jojipoji koromije
JF-Expert Member
- Mar 22, 2017
- 991
- 1,412
Katika kuendesha gari kwangu nchi hii sijawahi ona askari waliokosa weledi kama askari wa maeneo haya ya Mufindi Sao Hill check point barabara ya Dar-Mbeya. Wanalazimisha makosa sana au wameagizwa kila gari lazima waipige fine?
Wanataka kila gari itembee nyuma ya roli linalopanda mlima mkali na speed 10, wewe una gari nyepesi ukae nyuma yake tu muda wote mpaka umalize mlima kwasababu tu uki overtake hata hakuna gari linalokuja mbele yako tayari unapigwa fine.
Kwahiyo mko tayari sisi madereva na abiria tufe ikitokea lori lililopo mbele limefeli break ili msitulipishe fine? Tufe ili kukwepa fine?
Naombeni Jeshi la polisi Makao Makuu wadhibitini hawa askari wanaojificha bondeni kwenye mteremko wa changarawe; hasa huyu askari mwenye mustachi kama wa mkoloni Carl Peter’s wa Ujerumani, na hawa wanokaa Checkpoint ya Msitu wa Sao Hill, wamekosa ubinadamu kabisa zaidi ya kushinikiza fine na rushwa.
Ikibidi kamanda IGP hawa askari wako wahamishie njia za vumbi huko Kambi Katoto, Mtego wa Simba, Namanyere na Nanjilinji wakajifunze jinsi ya kuwa na utu na ubinadamu, wamejaa roho mbaya sana hawa askari.
IGP naomba ulifanyie kazi hili. Watafutie vituo hawa pembezoni mwa nchi, wakirudi barabara za lami tena labda watakuwa wamejifunza utu na ustaarabu katika kutimiza majukumu yao ambalo ndio jambo kubwa.
Mama yetu mpendwa Rais Dr. Samia Suluhu Hassan anahubiri kila siku ila wao wameshindwa kuendana na maono ya Mama.
Nawasilisha.
Wanataka kila gari itembee nyuma ya roli linalopanda mlima mkali na speed 10, wewe una gari nyepesi ukae nyuma yake tu muda wote mpaka umalize mlima kwasababu tu uki overtake hata hakuna gari linalokuja mbele yako tayari unapigwa fine.
Kwahiyo mko tayari sisi madereva na abiria tufe ikitokea lori lililopo mbele limefeli break ili msitulipishe fine? Tufe ili kukwepa fine?
Naombeni Jeshi la polisi Makao Makuu wadhibitini hawa askari wanaojificha bondeni kwenye mteremko wa changarawe; hasa huyu askari mwenye mustachi kama wa mkoloni Carl Peter’s wa Ujerumani, na hawa wanokaa Checkpoint ya Msitu wa Sao Hill, wamekosa ubinadamu kabisa zaidi ya kushinikiza fine na rushwa.
Ikibidi kamanda IGP hawa askari wako wahamishie njia za vumbi huko Kambi Katoto, Mtego wa Simba, Namanyere na Nanjilinji wakajifunze jinsi ya kuwa na utu na ubinadamu, wamejaa roho mbaya sana hawa askari.
IGP naomba ulifanyie kazi hili. Watafutie vituo hawa pembezoni mwa nchi, wakirudi barabara za lami tena labda watakuwa wamejifunza utu na ustaarabu katika kutimiza majukumu yao ambalo ndio jambo kubwa.
Mama yetu mpendwa Rais Dr. Samia Suluhu Hassan anahubiri kila siku ila wao wameshindwa kuendana na maono ya Mama.
Nawasilisha.