Hotuba yangu kwenye Kongamano la Katiba Day

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Dec 22, 2010
16,987
20,271
Salamu zangu kwenye Kongamano la Katiba Day
01/07/2021.

Ndugu Mgeni Rasmi Mh Freeman Aikael Mbowe Mwenyekiti wa Chadema Taifa.

Mheshimiwa John Mnyika Katibu Mkuu Chadema Taifa

Watoa Mada wakuu Prof Rwaitama na Askofu Emmanuel Mwamakula.

Wageni waalikwa wote na vijana wenzangu, itifaki imezingatiwa!

Walionitangulia wamezungumza mengi mazuri kwa mstakabali wa mchakato wetu wa Katiba Mpya.

Mimi ninaomba nizungumze jambo moja muhimu ambalo linaukabili mchakato huu tangu ulipoanza Mwaka 2011. Na jambo hilo ni Mitazamo tenge juu ya Katiba Mpya.

Lakini kabla sijaanza kueleza mitazamo hiyo naomba niwaeleze vijana wenzangu, Sisi Vijana tuliopo hapa hatujawahi kuandika Katiba ya Tanzania, Wazazi wetu na pia viongozi wetu mliopo hapa hamjawahi kuandika katiba ya Tanzania, Mababu zetu pia hawakuandika katiba ya Tanganyika wala katiba ya Zanzibar.

Katiba ya mkoloni iliandikwa na watu wachache (6) tu ndani ya ofisi ya Ukoloni Mjini London Uingereza 1919. Ifahamike kuwa huko nyuma kabla ya vita vya kwanza vya dunia alivyoshinda Muingereza, alikuwepo Mjerumani ambae aliitawala Tanganyika kama Kampuni na kuiongoza kama Kampuni la faida kwakutumia MoU badala ya katiba. Ingawa kwa mwaka mmoja wa 1919 nchi yetu iliitwa majina 9. Ambapo, Kwanza iliitwa Smutsland, Pili ikaitwa Eburnea, Tatu ikaitwa Azania, Nne ikaitwa New Maryland, Tano ikaitwa Windsorland, Sita ikaitwa Victoria, Saba ikaitwa Kilimanjaro , Nane ikaitwa Tabora na hatimaye jina la Tisa ikaitwa Tanganyika January 1920.

Katiba ya Tanganyika huru licha ya kuirithi Katiba ile katiba ya kikolini lakini kwa sehemu kubwa ilitokana na msingi wa katiba ya TANU, ambayo nayo msingi wake ni katiba ya chama cha AA iliyoandikwa na raia wa Gold Coast Dr James Emman Kwegyir Aggrey 1927. Chama cha AA rais wake Mwasusu akiwa Mwalimu Cecil Matola.

Lakini pia Mwalimu Julius Nyerere wakati wakiunda chama cha TANU 1954 walilazimika kuazima sehemu ya katiba ya chama cha CCP cha Ghana chini ya Dr Kwame Nkurumah.
Hadi hapo mtaona Katiba ya Tanganyika wala Tanzania haikuwahi kuandikwa na Wananchi bali watu wachache waliandika kwa niaba ya wengi, huu ulikuwa mfumo wa kale ambako dunia leo haiko huko, Leo dunia ni shirikishi na ya kidemokrasia.

Kwa mara ya kwanza 2013 Watanzania tulishiriki kuanza kuandika katiba mpya, na kwa sehemu tu hatua tulishaivuka kwakutoa maoni yakwamba tunataka katiba ya aina gani kupitia Tume ya Jaji Warioba. Maoni yale ndio ushiriki wetu kamili na thabiti kwaajili ya Katiba Mpya.

Dhana tata juu ya Katiba Mpya

Baada ya Maoni na mchakato kuanza wa Katiba Mpya, Ziliibuka dhana tata nyingi sana, zikianzia kwenye kutunga sheria ya mchakato wa Katiba Mpya, Kwenye Kanuni za Bunge la Katiba na mitazamo mingine imeendelea kuwepo hadi leo. Nitaorodhesha kwa uchache kama mifano hai.

1. Katiba Mpya itaiondoa ccm madarakani

2. Katiba Mpya itaisaidia Chadema kwenda Ikulu

3. Katiba Mpya itamuondolea rais Madaraka

Dhana hizi zote tunao wajibu wa kuzifafanua na kuwaelimisha wenzetu wanaojenga dhana hizi potofu.

