Huyu mkandarasi wa barabara ya Tanga, Turiani, Dumila, Kilosa mpaka Mikumi kulikoni?

kaburungu

JF-Expert Member
Mar 9, 2011
3,602
6,632
Huhitaji uwezo mkubwa wa kufikiri na kung'amua kuwa kampuni iliyopewa kazi ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Tanga kupitia Turiani, Dumila, Kilosa na hatimae Mikumi inafanya kazi kwa mwendo wa kinyonga.! Hii ni kwa sababu tangu wameanza kazi mwaka jana ni mwaka mzima na miezi kadhaa, na kwa kweli kinachoendelea ni kiini macho.! Kwa maoni yangu kampuni hii kwa vyovyote vile itakuwa cheap! Na ndo maana wakapewa tenda.. Watumiaji wa barabara hii hususan wanaosafiri kutoka Dumila kwenda Kilosa wanaendelea kutaabika kutokana na ubovu wa barabara hasa kipindi hiki cha mvua. Umbali wa kusafiri dk 45 unatumia takribani saa nne.! Je haya ndo maisha bora? Dr Magufuli fanya ziara ya ghafla uone madudu yanayofanywa na hawa wachina.
Source: Eye witness
 
Back
Top Bottom