Huwezi kufanikiwa, sababu hujui kudhibiti matamanio yako

Amani Dimile

JF-Expert Member
Jul 27, 2022
243
395
George Clason mwandishi wa kitabu cha The Richest Man in Babylon, anasema kwamba watu wengi hawawezi endelea kamwe maana hawajui kabisa umuhimu wa akiba lakini pia huwa wanajifanya wana matumizi makubwa hasa ya vitu ambavyo wao huona ni mahitaji ya lazima.

Lakini ukweli ni kwamba sisi wenyewe huwa tunashindwa kutofautisha kati ya matumizi ya lazima na matamanio.

Clason anaendelea kusema kwamba, matamanio ya mtu huongezeka kadri ambavyo kipato chake huongezeka. Yaani kama huwezi kujizuia nafsi yako dhidi ya vitu ambavyo ni vya matamanio basi fedha zako zitazidi kupukutika bila kujua sababu kuu.

Robert Kiyosaki ndani ya kitabu chake cha 'Rich Dady, poor Dady' aliwahi kusema ujinga wa watu ni kwamba mahitaji yao huongezeka kadri ambavyo fedha anazopata zikiongezeka. Yaani ikiwa mtu ana uwezo wa kula elfu 2 Kwa siku chakula tu na akashiba basi ukianza kumpa elfu 3 badala atumie ile ile elfu 2 na kusave buku basi ataanza kutumia elfu 3 yote yaani ataongeza mahitaji mengine huenda hata akaongeza soda ambayo hapo awali alikuwa hanunui. Jifunze kudhibiti matumizi yako, kamwe usinunue mahitaji mengine ya ziada kisa tu fedha ipo TUNZA.

Kila mtu ana matamanio mengi ambayo hawezi kuyatimiza lakini shauku ya hayo matamanio huwa kubwa kadri ambavyo kiwango cha kipato chake huongezeka.

Sijui kama naeleweka . Ila George Clason anagongelea msumari na kusema kwamba Ili uweze kumudu fedha zako, basi ni lazima ujiwekee kikomo. Kikomo cha vitu unavyoweza kununua, kikomo cha unachoweza kula, kikomo cha safari unazoweza kusafiri, kikomo cha maisha unayoishi na ujitahidi usivuke hapo.
Endapo usipoweka kikomo basi utajikuta unaishi maisha nje ya kiwango cha fedha zako, na hapo neno mafanikio basi lisahau.

Ahsante kwa kunisikiliza, na samahani ikiwa nilikusumbua na hujaelewa chochote. Hayakuwa maneno yangu, yalikuwa ni maneno ya George Clason ndani ya kitabu chake cha The Richest Man in Babylon

Tamati, ikiwa hutajifunza njia ya kupata mafanikio ukiwa angali kijana basi utatumia muda wa uzee wako wote kujuta na kulia ukiwa kwenye wimbi la umaskini. The Richest Man in Babylon, (page 28)

Naitwa Amani Dimile, follow me if you can
InShot_20230713_144037006.jpg


Sent from my TECNO KE5 using JamiiForums mobile app
 
Unaweza ukajinyima ndio lkn hiyo pesa ukaja kuwekeza kwenye biashara uchwara!.. nafikiri kuna zaidi ya kujinyima pia lazima mtu uwe na akili ya namna ya kuzalisha hiyo fedha na ilete tija alasivyo kujinyima kwako unakuja kuangukia patupu!
 
George Clason muandishi wa kitabu cha The Richest Man in Babylon, anasema kwamba watu wengi hawawezi endelea kamwe maana hawajui kabisa umuhimu wa akiba lakini pia huwa wanajifanya wana matumizi makubwa hasa ya vitu ambavyo wao huona ni mahitaji ya lazima.

Lakini ukweli ni kwamba sisi wenyewe huwa tunashindwa kutofautisha kati ya matumizi ya lazima na matamanio.
Clason anaendelea kusema kwamba, matamanio ya mtu huongezeka kadri ambavyo kipato chake huongezeka. Yaani kama huwezi kujizuia nafsi yako dhidi ya vitu ambavyo ni vya matamanio basi fedha zako zitazidi kupukutika bila kujua sababu kuu.

Robert Kiyosaki ndani ya kitabu chake cha 'Rich Dady, poor Dady' aliwahi kusema ujinga wa watu ni kwamba mahitaji yao huongezeka kadri ambavyo fedha anazopata zikiongezeka. Yaani ikiwa mtu ana uwezo wa kula elfu 2 Kwa siku chakula tu na akashiba basi ukianza kumpa elfu 3 badala atumie ile ile elfu 2 na kusave buku basi ataanza kutumia elfu 3 yote yaani ataongeza mahitaji mengine huenda hata akaongeza soda ambayo hapo awali alikuwa hanunui. Jifunze kudhibiti matumizi yako, kamwe usinunue mahitaji mengine ya ziada kisa tu fedha ipo TUNZA.

