Hongereni sana wafanyabiashara wa Kariakoo na nchi nzima, mmetuonesha njia Watanzania

fazili

JF-Expert Member
Jun 10, 2011
13,819
18,563
Watu wengi wana dhana potofu kuwa wafanyabiashara ni vilaza, wahuni, watu wasiojitambua, hawajui sheria wala kujieleza. Kinyume na dhana hii potofu wafanyabiashara mmeonesha weledi mkubwa (professionalism) kwa jinsi mlivyowasilisha na kudai ufumbuzi wa kero zenu mbele ya serikali.

Mmekuwa wazi na kueleza kero zenu mbele ya waziri mkuu bila woga wowote na bila kumumunya maneno na kuonesha kuwa nyie ni kada muhimu sana na yenye nguvu katika jamii yetu.

Nimevutiwa sana kwa jinsi mlivyoonesha kutoridhishwa kwenu na utendaji mbovu wa waziri wa fedha Mwigulu Nchemba na waziri wa viwanda na biashara Ashatu Kijazi na hamkusita kuwasema mbele ya waziri mkuu bila kupepesa macho!

Mmeonesha ushirikiano mkubwa na jinsi ya kudai haki na mazingira mazuri makazini. Watanzania hususani wafanyakazi katika sekta mbalimbali tunapaswa kuiga weledi na ujasiri huu kudai maslahi yetu.

Watanzania tutambue kuwa kero zetu hazitashughulikiwa bila kuunganisha nguvu zetu na kudai mabadiliko kama walivyofanya wafanyabiashara.

Hongereni wafanyabiashara kwa kuonesha njia!
 
Kuna mwalimu ana guts za kuongea kwa waziri mkuu kama walivyoongea wafanyabiashara?
Hapana.

Wafanyabiashara wanashikilia mpini, Gavo inashikilia makali, hapo lazima iombe poo.

Mwalimu anashikilia makali, Gavo inashikilia mpini, Mwalimu lazima aombe poo
 
Nilisikia mkisema nchi imefunguliwa,

Uhuru wa kibiashara tele

Uchumi unakua

Jana nmeshangaa kuambiwa eti wafanyabiashara wa nchi jirani wanahama! Wanahamaje nchi imefunguliwa
 
Hapana.

Wafanyabiashara wanashikilia mpini, Gavo inashikilia makali, hapo lazima iombe poo.

Mwalimu anashikilia makali, Gavo inashikilia mpini, Mwalimu lazima aombe poo
Hii ni usema kuwa wafanyakazi watapata tabu sana kutetea maslahi yao.

Hakuna mwalimu au nurse angepewa airtime ya jana ya kujiachia kwa muda wote ule, eti PM anasikiliza kero zao.

Kumbuka hawa jamaa waligoma kwenda sijui Dom kuwasikiliza wakubwa hawa..leo kuna rais wa chama chochote atamgomea waziri kwenda mahali waziri huyo alipo? There's is still long journey to go.
 
Nimevutiwa sana kwa jinsi mlivyoonesha kutoridhishwa kwenu na utendaji mbovu wa waziri wa fedha Mwigulu Nchemba na waziri wa viwanda na biashara Ashatu Kijazi na hamkusita kuwasema mbele ya waziri mkuu bila kupepesa macho!
 
Hii ni usema kuwa wafanyakazi watapata tabu sana kutetea maslahi yao.

Hakuna mwalimu au nurse angepewa airtime ya jana ya kujiachia kwa muda wote ule, eti PM anasikiliza kero zao.

Kumbuka hawa jamaa waligoma kwenda sijui Dom kuwasikiliza wakubwa hawa..leo kuna rais wa chama chochote atamgomea waziri kwenda mahali waziri huyo alipo? There's is still long journey to go.
Hii ni kawaida, unaponyoshewa Chuma kichwani utatii kila utakaloambiwa.

Walimu na watumishi wengine hawana chuma cha kuinyoshea Gavo kama Wafanyabiashara.

Ikifanywa tathmini ya kodi iliyopotea kwa siku 4 za mgomo, ni kubwa sana. Humo ndio pumzi ya Vigogo(Gavo) iliyopo ndio maana wanatii.
 
Hii ni kawaida, unaponyoshewa Chuma kichwani utatii kila utakaloambiwa.

Walimu na watumishi wengine hawana chuma cha kuinyoshea Gavo kama Wafanyabiashara.

Ikifanywa tathmini ya kodi iliyopotea kwa siku 4 za mgomo, ni kubwa sana. Humo ndio pumzi ya Vigogo(Gavo) iliyopo ndio maana wanatii.
Basi public servants wanalo.
 
Nilisikia mkisema nchi imefunguliwa,

Uhuru wa kibiashara tele

Uchumi unakua

Jana nmeshangaa kuambiwa eti wafanyabiashara wa nchi jirani wanahama! Wanahamaje nchi imefunguliwa
Nchi imefunguliwa ili Wafanyabiashara walioko ndani watoke nje kwenda Kenya au Uganda kufungua biashara zao!!!
 
Hii ni kawaida, unaponyoshewa Chuma kichwani utatii kila utakaloambiwa.

Walimu na watumishi wengine hawana chuma cha kuinyoshea Gavo kama Wafanyabiashara.

Ikifanywa tathmini ya kodi iliyopotea kwa siku 4 za mgomo, ni kubwa sana. Humo ndio pumzi ya Vigogo(Gavo) iliyopo ndio maana wanatii.
Ila tuseme ukweli! Wafanyabiashara ndiyo wanawalisha Viongozi pamoja na Watumishi wao wa Umma!!!
 
Watu wengi wana dhana potofu kuwa wafanyabiashara ni vilaza, wahuni, watu wasiojitambua, hawajui sheria wala kujieleza. Kinyume na dhana hii potofu wafanyabiashara mmeonesha weledi mkubwa (professionalism) kwa jinsi mlivyowasilisha na kudai ufumbuzi wa kero zenu mbele ya serikali.

Mmekuwa wazi na kueleza kero zenu mbele ya waziri mkuu bila woga wowote na bila kumumunya maneno na kuonesha kuwa nyie ni kada muhimu sana na yenye nguvu katika jamii yetu.

Nimevutiwa sana kwa jinsi mlivyoonesha kutoridhishwa kwenu na utendaji mbovu wa waziri wa fedha Mwigulu Nchemba na waziri wa viwanda na biashara Ashatu Kijazi na hamkusita kuwasema mbele ya waziri mkuu bila kupepesa macho!

Mmeonesha ushirikiano mkubwa na jinsi ya kudai haki na mazingira mazuri makazini. Watanzania hususani wafanyakazi katika sekta mbalimbali tunapaswa kuiga weledi na ujasiri huu kudai maslahi yetu.

Watanzania tutambue kuwa kero zetu hazitashughulikiwa bila kuunganisha nguvu zetu na kudai mabadiliko kama walivyofanya wafanyabiashara.

Hongereni wafanyabiashara kwa kuonesha njia!
Watanzania sasa wanaanza kujua namna ya kudai haki zao, haki haiombwi bali nadaiwa hata kwa nguvu.
 
hakika wanastahili pongezi wameonyesha umoja wa hali ya juu Mungu saidia siasa na mamluki wasije ingia na kuwavuruga wakaendelea kupata tabu

wana hoja ya msingi na wanaonekana wamevumilia sana shida

kumbe watanzania sio watu wa kuwachezea wakiamua eeeh
 
Back
Top Bottom