ndugu wana jf, jana kuna tangazo lililetwa hapa jamvini na kampuni moja inajiita plusfinance wakasema kwamba wanahitaji watu kwa ajili ya business planing training ambayo itafanyika tarehe 26/27 mwezi huu.kwa kuwa waliweka namba za simu nikaamua kuwapigia kwenye namba hii 0687024164 nikaongea na mmoja wa wahudumu na kuniambia nitume cv yangu na watanipa maelekezo.leo saa 10.00am wamenitumia sms kwenye simu yangu wakiniambia kuwa nahitajika kulipa sh 50000 kama ada ya kuhudhuria kwenye training hiyo na nilipe kabla ya tarehe 25 mwezi huu sehemu ya kulipa ni PFL located at IDEAL HOTEL 1st floor Faya area behind Exim bank.namba ya aliye nitumia hiyo sms ni 0758921404.naombeni ushauri mimi pamoja na wengine wote ambao hawafahamu ujanja wa huu mji.asanteni.