Anacheza mchezo wa hovyo. Hivi ikitokea huyo aliyembeba akaamua kumbwaga na kunyakua bunduki hali itakuwaje? Hata hivyo kosa si lake ni la wale waliompitisha kuwa askari. Askari wetu ni dhaifu sana kiasi cha kutumiwa na wanasiasa wachafu kulinda uchafu wao. Pamoja na watanzania kuwa kondoo hata jeshi letu nalo ni mbuzi. Hawana maana. Wanatumiwa kufanya vitu vya kipumbavu sambamba na jeshi la polisi. Kwa mfano, utasikia wanajeshi wakipiga watu kwa kugombea mabibi na upuuzi wengine huku askari wetu wakiongoza kwa kuua watu kwenye idara zote za serikali. Ajabu wanaua wachovu na kuwagwaya mafisadi. Wamenyonywa hata buti hawana lakini hawalioni hili! Angalia kanda mbili alizovaa huyo mjeshi mchovu.
Hii Si Tanzania itakuwa ni congo ndio kuna askali wanatembea na silaha hovyo na wamevaa viatu visivyo vya kiusalama...ushaona wapi askali wa kibongo kabeba siraha na viatu kama hivyo.
Lowassa alisema kuwa tuko tayari kwa vita !! Vita vyenyewe ni ya kugombea mpaka kwenye ziwa Nyasa (kwenye maji).
Sasa kwa mwendo huu, nachelea kusema kuwa Malawi wameshashinda vita hata kabla vita yenyewe haijaanza!!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.