Japo hii thread ilitakiwa iende jukwaa la elimu ila nimeona niiweke hapa jukwaa la siasa kutokana na mtajwa hapo juu kuwa mwanasiasa.Nimefika leo Dodoma kuhudhuria mahafali ya mdogo wangu,nlipofika kwenye mahafali nilimuona Mohamed Seif Khatibu akiwa mwanafunzi wa kwanza UDOM kutunikiwa Doctor of philosophy in Kiswahili literature,wanafunzi wengine wawili watatunikiwa kesho.Nimejaribu kuulizia nikaambiwa alikuwa na supervisors watatu ambao ni Prof.Mlacha,Prof Madumla na Prof.Rubagumya.Hii inaonyesha kuwa wanasiasa wengine kama J.Kikwete msipende phd za heshima bali tafuteni kama wengine wanavyorudi darasani.