Dhana kwamba Katiba Mpya itaiondoa ccm Madarakani ni dhana potofu kwakuwa Katiba mpya ni mstakabali wa kitaifa kati ya watawala na watawaliwa, ni mstakabali juu ya wakulima, Ni mstakabali juu ya wafanyakazi, Ni mstakabali juu ya wavuvi nk. Mstakabali huu hauhusu kundi la SIASA tu bali nchi nzima.

Dhana kwamba Katiba Mpya itaisadia Chadema kwenda ikulu, ni dhana mfu, na kama kuna yeyote miongoni mwetu hapa anafikiri hivyo namuombeni afute mawazo hayo, Tukikifikiri katika muono huo kamwe hatutapata katiba ambayo ndio mstakabali wa taifa lote na sio mstakali wa Chadema wala wa ccm tu.

Dhana kwamba Katiba mpya itamuondolea Rais Madaraka, Si kweli, bali Katiba Mpya itapunguza madaraka ya rais ya sasa na kumwekea misingi imara ya kuongoza nchi kama rais kuliko ilivyo sasa anavyoongoza kama mfalme. Katiba ya sasa inasema, Katika kutekeleza madaraka yake, Rais hatasikiliza wala hatashauriwa na mtu yoyote au kikundi chochote,

Katiba mpya itaweka sawa eneo hilo na kutomfanya Rais kuwa Mungu-Mtu.

Ni wajibu wetu vijana nchi nzima bila kujali chama ama itikadi, kuongoza vuguvugu hili kuhakikisha mchakato wa katiba mpya unaanzia kwenye Rasimu ya Jaji Warioba.

Asanteni sana vijana wenzangu!

Na Yericko Nyerere
FB_IMG_1625170694078.jpg
 
Sawa kamanda kwa hotuba yako nzuri pamoja na kuwa nimekusikia ukishindwa kutamka neno kampuni ila hoja yako ilikinzana na hoja ya makam mwenyekiti ndugu lisu juu ya mwaka wa kuanza kutumia katiba ya kwanza
Pili ningefurahi pia kupata hotuba ya mdude nyagari msomi mzuri na msafwa mwenzangu
 
Na dhana nyingine ambayo watu wanatakiwa waiondoe ni kwamba katiba mpya sio maendeleo.

Kitendo tu cha kua na katiba mpya ni maendeleo makubwa katika demokrasia yetu.
Chadema wanataka katiba mpya kwa ajili tu wao wapate fever

Ndio maana wanakazania katiba mpya na tume huru

Hiyo tume inakuwa sio huru kama wao wakishindwa ila kama wakishinda basi ni tume mzuri

Muhimu kwa serikali now ni kuweka mazingira ya kuhoji Watanzania kama wanakubali or not

Im very sure Watanzania wengi hawataki hiyo katiba
 
Chadema wanataka katiba mpya kwa ajili tu wao wapate fever

Ndio maana wanakazania katiba mpya na tume huru

Hiyo tume inakuwa sio huru kama wao wakishindwa ila kama wakishinda basi ni tume mzuri

Muhimu kwa serikali now ni kuweka mazingira ya kuhoji Watanzania kama wanakubali or not

Im very sure Watanzania wengi hawataki hiyo katiba
Katiba mpya itaweka balance ya harakati za kiuchumi, kijamii na kisiasa. Kwenye uzani huu Chadema lazima waibuke kidedea hili hatuhitaji kujadili sana
 
Yericko Nyerere unakuwaje na guts ya kupost hotuba yako binafsi badala ya hotuba ya chama? Kwani CDM haikuwa na hotuba yake? Wewe ni mkubwa kuliko chama? Hii ndo ile kitu Lowasa aliitaga 'Chadema kila mtu ana sharubu'. Siyo sahihi! Personally siwezi kusoma hotuba ya MC. Tunahitaji hotuba ya Mwenyekiti wa CFM Taifa not otherwise.
 
Chadema wanataka katiba mpya kwa ajili tu wao wapate fever

Ndio maana wanakazania katiba mpya na tume huru

Hiyo tume inakuwa sio huru kama wao wakishindwa ila kama wakishinda basi ni tume mzuri

Muhimu kwa serikali now ni kuweka mazingira ya kuhoji Watanzania kama wanakubali or not

Im very sure Watanzania wengi hawataki hiyo katiba
Mimi ni miongoni mwa watanzania tunaohitaji katiba mpya.
 
