"Idadi ya jumla ya benki 53 mpaka sasa Tanzania, BOT wanaweza kuzisimamia vyema?"

buhange

JF-Expert Member
Oct 23, 2011
505
110
Habari zenu wana JF.

Nimevutiwa kuanzisha thread hii baada ya swala hili kuletwa kama maada katika gazeti la THE CITIZEN la tar. 28 june 2014. Baadhi ya wasomi katika taaluma ya fedha wameilalamikia BOT kwa kuweka kiwango kidogo cha Tsh. 12 bilioni kama kiwango kwa taasisi ya fedha kupata banking lisence kama Commercial bank na Tsh. 2 bilioni kuwa Community bank, wengine wakisema hakuna haja ya kuwa na utitili wa benki 53 wakati asilimia kubwa ya watanzania wakiishi chini ya dola 2 kwa siku.

Lakini pia wengne wakaenda mbali kwa kutolea mifano nchi kama Nigeria ambayo miaka kumi iliyopita ilikuwa na jumla ya benki 83 huku uchumi wake ukiwa mbovu, huku kwa sasa ikibaki na benki 22 licha ya kiwango kizuri ilichonacho cha uchumi.

Mtanzania mwenzangu, unasemaje juu ya hili, benki zikipungua idadi ushindani utakuwaje!, vipi kuhusu hali ya mikopo kwa watanzania maskini?

Karibu kwa maoni wadau.
 
Ngoja wachumi waje hapa tutapata faida ya hizo bank au hasara zake,nadhani kwa wingi wa bank ni mzuri kuleta ushindani kibiashara hata mikopo Kwa wananchi,isitoshe nchi yetu tatizo la mitaji nikubwa sana
 
Ni kweli mkuu, kwa kutumia akili ya kawaida tuu ni kwamba kuongezeka kwa idadi ya benki inamaanisha kuongezeka kwa huduma za kibenki na pia huduma hizo kuwa bora kutokana na ushindani baina ya benki hizo.
 
Bot ikiwa chini ya Gavana Beno Ndullu hawajafanya kazi nzuri ya kuzisimamia hizi benki na bureaux de change na ndio maana watu wanaweza kutorosha fedha na kuziweka kwenye mabenki nchi za nje bila wao kujua. Mabenki kazi yao ya msingi ni kukopesha wateja na kutokana nakukopesha huko hutoza riba ambayo ndio inatakiwa kuwa chanzo kukubwa cha faida yao. Kwa bahati na kutokana na utendaji mbovu wa BOT mabenki mengi hapa nchini hutengeneza faida sio kwa kukopesha wananchi bali kwa kuwatoza ushuru [bank charges] wateja wao kutokana na huduma wanazotoa na charges hizo hupata kibali cha BOT ingawa nyingine ndio zinadumaza kuongezeka kwa wateja wanaotakiwa kutumia benki!!

Nitatoa mfano mmoja wa charges za benki zisizokuwa za msingi zinazotozwa na benki nyingi hasa CRDB; hawa wanatoza kwa mteja kuwa na account kila mwezi [ monthly maintenance fee]na hapo hapo wanakutoza ushuru kila mara unapotoa fedha zako benki [withdrawal charge]!! Ninavyoelewa mimi maintaining an account maana yake kuingiza na kutoa fedha kwenye account sasa kwanini wakutoze ushuru kwa kutoa fedha zako toka kwenye account yako ambayo unailipia kila mwezi?

Kama BOT inashindwa kusimamia mambo madogo madogo kama haya ya unnecessary repressive bank charges wakati wana hizo benki 53, je zikifika 100 watakuwa na uwezo wa kuzisimamia kwa umakini? Core capital requirement ya commercial banks ni shs 15 billion !!
 
Asante kwa mchango kaka, kiukweli benki nyingne wamezidi aiseeee
 
Bot ikiwa chini ya Gavana Beno Ndullu hawajafanya kazi nzuri ya kuzisimamia hizi benki na bureaux de change na ndio maana watu wanaweza kutorosha fedha na kuziweka kwenye mabenki nchi za nje bila wao kujua. Mabenki kazi yao ya msingi ni kukopesha wateja na kutokana nakukopesha huko hutoza riba ambayo ndio inatakiwa kuwa chanzo kukubwa cha faida yao. Kwa bahati na kutokana na utendaji mbovu wa BOT mabenki mengi hapa nchini hutengeneza faida sio kwa kukopesha wananchi bali kwa kuwatoza ushuru [bank charges] wateja wao kutokana na huduma wanazotoa na charges hizo hupata kibali cha BOT ingawa nyingine ndio zinadumaza kuongezeka kwa wateja wanaotakiwa kutumia benki!!

Nitatoa mfano mmoja wa charges za benki zisizokuwa za msingi zinazotozwa na benki nyingi hasa CRDB; hawa wanatoza kwa mteja kuwa na account kila mwezi [ monthly maintenance fee]na hapo hapo wanakutoza ushuru kila mara unapotoa fedha zako benki [withdrawal charge]!! Ninavyoelewa mimi maintaining an account maana yake kuingiza na kutoa fedha kwenye account sasa kwanini wakutoze ushuru kwa kutoa fedha zako toka kwenye account yako ambayo unailipia kila mwezi?

Kama BOT inashindwa kusimamia mambo madogo madogo kama haya ya unnecessary repressive bank charges wakati wana hizo benki 53, je zikifika 100 watakuwa na uwezo wa kuzisimamia kwa umakini? Core capital requirement ya commercial banks ni shs 15 billion !!

