Kashaijabutege
JF-Expert Member
- Oct 20, 2010
- 2,696
- 740
Cheche huzaa moto.
Nadhani, mbali na mambo mengine, hukumu mbovu ya Mwakibarila imechangia wananchi kuzidi kuichukia CCM. Inawezekana CCM waliweka mkono wao ili Jaji atende alivyotenda bila kujua athari zake. Sasa hivi CCM hakitamani kuwepo kwa uchaguzi mdogo Arusha. Nakuapia, hawautaki kabisa. Na hakika, moto huu utaenea nchi nzima. CCM kilifikiri CHADEMA ni Godbless Lema; kumbe sivyo.
Ogopa nguvu ya umma. Ogopa watu wenye hasira.
Arusha sasa wanakiona CCM kama kibaka. Wananchi wenye hasira wanataka kukichoma moto. Matairi, petroli na viberiti viko tayari; kilichobaki ni kumsubiri kibaka tu. Unachomwa baada ya kula kichapo; Arumeru Mashariki wamekipa kichapo kwanza; kisha watakimwagia wese; watakivika tairi; watakichoma.
Sala yangu imepaa. Mungu ameiumbua CCM mchana kweupe. Mungu usinichukue kabla ya kuona angamio la CCM. Amina.
Nadhani, mbali na mambo mengine, hukumu mbovu ya Mwakibarila imechangia wananchi kuzidi kuichukia CCM. Inawezekana CCM waliweka mkono wao ili Jaji atende alivyotenda bila kujua athari zake. Sasa hivi CCM hakitamani kuwepo kwa uchaguzi mdogo Arusha. Nakuapia, hawautaki kabisa. Na hakika, moto huu utaenea nchi nzima. CCM kilifikiri CHADEMA ni Godbless Lema; kumbe sivyo.
Ogopa nguvu ya umma. Ogopa watu wenye hasira.
Arusha sasa wanakiona CCM kama kibaka. Wananchi wenye hasira wanataka kukichoma moto. Matairi, petroli na viberiti viko tayari; kilichobaki ni kumsubiri kibaka tu. Unachomwa baada ya kula kichapo; Arumeru Mashariki wamekipa kichapo kwanza; kisha watakimwagia wese; watakivika tairi; watakichoma.
Sala yangu imepaa. Mungu ameiumbua CCM mchana kweupe. Mungu usinichukue kabla ya kuona angamio la CCM. Amina.