Hotuba yangu kwenye Kongamano la Katiba Day
01/07/2021.

Ndugu Mgeni Rasmi Mh Freeman Aikael Mbowe Mwenyekiti wa Chadema Taifa.

Mheshimiwa John Mnyika Katibu Mkuu Chadema Taifa

Watoa Mada wakuu Prof Rwaitama na Askofu Emmanuel Mwamakula.

Wageni waalikwa wote na vijana wenzangu, itifaki imezingatiwa!

Walionitangulia wamezungumza mengi mazuri kwa mstakabali wa mchakato wetu wa Katiba Mpya.

Mimi ninaomba nizungumze jambo moja muhimu ambalo linaukabili mchakato huu tangu ulipoanza Mwaka 2011. Na jambo hilo ni Mitazamo tenge juu ya Katiba Mpya.

Lakini kabla sijaanza kueleza mitazamo hiyo naomba niwaeleze vijana wenzangu, Sisi Vijana tuliopo hapa hatujawahi kuandika Katiba ya Tanzania, Wazazi wetu na pia viongozi wetu mliopo hapa hamjawahi kuandika katiba ya Tanzania, Mababu zetu pia hawakuandika katiba ya Tanganyika wala katiba ya Zanzibar.

Katiba ya mkoloni iliandikwa na watu wachache (6) tu ndani ya ofisi ya Ukoloni Mjini London Uingereza 1919. Ifahamike kuwa huko nyuma kabla ya vita vya kwanza vya dunia alivyoshinda Muingereza, alikuwepo Mjerumani ambae aliitawala Tanganyika kama Kampuni na kuiongoza kama Kampuni la faida kwakutumia MoU badala ya katiba. Ingawa kwa mwaka mmoja wa 1919 nchi yetu iliitwa majina 9. Ambapo, Kwanza iliitwa Smutsland, Pili ikaitwa Eburnea, Tatu ikaitwa Azania, Nne ikaitwa New Maryland, Tano ikaitwa Windsorland, Sita ikaitwa Victoria, Saba ikaitwa Kilimanjaro , Nane ikaitwa Tabora na hatimaye jina la Tisa ikaitwa Tanganyika January 1920.

Katiba ya Tanganyika huru licha ya kuirithi Katiba ile katiba ya kikolini lakini kwa sehemu kubwa ilitokana na msingi wa katiba ya TANU, ambayo nayo msingi wake ni katiba ya chama cha AA iliyoandikwa na raia wa Gold Coast Dr James Emman Kwegyir Aggrey 1927. Chama cha AA rais wake Mwasusu akiwa Mwalimu Cecil Matola.

Lakini pia Mwalimu Julius Nyerere wakati wakiunda chama cha TANU 1954 walilazimika kuazima sehemu ya katiba ya chama cha CCP cha Ghana chini ya Dr Kwame Nkurumah.
Hadi hapo mtaona Katiba ya Tanganyika wala Tanzania haikuwahi kuandikwa na Wananchi bali watu wachache waliandika kwa niaba ya wengi, huu ulikuwa mfumo wa kale ambako dunia leo haiko huko, Leo dunia ni shirikishi na ya kidemokrasia.

Kwa mara ya kwanza 2013 Watanzania tulishiriki kuanza kuandika katiba mpya, na kwa sehemu tu hatua tulishaivuka kwakutoa maoni yakwamba tunataka katiba ya aina gani kupitia Tume ya Jaji Warioba. Maoni yale ndio ushiriki wetu kamili na thabiti kwaajili ya Katiba Mpya.

Dhana tata juu ya Katiba Mpya

Baada ya Maoni na mchakato kuanza wa Katiba Mpya, Ziliibuka dhana tata nyingi sana, zikianzia kwenye kutunga sheria ya mchakato wa Katiba Mpya, Kwenye Kanuni za Bunge la Katiba na mitazamo mingine imeendelea kuwepo hadi leo. Nitaorodhesha kwa uchache kama mifano hai.

1. Katiba Mpya itaiondoa ccm madarakani

2. Katiba Mpya itaisaidia Chadema kwenda Ikulu

3. Katiba Mpya itamuondolea rais Madaraka

Dhana hizi zote tunao wajibu wa kuzifafanua na kuwaelimisha wenzetu wanaojenga dhana hizi potofu.

