Wakuu jana katika kipindi special cha American Pop Idol (BSS ya US) kiitwacho Idol Gives Back niliona kitu sikukielewa. Kipindi hicho ambacho ni mahususi kwa kuchangisha pesa kutoka kwa watazamaji luninga walio majumbani kwa ajili ya kusaidia watoto masikini kinatumia umaarufu wake, wa viongozi na wasanii maarufu duniani. Jana Obama na mkewe walikuwa live kupitia luninga kufungua kipindi hicho. Wengine walioshiriki ni Ban ki Moon, Morgan Freeman and Victoria Bekham. Kwa ujumla kilukuwa na watu wengine wengi maarufu akiwemo queen latifa.
Ni jambo zuri sana wanalifanya hakuna ubishi katika hilo. Ila mimi nlishangaa waliporusha clip yao moja waliyorekodi inayoonyesha watoto taabani wakiwa wanaugua maleria hospitali. Ilionyesha magari mawili yenye namba za SM na mojawapo ni landcruiser iliyoandikwa ubavuni 'hospitali ya amana manispaa ya Ilala'. Aliyekuwa ananarrate video akadai "our recent visit to Kenya encountered children in a hospital in Kenya...blabla....na ndipo gari hizo zinaonekana zikiingia hospitali ambayo nadhani itakuwa ndo Amana!!
Je ni makosa ya kiufundi au ni yale yale ya usanii wa wakenya dhidi ya Tanzania. Wanapotumia matukio ya Tanzania kuelezea Kenya kwenye tukio kubwa na maaruku kama hilo wana maana gani. Pesa zinazopatikana na hata mind set na huruma ya hao watoa misaada si itaelekea Kenya japo hali halisi (picha) iliyowatia huruma ni ya Tanzania? Ni yale yale ya Mlima Kilimanjaro kusemwa uko Kenya? Nikichanganya hili na hoja za ushirikiano wa afrika mashariki naungana kabisa na wanaopinga kushirikiana na especially wakenya...nadhani wana ubinafsi na utapeli flani wenye madhara makubwa!!
Naliacha kwenu kwa kuliwazua na kutoa maoni!!
Ni jambo zuri sana wanalifanya hakuna ubishi katika hilo. Ila mimi nlishangaa waliporusha clip yao moja waliyorekodi inayoonyesha watoto taabani wakiwa wanaugua maleria hospitali. Ilionyesha magari mawili yenye namba za SM na mojawapo ni landcruiser iliyoandikwa ubavuni 'hospitali ya amana manispaa ya Ilala'. Aliyekuwa ananarrate video akadai "our recent visit to Kenya encountered children in a hospital in Kenya...blabla....na ndipo gari hizo zinaonekana zikiingia hospitali ambayo nadhani itakuwa ndo Amana!!
Je ni makosa ya kiufundi au ni yale yale ya usanii wa wakenya dhidi ya Tanzania. Wanapotumia matukio ya Tanzania kuelezea Kenya kwenye tukio kubwa na maaruku kama hilo wana maana gani. Pesa zinazopatikana na hata mind set na huruma ya hao watoa misaada si itaelekea Kenya japo hali halisi (picha) iliyowatia huruma ni ya Tanzania? Ni yale yale ya Mlima Kilimanjaro kusemwa uko Kenya? Nikichanganya hili na hoja za ushirikiano wa afrika mashariki naungana kabisa na wanaopinga kushirikiana na especially wakenya...nadhani wana ubinafsi na utapeli flani wenye madhara makubwa!!
Naliacha kwenu kwa kuliwazua na kutoa maoni!!