Imekaaje wachezaji mpira kufanya sala au dua kabla ya mechi dhidi ya wapinzani wao?

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,634
46,277
Huwa naona wachezaji mpira wakisali kabla ya kuanza kucheza, pia katika nchi kama yetu huwa nasikia wadau, viongozi wa serikali, timu na mpira kwa ujumla wakihamasisha raia waiombee timu ya taifa au vilabu vyao pendwa vishinde mechi.

Ikiwa upande wa pili wa timu pinzani nao itafanya au unafanya hivyo haya si yatakuwa mashindano ya kusikilizwa kwa sala au dua?

Je hii inakuwa na mashiko yoyote katika timu kushinda au kushindwa?

Mungu anakubali maombi ya aina hii ya kuiombea timu nyingine ishindwe?
 
Halafu mchezaji huyo huyo anayeonekana kufanya sala kabla ya match ndio mchezaji huyo huyo ambaye aliingia uwanjani kinyume nyume kupitia mlango usio rasmi (siwasemi Yanga)

Halafu ikatokea amefunga goli anafanya ishara ya msalaba au anasujudu.

Then fans kama kawaida yao wanatoa appreciation sehemu isiyo stahili utaskia "Azizi Ki ni kiboko" (nimetolea mfano japo una ukweli)

NB: Haters wataumizwa na maneno machache ya kwenye mabano na kusahau ujumbe mzuri nilioandika kwa maneno mengi
 
Angalia mifano hii. Ulishaenda kufanya usaili?, Mfungwa, Mkulima, Mgonjwa alioko hospital/Nyumbani n.k n.k Kila MTU anaomba kwa ajili yake tu. Yaani anaeomba anakuwa specific na si general.
 
Halafu mchezaji huyo huyo anayeonekana kufanya sala kabla ya match ndio mchezaji huyo huyo ambaye aliingia uwanjani kinyume nyume kupitia mlango usio rasmi (siwasemi Yanga)

Halafu ikatokea amefunga goli anafanya ishara ya msalaba au anasujudu.

Then fans kama kawaida yao wanatoa appreciation sehemu isiyo stahili utaskia "Azizi Ki ni kiboko" (nimetolea mfano japo una ukweli)

NB: Haters wataumizwa na maneno machache ya kwenye mabano na kusahau ujumbe mzuri nilioandika kwa maneno mengi
Wewe, zipo kweli au dishi limeyumba?
 
Kwanza mpira ni ushetwani, Mungu huwa anaziba masikio na kufumba macho mpira unapochezwa.
 
Huwa naona wachezaji mpira wakisali kabla ya kuanza kucheza, pia katika nchi kama yetu huwa nasikia wadau, viongozi wa serikali, timu na mpira kwa ujumla wakihamasisha raia waiombee timu ya taifa au vilabu vyao pendwa vishinde mechi.

Ikiwa upande wa pili wa timu pinzani nao itafanya au unafanya hivyo haya si yatakuwa mashindano ya kusikilizwa kwa sala au dua?

Je hii inakuwa na mashiko yoyote katika timu kushinda au kushindwa?

Mungu anakubali maombi ya aina hii ya kuiombea timu nyingine ishindwe?
Afrika(nyeusi) kila kitu ni kumwachia Mungu!
Kila kitu tunaenda kuomba Mungu kanisani, kuna nchi huwa zinatenga kabisa player day, breakfast! Unatumia pesa ya umma kuwaleta viongozi wa dini wapige Dua! Ukame uishe! Na kusiwe na mafuriko!
Ukame unakuja na mafuriko yanakuja na watu wanakufa! Badala ya kutumia pesa hizo kujenga miundombinu!
 
Kwa mujibu wa dini yangu.
Sio dua zoote zinapokelewa, nyingine hazifiki popote kutokana na uchamungu wa mtu,
Zikipokelewa si lazima mungu akupe kike ulichoomba tu, huenda akakupa kingine bora zaidi.
Kuna elimu ya qadar hapo ndani yake. Elimu pana hii.

Sasa umevaa muhirizi, bado una muomba mungu hilo moja.
Lakini pia wengine huwa hawaombi matokeo tu, wengine wanaomba usalama wao uwanjani..
 
Maombi yako hivi
Ukijibiwa ndio.. ni Mungu amefanya hata Kama ni bahati tu au jitihada zimetumika
Ukijibiwa hapana.. Mungu ana mpango wake cjui we sio mcha Mungu.. etc
Usipojibiwa.. it's either yes or no plus time
So prayer ni sawa na kubeti.. na either way Mungu bado atapewa sifa hata Kama mtoto wa miaka 2 kafa na cancer bado watasema mungu ana mpango mzuri baadae...😓dini ni upofu
 
Back
Top Bottom