Kila mtu ana matamanio mengi ambayo hawezi kuyatimiza lakini shauku ya hayo matamanio huwa kubwa kadri ambavyo kiwango cha kipato chake huongezeka.

Sijui kama naeleweka . Ila George Clason anagongelea msumari na kusema kwamba Ili uweze kumudu fedha zako, basi ni lazima ujiwekee kikomo. Kikomo cha vitu unavyoweza kununua, kikomo cha unachoweza kula, kikomo cha safari unazoweza kusafiri, kikomo cha maisha unayoishi na ujitahidi usivuke hapo.
Endapo usipoweka kikomo basi utajikuta unaishi maisha nje ya kiwango cha fedha zako, na hapo neno mafanikio basi lisahau.

Ahsante kwa kunisikiliza, na samahani ikiwa nilikusumbua na hujaelewa chochote. Hayakuwa maneno yangu, yalikuwa ni maneno ya George Clason ndani ya kitabu chake cha The Richest Man in Babylon

Tamati, ikiwa hutajifunza njia ya kupata mafanikio ukiwa angali kijana basi utatumia muda wa uzee wako wote kujuta na kulia ukiwa kwenye wimbi la umaskini. The Richest Man in Babylon, (page 28)

Naitwa Amani Dimile, follow me if you can View attachment 2686692

Sent from my TECNO KE5 using JamiiForums mobile app
Elimu nzuri sana, asante sana.
 
Wote wakifanikiwa utamwajiri nan
Wote wakifanikiwa papuchi za buku5 utatoa wap
Wote wakifanikiwa nan atakua chawa
Wote wote wote

Dunian kla mtu amekuja na purpose yake na sio binadamu wote wameumbiwa kufanikiwa ata ktk vitabu vya dini kuna kichwa na mikia kuna viongozi na waongozwaji kuna matajiri na kuna mafukara
Jifunze kufurahia kle Mungu amekupa km una amin ktk dini ila km huamini ktk dini bas jivunie uwezo wako wa akili na fikla ulipoishia
 
Kuna mafunzo mengi na halisia kwenye hiki kitabu. Mtu unapaswa kukisoma mara kwa mara ili kikupe makumbusho na kuweza kuwa unajiakisi.

Bila nidhamu ya fedha, kujibana na akiba ni ngumu sana kupiga hatua kiuchumi.

Kwenye jamii zetu, kuna wale watu wa kigoma-waha, wale jamaa ni kiboko kwenye kujibana.
 
Kuna mafunzo mengi na halisia kwenye hiki kitabu. Mtu unapaswa kukisoma mara kwa mara ili kikupe makumbusho na kuweza kuwa unajiakisi.

Bila nidhamu ya fedha, kujibana na akiba ni ngumu sana kupiga hatua kiuchumi.

Kwenye jamii zetu, kuna wale watu wa kigoma-waha, wale jamaa ni kiboko kwenye kujibana.
Hakika na uwe na sehemu pembeni ya ku note ili yawe makumbusho kwako.

Sent from my TECNO KE5 using JamiiForums mobile app
 
Vitabu vizuri sanaa hvyo tena sasa hvi…vpo vilivyotafsiria kwa lugha ya kiswahili…

Kuna application inaitwa maktaba…nilikuwa nayo ila baada simu yngu kuharibika na kupata simu nyengine nmejaribu kuitafuta hyo app bila mafanikiwa sijaipata…..ni app nzuri ina hcho kitabu kwa lugha ya kiswahili,

Watu wengi wanaendesha maisha yao kihasara hasa watumishi wa serikali….mtu kwa mwezi anaingiza 1Ml akitoa makato ya serikali na matumizi yake binafsi anabaki na loss/hasara laki 1….lakini ukweli ni kuwa hatuna tabia ya kufanya hzo hesabu as long as tunaona maisha yanaenda na ccm wapo madarakani..
 
Unaweza ukajinyima ndio lkn hiyo pesa ukaja kuwekeza kwenye biashara uchwara!.. nafikiri kuna zaidi ya kujinyima pia lazima mtu uwe na akili ya namna ya kuzalisha hiyo fedha na ilete tija alasivyo kujinyima kwako unakuja kuangukia patupu!
Fact
Unatafuta ela kwa mda mrefu inakuja kuisha kwa siku moja
 
Back
Top Bottom