Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,660
- 46,347
Anna Tibaijuka kuwa Mkurugenzi wa shirika la makazi la umoja wa mataifa kunamfanya kuwa mtu sahihi na makini sana katika suala la makazi na mipango miji. Hakuwa anabahatisha alipoukataa uhuni wa kuwekwa kituo cha mafuta sehemu isiyostahili katika mtaa wake. Wengine tunapaswa kuiga mfano wake, pia anafaa sana kuwa mshauri wa Rais katika mazingira na mipango miji.
Jerry Silaa usirudi nyuma kutaka viwanja vyote vinavyouzwa vipimwe kwanza. Pia kupinga uholela katika ujenzi wa miji ni jambo la kutia moyo sana. Usiishie Dar es Salaam tu, fanya nchi nzima. Hakikisha maafisa ardhi wa wizarani na serikali za mitaa wanafanya kazi zao pia kwani ni kama wamelala usingizi.
Jerry Silaa usirudi nyuma kutaka viwanja vyote vinavyouzwa vipimwe kwanza. Pia kupinga uholela katika ujenzi wa miji ni jambo la kutia moyo sana. Usiishie Dar es Salaam tu, fanya nchi nzima. Hakikisha maafisa ardhi wa wizarani na serikali za mitaa wanafanya kazi zao pia kwani ni kama wamelala usingizi.