mlekulechoma
JF-Expert Member
- Nov 2, 2014
- 1,367
- 1,057
Suala la afya kwa wananchi wa Tanzania hususani wa kipato cha chini limeendelea kuwa na changamoto kila kukicha!ni jambo la kawaida kusikia hospitali zetu zote kuanzia Muhimbili ambayo ndiyo hospitali kuu ya taifa hadi kwenye zahanati zetu huko vijijini kwamba hakuna dawa za kutosha pia vifaa tiba hakuna!
Mgomo wa madaktari ambao ulipelekea kuteswa na kuumizwa vibaya karibu na kifo kwa kiongozi wa jumuiya ya madaktari Dr. Ulimboka ninaamini bado unaendelea ila kwa mtindo tofauti!
Siku hizi wataalam wetu hawa wa afya hawafanyi kazi kwa moyo wa wito kama zamani! Nilibahatika kuongea na daktari mmoja mwandamizi wa hospitali kubwa hapa nchini kuhusiana na suala hili, alisema mgomo wao ulikuwa ni kudai maboresho ya huduma za afya na wafanyakazi katika sekta hiyo kwa ujumla.Majibu ya Rais yaliwakatisha tamaa sana.
Alisema anaetaka kazi afanye na siyetaka aache!Kinachoendelea sasa ndio matokeo ya mgomo huo na majibu ya Rais wa nchi.
Wataalam hawana muda wa kutafuta vifaa tiba/dawa katika hospitali zetu!
Wengi wa wataalam wetu wanavijiwe vyao hawana muda na hospitali zetu!
Baadhi yao wameingia kwenye mashirika binafsi hivyo kupelekea upungufu mkubwa wa wataalam katika sekta ya afya!!
Waliobaki hawana morali ya kazi,wanasubiri mshahara siku ziende!
Je, nini kifanyike kunusuru maisha ya watanzania wenzetu hasa wa kipato cha chini?
Mgomo wa madaktari ambao ulipelekea kuteswa na kuumizwa vibaya karibu na kifo kwa kiongozi wa jumuiya ya madaktari Dr. Ulimboka ninaamini bado unaendelea ila kwa mtindo tofauti!
Siku hizi wataalam wetu hawa wa afya hawafanyi kazi kwa moyo wa wito kama zamani! Nilibahatika kuongea na daktari mmoja mwandamizi wa hospitali kubwa hapa nchini kuhusiana na suala hili, alisema mgomo wao ulikuwa ni kudai maboresho ya huduma za afya na wafanyakazi katika sekta hiyo kwa ujumla.Majibu ya Rais yaliwakatisha tamaa sana.
Alisema anaetaka kazi afanye na siyetaka aache!Kinachoendelea sasa ndio matokeo ya mgomo huo na majibu ya Rais wa nchi.
Wataalam hawana muda wa kutafuta vifaa tiba/dawa katika hospitali zetu!
Wengi wa wataalam wetu wanavijiwe vyao hawana muda na hospitali zetu!
Baadhi yao wameingia kwenye mashirika binafsi hivyo kupelekea upungufu mkubwa wa wataalam katika sekta ya afya!!
Waliobaki hawana morali ya kazi,wanasubiri mshahara siku ziende!
Je, nini kifanyike kunusuru maisha ya watanzania wenzetu hasa wa kipato cha chini?