Lukwangule
Senior Member
- May 25, 2009
- 157
- 2
Mimi sina kawaida ya kutukana watu , lakini huwa najiuliza nini maana ya kuwa na wataalamu, viongozi na wanasiasa kama kila kitu kinakwama kinahitaji msimamo wa kiongozi mkuu?
Kuna kitu kinanikera sana kuhusu suala la kuimarisha upatikanaji wa umeme katika mkoa wa dar es salaam.
Wajep wametupatia fedha mabilioni kuimarisha mfumo na ipo kampuni yao inatengeneza njia kwa ajili ya kupeleka umeme katika kituo kidogo pale usalama wa taifa (mkabala) kutoka Ubungo.
Umeme ule unatakiwa kupelekwa Temeke kuimarisha upatikanaji wa umeme na maeneo mengine ya jiji hili. Lakini hawa jamaa waliopewa zabuni ya kusuka nguzo za umeme kupeleka pale huenda wakarejea na fedha zao Japan kama huu ninaouita upuuzi hautaangaliwa na kuondolewa mapema.
Kwanza fedha zenyewe si zetu na kampuni si yetu na sisi ndio wenye shida anatokea mtu mmoja anazuia umeme usipite eneo la tanroad eti kwa dai kuwa watu wake wanaosali wataharibikiwa.
Ule umeme lazima tuupitishe pale, yeye kanisa anaweza kuhamisha, kama alikuwa anajua kwamba yupo katika eneo karibu kabisa na reserve ya Tanroad basi ajue na athari zake. maeneo hayo ndiyo yanayopitisha mabomba na vitu vingine vya jamii, kwanini kaleta karibu namna ile kanisa lake?Pili mbona hizo nguzo zinainamia kwingine wala hazina uhusiano na yeye. mawasiliano gani duniani hapa anadhani yataharibiwa kwa kuwa karibu na nguzo zile?
Kuna nguzo zinasafiri kutoka kidatu zinabeba msongo mkubwa kabisa, wote tunajua umbali wake, wale wapogoro wakatae nini? Tuache hayo!
Mimi najiuliza Ngeleja anafanya nini hasa kuhusiana na suala hili au anaogopa serikali ya CCM haitapata kura kwa kumshauri anayehusika atuache tupitishe nguzo zetu kwani muda unakwenda na Wajapan hawatuelewi? Lakini kwa mitaji hii ya umeme wa kubabaisha si lazima tuwaondoe madarakani tu?
Nina hasira sana kwani kule temeke kunakatikakatika hovyo umeme na huyu kakobe anadai kwamba lile eneo likipitishwa umeme wananchi wake watafadhaika halafu watashindwa kutekeleza majukumu yao ya kijamii. kama kweli apewe neno limuingie.Sawa apewe kiwanja kingine akajenge kama inaonekana anaonewa. Asisahau kuwa umeme ule unataka kusaidia eneo maskini kabisa ambalo zamani aliishi nyakati hizo ambazo sina sababu zozote zile za kuzitaja. Mimi nataka atuachie nafasi tupitishe umeme.
Si suala la kututisha na Mungu. Mungu ni wetu na alituambia tuyatumie vyema majambo haya ya dunia ili kufika kwake. Umeme wa kubahatisha ndio unaomaliza miti kwa kutengeneza mikaa na ndio unaangamiza dunia kwa kuondoa kinasa kaboni.(miti).
Mimi nasema kwa kukasirika sana kwani haya mavitu tunayalealea tu. Huyo aliyechora amekuwa chizi? hana akili? mwendawazimu?Kichaa au punguani? Kama ni mtaalamu huyu mwingine ambaye naye hakusomea utaalamu anasema nini hasa? Anasema anao wataalamu. sawasawa kila dhehebu lina wataalamu. Wale wa kanisa la wakatoliki Msimbazi nao wanahaki ya kupiga kelele basi. Wana kitu kinachoongoza ndege magneti ile au sio . Huyu anayesema vipaza sauti vyake vitazidi anataka kutueleza nini? pale katika kona ya Tazara kuna substation basi Radio Tanzania wangelisema iondolewe inavuruga utaratibu.
Tusidanganyane bwana.
Si sumaku wala si umeme. mainjinia wanaofua umeme huo basi wangelikosa urijali .
Narudia tena Sijui kwanini viongozi inapofika wakati wa uchaguzi huwa hawafanyikazi zao sawasawa, nini woga wa kunyimwa kura? Mimi nadhani hili wala si jambo.Watu wanasema tu kama serikali haipo. Kama uongozi haupo? Nini maana yake hata shauri la kanisa linahitaji miniti za kabineti? ili iweje huu mradi wa kuboresha umeme dar urejee kwa wajep wenyewe nini? sisi kama si wehu tuna kasoro ya kuzaliwa kama vyote havipo tuna shida kubwa kwelikweli.
