Inasikitisha na kuhuzunisha sana jinsi 'plants' za madini zinavyohatarisha maisha ya watu

Artificial intelligence

JF-Expert Member
Jan 28, 2021
1,262
2,192
Kiukweli nilibahatika kutembelea jumla ya plants za madini 9, tatu kahama Shinyanga na 6 wiliya ya Bukombe Geita. Nilichokiona na kukishuhudia kwenye plants hizo ni cha kuhuzunisha na kusitikisha sana haswa kuhusu afya za watu walioajiriwa kwenye hizo plants na wanaoishi kuzunguka hizo plants.

Plants hizo ambazo zinajihusisha na uchenjuaji wa dhahabu kutoka kwenye mchanga au mawe ni za watu wenye kipato cha kati na cha juu, ili kuendesha plants hizo, wataalamu mbalimbali wa kusimamia na kuendesha shughuli hiyo uhitajika.

Jinsi gani zinahatarisha afya za watu, niligundua baadhi ya mambo kama ifuatavyo

Kwanza
Wataalamu walioajiriwa ni unprofessional, hawana taaluma ya kile wanachokifanyia kazi. Hapa nitatolea mfano wakemia wanaotumika kupima na kuandaa kemikali zinazohitajika Kwa ajili ya uchenjuaji, cha kwanza kabisa katika plants zote hizo ni plant moja tu iliyokuwa na mkemia ambaye ni professional (na huyo anasema ndiye anaye wafundisha vijana), zilizobaki ni vijana wanachukuliwa mtaani na kufundishwa jinsi ya kupima na kuandaa hizo kemikali, vijana hawa kwa sababu hawana ujuzi zaidi kuhusu hiyo taaluma wanajikuta wakifanya kazi katika mazingira magumu sana.

Vijana wanaingia maabara bila vifaa maalumu vya kujikinga na kumwagikiwa au kudondokewa na sumu hizo za kemikali, katika hali ya kustahajabisha vijana hawa ushika kemikali kwa mikono na vifaa vya kemikali bila kujali, hapa ndipo wanajikuta katika matatizo ya kiafya kwani nilishuhudia baadhi yao wakikohoa damu, kucha kuchomoka, nywele kuungua, ngozi kubabuka n.k, baada ya kuwauliza Kwa nini jibu lilikuwa ni sisi "tumeshazoea haya ndiyo maisha yetu, tunajua tutakufa". Hii ni kwa sababu maabara hazikizi viwanga na ukosefu wa maarifa kuhusu good laboratory practices na laboratory safety.

Wakati nikiwa Bukombe, sehemu moja inaitwa namba moja, kuna plant moja kijana alikuwa anachanganya conc. Sulfuric acid kwa bahati mbaya sijuhi alikosea nini, kutokana na kuvuta hewa yake kwa sababu moshi ulitanda chumba kizima, alipiga kelele na kuomba msaada, wakati anatolewa kupelekwa kituo cha afya alisema hivi "siwezi kuona", kituoni aliambiwa sumu aliyovuta hawaiwezi ikabidi apelekwe hospitali ya wilaya Bukombe, kiukweli mpaka natoka kule kijana niliacha hajaweza kuona tena.

Pili
Uchafuzi wa vyanzo vya maji vinavyozunguka plants hizo, hapa ndipo kuna hatari kubwa sana ya watu wa kanda ya ziwa kupata cancer, kwani plants hizo hazina wataalamu wenye utaalamu wowote kuhusu "chemical speciation" na "waste management", hivyo hawajuhi chochote kuhusu bio-concentration, bio-accumulation concepts, hivyo kemikali hizo baada ya kuzifanyia treatment uzitoa kwenye mantenki na kwenda kuzitupa bila utaratibu, kwahiyo kemikali hizo utiririka hadi kwenye vyanzo vya maji kama mito na visima ,hali hii inapelekea maji wanayotumia kutoka kwenye visima na samaki kutoka kwenye mabwawa na hiyo mito kuwa na kiasi kikubwa cha kemikali hizo zenye sumu.

