Huyu George Maratu wa ITV style yake ya utangazaji ikoje?

Yaani katika watangazaji naowapenda wakitangaza nia Joooooooooooooooojiiiiiiiiiiiiii Marato wa Aiiiiiiiiiiiii tiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii viiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii

Na Masako huwa napenda sana wakitangaza sio unatangaza kama unasoma taarifa kama ulikariri ai
 
Ni ulimbukeni tu hana jipya. Hivi akiwa anaongea na mkewe nyumbani au anatoa maagizo kwa mwanawe asubuhi anaongea hivyo?
Mbona watangazaji na waigizaji wengi, hasa wa kike, wanapenda kuongelea puani kama vile ni wazungu? Hiyo ni professional identity. Kila mtu akisikia anajua huyo ni Marato. Bibie ana wivu wa ki..............
 
Hii sio style yake amemuiga mtangazaji mmoja wa Radio moja ya FM Kenya inatangaza kutokea maeneo ya Kisiii. Nimesahau jina la hiyo radio stesheni. Hio radio yule Mghaka wa vitimbwi anakuwa na kipindi kama kile cha Power Breakfast. Ukimsikia huyo mtangazaji utajua wapi Maratu aliiga hiyo sauti. Yeye ndo aliiga maana yeye alikuwa sio mtangazaji wa radio wala TV, wakati wa Kenya yupo Radioni toka 1980's
Kuna tatizo kuiga jambo mbalo unavutiwa nalo? Wakati mwingine kuiga ni kujifunza.
 
angekuwa sio maarufu hata ze comedy wasingemuiga, hiyo ni staili yake mbona humsemei Alfedi Masako?
kila mtu na namna yake eya utangazaji wapo wakongwe kama david wakati, kina mbotela, fredi machokaa nk wanakubalika na utabulisho wao ni namna wanavotangaza.
yale yale ya mwanao anataka kuwa muimbaji au msanii unamzuia kisa wadhani ni uhuni kumbe kila mtu kazaliwa na kipaji
MURAAAAAAA PIGA KAZI BABA WENYE WIVU WAKAJINYONGE.

Si ongelei umaarufu wake huo hauna shaka kabisa, ni maarufu sana tu na ndio maana namuongelea kwa huo umaarufu wake. Kwa hiyo anamuiga Masako?
 
nikiripoti kutoka kiabakari musomaaaa..mimi ni jojii maratu wa itviiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
Sio siri jamaa anakera sana mie huwa simsikilizi kabisa yaani ikitokea naangalia taarifa ya habari wakasema wanaleta habari za kanda ya ziwa nahamisha maana jamaa ananichefua.
 
Dada yangu FaizaFox, kumbe na wewe ni wa juzi juzi tuu enzi hizi za TV na stesheni kibao za redio?!.

Hiyo ni indentity yake kama Masako, mimi nampenda na namkubali sana, ukiondoa kumtangaza mmbunge mmoja tuu wa Musoma, Mhe. Nimrodi Mkono, kupita kiasi, najua ni kwa sababu ya mkono mrefu!.

Sisi wa zamani tunakumbuka enzi za Ben Kiko alikuwa na signature yake!, Bati Kobwa naye alikuwa na yake, David Wakati kwenye Nipe Habari, naye alikuwa na yake, kina Uncle J, Charle Hilary etc nao wana signature identies zao, mwache
"Mimii ni George.. Maratu, naaa Aiii ...Tiii .. Viii!" I like it!

Identity na signature za watangazaji ni sauti zao za asili, kila binadam ana sauti yake ya asili ambayo inampa signature yake na kuiongezea inakuwa hujiamini na inakuwa ni mchezo wa kuigiza, wewe ni mtangazaji na ilikuwa inatakiwa hili la uasilia wa sauti ulijuwe vizuri sana.

Hao uliowataja wote walikuwa hawaongezei maneno mpaka inafikia unaemsikiliza unafikiri kuwa unasikiliza "gramophone" na linataka lifanyiwe "winding" nadhani kama uliwahi kuyatumia haya utanielewa kwa huu mfano.

Nawakumbuka sana na walikuwa na uasilia na signature zao na si kama Maratu anaongezea kama ni muigizaji, kumbuka yule si muigizaji {actor), ni "reporter".
 
Hapa ni mwenye namba ya huyo bwana aitundike hapa halafu tupige kura kupitia simu yake yaangi sms zinazokubali au kukataa utangazaji wake halafu apime mwenyewe.

I miss Ben Kiko RTD Kanda ya Kati RIP.
 
good one ... next time do some little respect to what they do and who they chose to be. I mean mind your own business
napenda majibizano yenu,natamani muendelee.raha sana kwa mwanaume kuona watoto wa kike wakijibisahana.lol
 
Mbona watangazaji na waigizaji wengi, hasa wa kike, wanapenda kuongelea puani kama vile ni wazungu? Hiyo ni professional identity. Kila mtu akisikia anajua huyo ni Marato. Bibie ana wivu wa ki..............

Imedihirika kuwa ni wengi tu hawapendezewi, na hao wote wana wivu?

Usichange kati ya "waigizaji" na "watangazaji" na "reporter" hizo ni kazi tofauti na kila moja ina namna zake. "reporter" anatakiwa a "report" na asiigize. "Muigizaji" umeshaona anaitwa muigizaji hakuna cha ajabu katika kuigiza. "Mtangazaji" inategemea anatangaza nini, Taarifa ya habari, Mpira, sasa mwambie masakao akatangaze mpira kama utausikiliza tena akitangaza, itakuwa ni "tunamuona Kiiiiibaaaaadddeeeeeennnnnnnnnn anapiiiigaaaa chengaaaaaaaaa" ukitahamaki goli tayari yeye bado hajamalizia kwenye chenga.
 
Acha mzee wa watu na tone yake kwani imeathiri nini katika ukuaji wa kiswahili,angekuwa anapotosha ningesema kitu.
 
Mimi sijaelewa hasa kinachokukera. Je ni pale anapomalizia habari kwa kujitambulisha ("mimi ni joooooji maaaratuu wa aaai tiii viiii"!)? Ama ni usomaji/usimuliaji wake mzima wa habari?

Binafsi na kwa hakika watu wengi ninaowafahamu huwa wanafurahia kile kibwagizo chake cha mwisho (anavyojitambulisha)!...ni kama brand yake hivi!

Si mwisho tu, ni kila anapomalizia sentensi anakuwa kama "gramophone" linalotaka kuwa "rewound" na kubadilishwa sindano. Ukiyajuwa haya utajuwa nasema nini.
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Back
Top Bottom