Sudysoko
JF-Expert Member
- Aug 19, 2015
- 449
- 180
Hotuba ya Magufuli
Mchague MAGUFULI kwa maendeleo ya Tanzania.
#HapaKaziTu
Katika Sekta ya ELIMU:
"Tutatekeleza Sera ya Mfumo mpya wa Elimu unaotaka Elimu ya msingi iishie kidato cha Nne na iwe BURE. Itahakikisha Tatizo la Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya juu linashughulikiwa kikamilifu na kuondoa usumbufu ambao ambao Wanafunzi wamekuwa wakiupata ikiwa ni pamoja na kupata fedha kwa wakati ili muda wao wautumie kwa kusoma na sio migomo.
Aidha kwa kushirikiana na mifuko ya pensheni na Sekta Binafsi tutajenga hosteli za kutosha ili kuwaondoa wanafunzi adha ya malazi.Kuhusu masilahi ya Walimu, napenda mfahamu kuwa mimi pia ni mwalimu,hakuna mgombea anayezijua adha zenu kama mimi. Matatizo mliyonayo hata mimi nilipata, nayajua.
SITAWAANGUSHA; Mnatufundishia Wataalamu katika Sekta mbalimbali,nitawapa kipaumbele. Lazima tuboreshe masilahi yenu, tutatekeleza kikamiifu Muundo mpya wa Walimu na kuimarisha Tume ya Utumishi wa Walimu.
Mazingira ya kazi yataboreshwa.Ujenzi wa nyumba za walimu utatoa kipaumbele katika shule za vijijini." JP Magufuli.
Mchague MAGUFULI kwa maendeleo ya Tanzania.
#HapaKaziTu