Kati ya watanzania 48m wanaotumia huduma za kibenki hawazidi 14%
 
Kuwa na bank 53 ni kupoteza rasilimali.

Ndo mana financial statements zinachelewa zaidi ya mwaka mmoja mbele.

Regulations inakuwa shida sana kukiwa na benki nyingi.

Wanachotakiwa hizo banks ziwe merged na kutoa banks 20 tu.
 
Kuna baadhi ya watanzania wamekuwa na walakini ktk wazo lako Bulldog la kushauri kwamba hizi banks ziwe merged ili kupata banks chache zilizo bora kwa maelezo kwamba, uchache wa banks utazifanya taasisi hizo kuendekeza Monopoly policy kiasi cha kutengeneza financial services expensive na wachache wenye kipato ndo watakuwa na uhakika wa kupata huduma ipasavyo. Watanzania waliowengi ni low income earners, so acha huo utitili uendelee ili kuruhusu market competition ktk banking industry
 
Tanzania tuna benki chache sana nenda Kenya kaulize wana benki ngapi ndio ujue.

Mimi kama mteja nataka ziongezeke zifike hata 100 , hapo ndio sisi wananchi tutapata huduma nzuri, wananchi wa vijijini watafikiwa, huduma itakuwa bei nafuu na tutakuwa na uhuru zaidi wa kuchagua. Kwa sasa riba ni 20% tukikopa just imagine.

Leo wakisema Voda na Airtel zinafungwa mtafurahi ibaki Tigo peke yake mtafurahi?
 
Kati ya watanzania 48m wanaotumia huduma za kibenki hawazidi 14%


Kama nia ni kuongeza wananchi wengi kutumia mabenki, je ni sahihi kuwatoza hao wachache [14% ] charges ambazo kiukweli sio halali kwa nia ya kutengeneza faida? In fact hata hao 14% hawaweki fedha zao nyingi kwenye mabenki kasababu ya makato yasiyo halali hivyo kuamua kuficha kwenye magodoro with all the attendant risks!! BOT will be well advised to review all the bank charges currently in operation.
 
Haha! haha! haha! Bila FINCA Microfinance mambo hayaendi kwa sisi wajasiliamali wa chini. Sina nyumba, sina kiwanja, sina mdhamini wanaeona wao anafaa CRDB au Barclays mkopo ntaupata wapi? Waongeze tuu hizo benki zifike hata 98 ndo nafuu yetu
 
Bot ikiwa chini ya Gavana Beno Ndullu hawajafanya kazi nzuri ya kuzisimamia hizi benki na bureaux de change na ndio maana watu wanaweza kutorosha fedha na kuziweka kwenye mabenki nchi za nje bila wao kujua. Mabenki kazi yao ya msingi ni kukopesha wateja na kutokana nakukopesha huko hutoza riba ambayo ndio inatakiwa kuwa chanzo kukubwa cha faida yao. Kwa bahati na kutokana na utendaji mbovu wa BOT mabenki mengi hapa nchini hutengeneza faida sio kwa kukopesha wananchi bali kwa kuwatoza ushuru [bank charges] wateja wao kutokana na huduma wanazotoa na charges hizo hupata kibali cha BOT ingawa nyingine ndio zinadumaza kuongezeka kwa wateja wanaotakiwa kutumia benki!!

Nitatoa mfano mmoja wa charges za benki zisizokuwa za msingi zinazotozwa na benki nyingi hasa CRDB; hawa wanatoza kwa mteja kuwa na account kila mwezi [ monthly maintenance fee]na hapo hapo wanakutoza ushuru kila mara unapotoa fedha zako benki [withdrawal charge]!! Ninavyoelewa mimi maintaining an account maana yake kuingiza na kutoa fedha kwenye account sasa kwanini wakutoze ushuru kwa kutoa fedha zako toka kwenye account yako ambayo unailipia kila mwezi?

Kama BOT inashindwa kusimamia mambo madogo madogo kama haya ya unnecessary repressive bank charges wakati wana hizo benki 53, je zikifika 100 watakuwa na uwezo wa kuzisimamia kwa umakini? Core capital requirement ya commercial banks ni shs 15 billion !!

Issue ya charges haiwezi kutatuliwa na idadi ya mabenki, in fact tunachoitaji ni kuwa na sheria za kumlinda mteja katika huduma za kifedha. Ukosefu wa sheria hii ndio unaotoa mwanya kwa mabenki na hata taasisi nyingine za fedha kucharge wateja isivyo sawa. Kwa sasa bot inayalazimu mabenki kupublish tarifs and charges ili mwananchi afanye mwenyewe decision lkn iyo haisaidii coz always panakua na hiden charges.
 
Ni kweli, kama issue ya client direct charges ingewekwa wazi katika haya mabenki atleast sisi clients tungekuwa na option kwa kuangalia interest on loan na nyingine pia, ila hizi hidden charges ndo zinazotuumiza, BOT lazima waweke law enforcenment strategies zitakazomsaidia mteja wa hali yoyote awe na confidence ya ku-join ktk banking services bila walakini wowote
 
Niliona shida hii Muda kidogo. Sweden ambayo Imeendelea kuliko sisi Ina benki 4 tu. Hapa kwetu katika mabenki hayo yote wenye account Ni wale wale tu unakuta mtu Ana akaunti 5 benki tofauti. Hizi haziwezi leta maendeleo Bali ni kama Kamari tu.
 
Duuuh! Sure hili swala la mtu mmoja kuwa na akaunti 4 ktk benki tofauti nalo ni kamali zile zile
 
Back
Top Bottom