Kuna kitu kinanikera sana kuhusu suala la kuimarisha upatikanaji wa umeme katika mkoa wa dar es salaam.
Wajep wametupatia fedha mabilioni kuimarisha mfumo na ipo kampuni yao inatengeneza njia kwa ajili ya kupeleka umeme katika kituo kidogo pale usalama wa taifa (mkabala) kutoka Ubungo.
Umeme ule unatakiwa kupelekwa Temeke kuimarisha upatikanaji wa umeme na maeneo mengine ya jiji hili. Lakini hawa jamaa waliopewa zabuni ya kusuka nguzo za umeme kupeleka pale huenda wakarejea na fedha zao Japan kama huu ninaouita upuuzi hautaangaliwa na kuondolewa mapema.
Kwanza fedha zenyewe si zetu na kampuni si yetu na sisi ndio wenye shida anatokea mtu mmoja anazuia umeme usipite eneo la tanroad eti kwa dai kuwa watu wake wanaosali wataharibikiwa.
Ule umeme lazima tuupitishe pale, yeye kanisa anaweza kuhamisha, kama alikuwa anajua kwamba yupo katika eneo karibu kabisa na reserve ya Tanroad basi ajue na athari zake. maeneo hayo ndiyo yanayopitisha mabomba na vitu vingine vya jamii, kwanini kaleta karibu namna ile kanisa lake?Pili mbona hizo nguzo zinainamia kwingine wala hazina uhusiano na yeye. mawasiliano gani duniani hapa anadhani yataharibiwa kwa kuwa karibu na nguzo zile?
Kuna nguzo zinasafiri kutoka kidatu zinabeba msongo mkubwa kabisa, wote tunajua umbali wake, wale wapogoro wakatae nini? Tuache hayo!
Mimi najiuliza Ngeleja anafanya nini hasa kuhusiana na suala hili au anaogopa serikali ya CCM haitapata kura kwa kumshauri anayehusika atuache tupitishe nguzo zetu kwani muda unakwenda na Wajapan hawatuelewi? Lakini kwa mitaji hii ya umeme wa kubabaisha si lazima tuwaondoe madarakani tu?
Nina hasira sana kwani kule temeke kunakatikakatika hovyo umeme na huyu kakobe anadai kwamba lile eneo likipitishwa umeme wananchi wake watafadhaika halafu watashindwa kutekeleza majukumu yao ya kijamii. kama kweli apewe neno limuingie.Sawa apewe kiwanja kingine akajenge kama inaonekana anaonewa. Asisahau kuwa umeme ule unataka kusaidia eneo maskini kabisa ambalo zamani aliishi nyakati hizo ambazo sina sababu zozote zile za kuzitaja. Mimi nataka atuachie nafasi tupitishe umeme.
Si suala la kututisha na Mungu. Mungu ni wetu na alituambia tuyatumie vyema majambo haya ya dunia ili kufika kwake. Umeme wa kubahatisha ndio unaomaliza miti kwa kutengeneza mikaa na ndio unaangamiza dunia kwa kuondoa kinasa kaboni.(miti).
Mimi nasema kwa kukasirika sana kwani haya mavitu tunayalealea tu. Huyo aliyechora amekuwa chizi? hana akili? mwendawazimu?Kichaa au punguani? Kama ni mtaalamu huyu mwingine ambaye naye hakusomea utaalamu anasema nini hasa? Anasema anao wataalamu. sawasawa kila dhehebu lina wataalamu. Wale wa kanisa la wakatoliki Msimbazi nao wanahaki ya kupiga kelele basi. Wana kitu kinachoongoza ndege magneti ile au sio . Huyu anayesema vipaza sauti vyake vitazidi anataka kutueleza nini? pale katika kona ya Tazara kuna substation basi Radio Tanzania wangelisema iondolewe inavuruga utaratibu.
Tusidanganyane bwana.
Si sumaku wala si umeme. mainjinia wanaofua umeme huo basi wangelikosa urijali .
Narudia tena Sijui kwanini viongozi inapofika wakati wa uchaguzi huwa hawafanyikazi zao sawasawa, nini woga wa kunyimwa kura? Mimi nadhani hili wala si jambo.Watu wanasema tu kama serikali haipo. Kama uongozi haupo? Nini maana yake hata shauri la kanisa linahitaji miniti za kabineti? ili iweje huu mradi wa kuboresha umeme dar urejee kwa wajep wenyewe nini? sisi kama si wehu tuna kasoro ya kuzaliwa kama vyote havipo tuna shida kubwa kwelikweli.