Pamoja na kwamba ni uchimbaji mdogo, lakini unahitaji utaalamu na usimamizi pia, wamiliki wa plants wanapata pesa nyingi, lakini hawajali kabisa kuhusu afya za watu, NEMC pamoja na ofisi ya mkemia mkuu mkuu wa serikali (GCLA) kwa kushirikiana na wizara ya madini chini ya serikali mnao wajibu wa kusimamia hili ili kuwanusuru watu kutokana na hizo sumu za kemikali.

Najua kuna rushwa kubwa sana kule, Ila wekeni nguvu, vijana mikono, miguu inatoboka tu, huku wenye plants wakivuna pesa.
 
Dah umeongea kwa uchungu sana mkuu. Kikubwa wawe na vifaa na wapate mafunzo kazini.

Hata uwe na degree ukifika site unaanza kujifunza upya ndio maana mgodini utakuta form four aliyefeli anamfundisha kazi mtu mwenye degree ya geology.

Degree za kukariri ni tofauti na uhalisia huko migodini.
 
Ulicho kiongea nikweli shida iliyopo ndg ni tamaa...iko hivi utakuta mtaalam au professional wa taaluma husika mkemia anakuwa na msaidizi akisha jua namna ya kuchanganya kemiko zile anavimba kichwa anaanza kufanya kazi kimya kimya kisa ameonekana Mara kwa Mara yuko na mkemia.

Mkemia mmekubaliana 1.5m kukamilisha kazi plant hadi elution tutakapo maliza kazi yetu.sasa huyu msaidizi anajiona ameiva anachukuliwa na MTU frani anakuwa anaenda kumchekia kazi yake huko ila wamekubaliana atapewa laki 8 anakubali anaweza akawa ameshika plant kama 3 akilipwa hizo bei za laki 8 anaona bingo.

Unakuja kwa opp yye anapewa maelekezo na mkemia kaweke cyanide kiasi frani tank namba frani anachukuwa kwa mkono bila groves wala nni anajiita jembe.wanateseka sna hawa vijana kiukweli kama kuhusu maji usiseme ile ballen unakuta iko overflow hadi unashindwa kuelewa hivi hawa wanafahamu madhara ya hivi kemikali kweli, mbaya zaidi tunaenda kipindi cha mvua yani NEMC wanatakiwa kufanya kazi yaziada sna.

Wito Mchimbaji yoyote ukitaka kusaidia hili jambo 1.ukitaka kupeleka mzigo wako plant kagua mszingira husika ya plant pamoja na choo,2,tafuta mkemia'usitafute hao wa bei ya chini wanahalibu kazi za watu,3,mjitahidi wahusika wa mnao peleka mzigo punguzeni ushikaji ktk kazi ili kunusulu hawa vijana kuwapoteza'ile lugha ya kusema mbona kafrani kalinitolea kilo kadhaa kazuri kuliko yule mkemia'hacheni sipo kupiga promo kwa hawa wakemi la hasha natazama madhara baada ya mda frani itakuwaje atakuwa ata ndg yako siku moja.mleta mada umeongea kitu kikubwa sna safi sana
 
Nilishuhudia baadhi yao wakikohoa damu, kucha kuchomoka, nywele kuungua, ngozi kubabuka n.k, baada ya kuwauliza Kwa nini jibu lilikuwa ni sisi "tumeshazoea haya ndiyo maisha yetu, tunajua tutakufa".

mtu ana chomoka kucha afu anasema kazoea pesa bwana
 
Hii nayo ngumu kumeza,pamoja na ugumu wa maisha tulionao watanzania wenzangu bado uhai ni kiti cha thamani sana!!!

Unakubalije kuingia Plant area bila PPE?
Hamna cha PPE wala nini ndugu, Kwanza vijana ukiwauliza kuhusu PPE wanakushangaa kabisa, kiukweli niliwahurumia sana.
 
