “and a drop there sent the overall rate to 4.5 per cent in September from 6.6 per cent in August”.
“Food was the main reason for the fall in the inflation rate. Prices of items like rice actually fell,” Ephraim Kwesigabo, director of population census and social statistics, told Reuters.
According to NBS, rainfall had an outsized influence on inflation rates in East Africa because good rains lead to good harvests and lower prices. The region relies on rain-fed agriculture and drought in the past few years drove up inflation and hurt growth.
 
Hii habari kwa kweli nina mashaka nayo, katika miaka mitano iliopita bei ya mkate tu imepanda kutoka 300 hadi kwenye mia 500, halafu unaniambia inflation tanzania ni 4.5 haiwezekani.
the info i have the rate stands at about 11.06%
 
Yaani ni kichekesho na kichefuchefu papo!

Sijui wanatuona sote majuha!...yani hata picha tumeshindwa kuzitafsiri hivi unaniambiaje inflation imeshuka wakati mtaani mfumuko wa bei za kila kitu ziko katiaka record speed ya kupanda? Hizi ni habari za kuwapamba walengwa na kwa kwa kweli hazina uhalisia; leo hii kwa mara ya kwanza nashuhudia hadi CHUMVI ikipanda bei kwa kiwango cha kustusha!

Mia tano iliyokuwa ikitosha maandazi maane na sahani ya maharage na kikombe cha chai ya rangi miaka 5 nyuma sasa inanua maandazi mawili na chai ya rangi na unabaki na sh 50 amabayo haitoshi sahani ya maharage ya mia 2!

Mungu tusaidie!
 
Analysis hii haiko 'exhaustive'. Inflation ya Tanzania haichangiwi na chakula pekee, kuna vitu kama mafuta (petroli na dizeli) na pia nishati (umeme).
Kufanya uchambuzi kwa kuangalia chakula tu inatia mashaka.
 
Wamelipwa hao kuipamba ccm na utawala wa hovyo!we re tired with fucking ...
 
Inflation rate ya 4.5% siyo ya kweli kwa sababu
  • Karibu miaka miwili ilikuwa kwenye 10%- over 11%.
  • It was easy to agree hata kwa mlalahoi sabau bei bei za kila kitu zilikuwa juu mafuta, vyakula, etc
  • kwa kushuka kwa kiwango kikubwa hivyo lazima tungeona impact yake kwenye bei ya vitu vyakula, mafuta n.k bila hata serikali kutoa figure
  • Ukweli hamna hata bei ya kitu chochote kilichoshuka bei, mkate, sukari, chumvi, mboga, matunda, mchele, unga, vyakula mahotelini na kwa mama ntilie, dizeli, petrol, gas, mafuta ya taa, umeme. vyote bei juu na vinapanda kila siku kidogo kidogo, hata benki interest rate ni juuuuuu.
  • Figure zimetolewa kudanganya wananchi, investors na donors kipindi hiki cha uchaguzi, ukweli ni kuwa figure zimepikwa
Kwahili limenikera na naamini waungwana wote wamekereka kwa upotoshaji huu wa makusudi
 
Jamani hizi ni annual Inflation rate figures ambazo zinaangalia ongezeko la bei toka mwezi kama huo mwaka uliopita. Yaani bei za bidhaa za Septemba 2010 zimeongezeka kwa wastani wa asilimi 4.5 toka mwezi Septemba mwaka jana. Sasa cha msingi hapa ni kuangalia bei (na si viwangi vya mfumuko wa bei) za mwaka jana zilikuwaje na kisha ulinganishe na mwaka huu katika kipindi kinachowiana (i.e mwezi sawa sawa).

Lakini pia kumbukeni ya kwamba mfumuko wa bei ni weighted average ambako ndani yake kuna price indices za bidhaa mbalimbali ambazo zimepewa uzito tofauti. Hivyo ni kitu cha kawaida kukuta bei za bidhaa X zimeongezeka hata mara mbili au tatu ya mfumuko mzima wa bei unaotolewa lakini unakuta uzito wake "mchango" wake katika wastani huo si mkubwa kiasi cha kuweza kubadilisha wastani kwa kiasi kikubwa.

Unapotoa taarifa chache hivi inakuwa ni vigumu kidogo mtu kupata picha kamili ya mambo. Hili la kuongezeka wa bei ya mkate toka shilingi 300 mpaka 600 katika kipindi cha miaka mitano, ni vyema mtu akachukua taarifa za price indices za miaka husika (i.e 2005 na 2010), akamua mwaka upi atautumia kama kigezo, aka normalize indices na kisha kuangalia ongezeko limekuwa la kiasi gani. Katika survey ya bajeti na matumizi ya kaya ya 2007, walilinganisha indices za 2007 na 2001 na kukuta ya kuwa bei zimeongezeka kwa asilimia 93 katika kipindi hicho. Hiii kitu ni rahisi kwa mtu mwenye kufahamu haya mambo, naweza kuifanya na kuweka hapa ila mambo yamenikamata. Nikipata muda nitaweka.
 
[Sielewi CPI yetu inakokotolewa vipi na kwa vigezo gani, na kama kweli kikapu cha kukukokotolea CPI ni cha mboga na chakula tu.]

Sijui mtoa mada alikuwa anamaanisha nini,alipokuongelea CPI,lakini mimi naamini alikuwa anaanisha Consumer Price index.
Nikija kwenye hoja ya msingi,mimi nafikiri kushuka kwa mfumuko wa bei kunatokana na kubadilishwa kwa kanuni ya kukokotoa mfumuko wa bei na wala si hali halisi ya kupungua kwa mfumuko wa bei sokoni.Kanuni ya zamani ilikuwa inatoa weight kubwa kwa foodstuffs,lakini ya sasa a great weight is given to products like airtime expenses,construction materials and other importance materials rather than foodstuffs.kwa kuwa foodstuffs inapanda na kushuka mara kwa mara,kuliko bidhaa nyingine!
 
Back
Top Bottom