Dhana kwamba Katiba Mpya itaiondoa ccm Madarakani ni dhana potofu kwakuwa Katiba mpya ni mstakabali wa kitaifa kati ya watawala na watawaliwa, ni mstakabali juu ya wakulima, Ni mstakabali juu ya wafanyakazi, Ni mstakabali juu ya wavuvi nk. Mstakabali huu hauhusu kundi la SIASA tu bali nchi nzima.

Dhana kwamba Katiba Mpya itaisadia Chadema kwenda ikulu, ni dhana mfu, na kama kuna yeyote miongoni mwetu hapa anafikiri hivyo namuombeni afute mawazo hayo, Tukikifikiri katika muono huo kamwe hatutapata katiba ambayo ndio mstakabali wa taifa lote na sio mstakali wa Chadema wala wa ccm tu.

Dhana kwamba Katiba mpya itamuondolea Rais Madaraka, Si kweli, bali Katiba Mpya itapunguza madaraka ya rais ya sasa na kumwekea misingi imara ya kuongoza nchi kama rais kuliko ilivyo sasa anavyoongoza kama mfalme. Katiba ya sasa inasema, Katika kutekeleza madaraka yake, Rais hatasikiliza wala hatashauriwa na mtu yoyote au kikundi chochote,

Katiba mpya itaweka sawa eneo hilo na kutomfanya Rais kuwa Mungu-Mtu.

Ni wajibu wetu vijana nchi nzima bila kujali chama ama itikadi, kuongoza vuguvugu hili kuhakikisha mchakato wa katiba mpya unaanzia kwenye Rasimu ya Jaji Warioba.

Asanteni sana vijana wenzangu!

Na Yericko NyerereView attachment 1837238
Kwa heshima kubwa Tunaomba hotuba ya Mwenyekiti wako.
 
Yericko Nyerere unakuwaje na guts ya kupost hotuba yako binafsi badala ya hotuba ya chama? Kwani CDM haikuwa na hotuba yake? Wewe ni mkubwa kuliko chama? Hii ndo ile kitu Lowasa aliitaga 'Chadema kila mtu ana sharubu'. Siyo sahihi! Personally siwezi kusoma hotuba ya MC. Tunahitaji hotuba ya Mwenyekiti wa CFM Taifa not otherwise.
Kwahiyo mtu binafsi huwa hatoi hotuba? na hii akaurnt uake binafsi halazimiki kuposti hotuba za mwingine
 
Asante kwa hotuba nzuri.Ukikumbuka vizuri dhana ulizoeleza happy juu,pamoja na mambo mengine,ndizo zilizoleta mkwamo katika bunge la katiba.Rais mwenyewe alitishwa kwa kutumia dhana hizi,na bunge likajaa ushabiki wa kivyama.Kuna walioona kwamba Sasa Ccm watakoma na CCM wakakomaa kwamba hawatoitoa nchi katu.Hapa nakumbuka kauli nzito za mama Asha Bakari kutoka Zanzibar ( marehemu)alipokuwa akimshambulia Ismail Jussa.
 
Chadema wanataka katiba mpya kwa ajili tu wao wapate fever

Ndio maana wanakazania katiba mpya na tume huru

Hiyo tume inakuwa sio huru kama wao wakishindwa ila kama wakishinda basi ni tume mzuri

Muhimu kwa serikali now ni kuweka mazingira ya kuhoji Watanzania kama wanakubali or not

Im very sure Watanzania wengi hawataki hiyo katiba
Umefanya utafiti gani hadi ukasuluhu kwamba watanzania wengi hawataki katiba mpya? Suala la katiba Ni muhimu Sana,nani anataka rais aendelee kuhodhi kila mamlaka katika nchi? Nani anataka Dpp awe ndiye wa kuamua kila jambo dhidi ya watuhumiwa wa jinai katika nchi hii? Nani anataka mtuhumiwa akae miaka nane rumande bila kuhukumiwa? Ni nani anataka kuendelea kukosa haki ya kugombea uchaguzi kwakuwa tu hana chama cha siasa? Hayo ni macheche ,yapo mengi.Kama huoni Hilo Basi hata maana ya neno katiba hujui.
 
Back
Top Bottom