Hawa wamerekani watakuwa hawajui demokrasia kama chadema, wanataka kumtoa Obama, wakati uchaguzi ulisha fanyika?
Maelfu Waandamana Marekani Kupinga Serikali ya Obama
Maelfu waliojitokeza jana kupinga utawala wa Obama
Maelfu ya watu wakibeba mabango yanayopinga utawala wa rais Obama na mageuzi yake katika mfumo wa afya anayotaka kuyafanya, waliandamana jana hadi katika maeneo ya ikulu ya Marekani.
"Utoaji mimba sio mageuzi katika Afya" lilisema bango moja huku bango jingine lililobebwa na mhamiaji nchini Marekani toka Ukraine lilisema "Nilishauchoka ujamaa kwenye muungano wa soviet USSR".
Mtoto Quinn Ryan, 11, alisimama katikati ya mtaa wa Pennsylvania Avenue, karibu na sehemu ambayo Obama na mkewe Michelle walitembea siku ile yenye baridi wakati Obama alipoapishwa kuwa rais wa kwanza mweusi wa Marekani.
Ryan alikuwa amebeba bango linalosema "Nimezaliwa bure, nitalipishwa kodi mpaka nitakapofariki".
"Hali mbaya ya uchumi imeathiri nyumba nyingi, imetubidi tuandamane ili hali isiwe mbaya zaidi" alisema dada yake Ryan mwenye umri wa miaka 13 ambaye naye alikuwa amebeba bango lake tofauti.
Maandamano hayo yalilenga kupinga utawala wa rais Obama na kukishtumu chama cha democratic kwa kutaka kuigeuza Marekani nchi ya kijamaa.
Maandamano hayo yaliandaliwa Freedomworks, taasisi inayopigania kushushwa kwa viwango vya kodi na uchumi huria ikipinga mabadiliko ambayo rais Obama anataka kuyafanya katika masuala ya bima katika mfumo wa afya wa Marekani.
Waandaaji wa maanandamano hayo walisema awali katikati ya wiki kuwa walitegemea kati ya watu 20,000 na 30,000 toka kila kona ya Marekani kuhudhuria maandamano hayo.
Maelfu waliitikia wito wa maandamano hayo wakiwa na mabango mbali mbali kuonyesha upinzani kwa rais Obama.
Waandamanaji wengine walibeba mabango yaliyosema "You lie" wakikumbushia maneno aliyosema seneta wa Arizona toka chama cha Republican, Joe Wilson ambaye alimwambia Obama muongo wakati alipokuwa akisoma hotuba yake kwenye bunge la kongresi la Marekani kuhusiana na mageuzi anayotaka kuyafanya kwenye mfumo wa afya wa Marekani.
Maandamano hayo yaliisha mapema kabla ya muda uliopangwa kutokana na idadi ya watu kuwa kubwa sana kuliko uwezo wa eneo hilo.
Inakadiriwa watu milioni mbili toka kona mbali mbali za Marekani walihudhuria maandamano hayo
Maelfu Waandamana Marekani Kupinga Serikali ya Obama
Maelfu waliojitokeza jana kupinga utawala wa Obama
Maelfu ya watu wakibeba mabango yanayopinga utawala wa rais Obama na mageuzi yake katika mfumo wa afya anayotaka kuyafanya, waliandamana jana hadi katika maeneo ya ikulu ya Marekani.
"Utoaji mimba sio mageuzi katika Afya" lilisema bango moja huku bango jingine lililobebwa na mhamiaji nchini Marekani toka Ukraine lilisema "Nilishauchoka ujamaa kwenye muungano wa soviet USSR".
Mtoto Quinn Ryan, 11, alisimama katikati ya mtaa wa Pennsylvania Avenue, karibu na sehemu ambayo Obama na mkewe Michelle walitembea siku ile yenye baridi wakati Obama alipoapishwa kuwa rais wa kwanza mweusi wa Marekani.
Ryan alikuwa amebeba bango linalosema "Nimezaliwa bure, nitalipishwa kodi mpaka nitakapofariki".
"Hali mbaya ya uchumi imeathiri nyumba nyingi, imetubidi tuandamane ili hali isiwe mbaya zaidi" alisema dada yake Ryan mwenye umri wa miaka 13 ambaye naye alikuwa amebeba bango lake tofauti.
Maandamano hayo yalilenga kupinga utawala wa rais Obama na kukishtumu chama cha democratic kwa kutaka kuigeuza Marekani nchi ya kijamaa.
Maandamano hayo yaliandaliwa Freedomworks, taasisi inayopigania kushushwa kwa viwango vya kodi na uchumi huria ikipinga mabadiliko ambayo rais Obama anataka kuyafanya katika masuala ya bima katika mfumo wa afya wa Marekani.
Waandaaji wa maanandamano hayo walisema awali katikati ya wiki kuwa walitegemea kati ya watu 20,000 na 30,000 toka kila kona ya Marekani kuhudhuria maandamano hayo.
Maelfu waliitikia wito wa maandamano hayo wakiwa na mabango mbali mbali kuonyesha upinzani kwa rais Obama.
Waandamanaji wengine walibeba mabango yaliyosema "You lie" wakikumbushia maneno aliyosema seneta wa Arizona toka chama cha Republican, Joe Wilson ambaye alimwambia Obama muongo wakati alipokuwa akisoma hotuba yake kwenye bunge la kongresi la Marekani kuhusiana na mageuzi anayotaka kuyafanya kwenye mfumo wa afya wa Marekani.
Maandamano hayo yaliisha mapema kabla ya muda uliopangwa kutokana na idadi ya watu kuwa kubwa sana kuliko uwezo wa eneo hilo.
Inakadiriwa watu milioni mbili toka kona mbali mbali za Marekani walihudhuria maandamano hayo