Hotuba ya obama - machache yaliyonigusa

Kamakabuzi

JF-Expert Member
Dec 3, 2007
2,861
1,302
Pamoja na hotuba yote kuwa nzuri, yafuatayo yamegusa sana matarajio yangu kwake.
1.To those who cling to power through corruption and deceit and the silencing of dissent, know that you are on the wrong side of history; but that we will extend a hand if you are willing to unclench your fist.
Hapa anawaonya mfisadi popote walipo kuwa wapo katika upande mbaya wa historia yaani hawatavumiliwa.
Ukiangalia nchi nyingi za Africa hili ndilo tatizo letu kubwa. Viongozi wanaingia madarakani kwa kutumia ufisadi, na hata pale wanapojitia kuachia madaraka basi huwaachia wenzao watakaowalinda na ufisadi walioufanya wakiwa madarakani na wao kuendeleza ufisadi ule ule. Mifano ni mingi Tanzania, Kenya, Uganda nk. Hawa chamtema kuni chaja maana Obama anataka dunia nzima kwa ujumla iwe mahali bora pa kuishi kwa kila mtu

2.To the people of poor nations, we pledge to work alongside you to make your farms flourish and let clean waters flow; to nourish starved bodies and feed hungry minds. And to those nations like ours that enjoy relative plenty, we say we can no longer afford indifference to suffering outside our borders; nor can we consume the world's resources without regard to effect. For the world has changed, and we must change with it.
Obama hatavumilia mateso kwa wanaoishi nje ya Marekani na anasisitiza kuwa hatavumilia kuona Amerika inatumia raslimali za dunia bila kujali madhara yake. Anapounganisha hili na nchi maskini naona anayaonya makampuni ya Marekani kuhusu udanganyifu yanaoufanya, Haya ndiyo yanachochea migogoro Afrika kwa kuchota raslimali bila kujali ali mradi wamekubaliana na viongozi wa nchi husika kwa kuwahonga. Mifano ni mingi, angalia mikataba yetu ya madini, angalia vita kule DRC nk.
 
Back
Top Bottom