Dah umeongea kwa uchungu sana mkuu. Kikubwa wawe na vifaa na wapate mafunzo kazini.
Hata uwe na degree ukifika site unaanza kujifunza upya ndio maana mgodini utakuta form four aliyefeli anamfundisha kazi mtu mwenye degree ya geology.
Degree za kukariri ni tofauti na uhalisia huko migodini.
Mimi concern yangu kubwa ni usalama wao, vifaa hawapewi, kuhusu suala la degree hata kama mtu kakariri uelewa wake ni mkubwa kuhusu kitu anachokifanyia kazi kwa sababu tayari angalau ana basics, tofauti na mtu anayefundishwa tu kazi, hajuhi basics za kile anachokifanyia kazi.
 
Ulicho kiongea nikweli shida iliyopo ndg ni tamaa...iko hivi utakuta mtaalam au professional wa taaluma husika mkemia anakuwa na msaidizi akisha jua namna ya kuchanganya kemiko zile anavimba kichwa anaanza kufanya kazi kimya kimya kisa ameonekana Mara kwa Mara yuko na mkemia.

Mkemia mmekubaliana 1.5m kukamilisha kazi plant hadi elution tutakapo maliza kazi yetu.sasa huyu msaidizi anajiona ameiva anachukuliwa na MTU frani anakuwa anaenda kumchekia kazi yake huko ila wamekubaliana atapewa laki 8 anakubali anaweza akawa ameshika plant kama 3 akilipwa hizo bei za laki 8 anaona bingo.

Unakuja kwa opp yye anapewa maelekezo na mkemia kaweke cyanide kiasi frani tank namba frani anachukuwa kwa mkono bila groves wala nni anajiita jembe.wanateseka sna hawa vijana kiukweli kama kuhusu maji usiseme ile ballen unakuta iko overflow hadi unashindwa kuelewa hivi hawa wanafahamu madhara ya hivi kemikali kweli, mbaya zaidi tunaenda kipindi cha mvua yani NEMC wanatakiwa kufanya kazi yaziada sna.

Wito Mchimbaji yoyote ukitaka kusaidia hili jambo 1.ukitaka kupeleka mzigo wako plant kagua mszingira husika ya plant pamoja na choo,2,tafuta mkemia'usitafute hao wa bei ya chini wanahalibu kazi za watu,3,mjitahidi wahusika wa mnao peleka mzigo punguzeni ushikaji ktk kazi ili kunusulu hawa vijana kuwapoteza'ile lugha ya kusema mbona kafrani kalinitolea kilo kadhaa kazuri kuliko yule mkemia'hacheni sipo kupiga promo kwa hawa wakemi la hasha natazama madhara baada ya mda frani itakuwaje atakuwa ata ndg yako siku moja.mleta mada umeongea kitu kikubwa sna safi sana

Sent from my itel it1408 using JamiiForums mobile app
Unaongea ukweli kabisa, baadhi niliowauliza walisema wanalipwa laki 2 hadi laki 3 na nusu, hebu fikiria kemikali zilivyo hatari zile mtu ana hatarisha maisha yake vile alafu malipo kama hayo, ndiyo maana ni ngumu sana kukutana na mkemia sahihi kule, wengi ni wanatoa mtaani wanawafundisha ndiyo wanawapeleka kuwaua na kemikali zao hizo. Kuhusu maji wananchi wenyewe wa hayo maeneo wanasema wanafahamu Ila hawana namna zaidi ya kuyatumia.
 
Nilishuhudia baadhi yao wakikohoa damu, kucha kuchomoka, nywele kuungua, ngozi kubabuka n.k, baada ya kuwauliza Kwa nini jibu lilikuwa ni sisi "tumeshazoea haya ndiyo maisha yetu, tunajua tutakufa".

mtu ana chomoka kucha afu anasema kazoea pesa bwana
Inasikitisha sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom